< Yoshua 18 >

1 Kusanyiko lote la Waisraeli likakusanyika huko Shilo na kusimamisha Hema la Kukutania. Nchi ikawa chini ya utawala wao,
تمام قوم اسرائیل در شیلوه جمع شدند و خیمهٔ ملاقات را بر پا کردند. هر چند آنها بر تمام سرزمین مسلط شده بودند، ولی هنوز هفت قبیله باقی مانده بودند که ملکی نداشتند.
2 lakini palikuwa bado makabila saba ya Israeli ambayo yalikuwa hayajapokea urithi wao.
3 Hivyo Yoshua akawaambia Waisraeli, “Je, mtasubiri hata lini ili kuingia kumiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa?
پس یوشع به آنها گفت: «تا کی می‌خواهید سهل‌انگاری کنید؟ چرا نمی‌روید و زمینهایی را که خداوند، خدای اجدادتان به شما داده است، تصرف نمی‌کنید؟
4 Chagueni watu watatu kutoka kwenye kila kabila. Nitawatuma hao watu kukagua hiyo nchi na kuniandikia mapendekezo ya mgawanyo wa urithi wa kila kabila. Nao watanirudia.
از هر قبیله سه مرد انتخاب کنید. من آنها را می‌فرستم تا آن زمینها را بررسی کنند و از وضع آنها به من گزارش دهند تا بتوانم زمینها را بین شما تقسیم کنم.
5 Mtaigawanya hiyo nchi katika sehemu saba. Yuda atabaki katika eneo lake upande wa kusini na nyumba ya Yosefu katika nchi yake upande wa kaskazini.
آنها باید زمین را به هفت قسمت تقسیم کنند و گزارش آن را برای من بیاورند تا من در حضور خداوند، خدایمان سهم هفت قبیله را به حکم قرعه تعیین نمایم. «قبیلهٔ یهودا و قبیلهٔ یوسف که قبلاً به ترتیب زمینهای جنوب و شمال را گرفته‌اند در همان جا می‌مانند.
6 Baada ya kuandika maelezo ya hizo sehemu saba za nchi, yaleteni kwangu, nami nitawapigia kura kwa kura mbele za Bwana Mungu wetu.
7 Hata hivyo, Walawi hawatakuwa na sehemu miongoni mwenu, kwa maana huduma ya ukuhani kwa Bwana ndio urithi wao. Nao Gadi, Reubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapata urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, ambako Mose mtumishi wa Bwana aliwapa.”
قبیلهٔ لاوی هم از زمین سهمی ندارند، زیرا آنها کاهن هستند و خدمت خداوند سهم ایشان است. قبایل رئوبین و جاد و نصف قبیلهٔ منسی هم که قبلاً سهم خود را در سمت شرقی رود اردن که موسی برای ایشان تعیین نموده بود، گرفته‌اند.»
8 Watu hao walipokuwa wanaondoka kwenda kuandika vizuri kuhusu hiyo nchi, Yoshua akawaagiza, “Nendeni mkakague hiyo nchi na mwandike maelezo kuihusu. Kisha mrudi kwangu, nami nitawapigia kura hapa Shilo mbele za Bwana.”
پس آن افراد رفتند تا زمینها را بررسی کنند و گزارش آن را برای یوشع بیاورند تا او در شیلوه در حضور خداوند سهم هفت قبیله را به حکم قرعه تعیین کند.
9 Ndipo hao watu walipoondoka na kupita katika ile nchi. Wakaandika maelezo yake kwenye kitabu, mji kwa mji, katika sehemu saba na kurudisha taarifa kwa Yoshua huko kambini Shilo.
فرستادگان یوشع مطابق دستوری که یافته بودند عمل کردند. زمینها را به هفت قسمت تقسیم نمودند و نام شهرهای هر قسمت را نوشتند. سپس به اردوگاه شیلوه نزد یوشع بازگشتند.
10 Basi Yoshua akawapigia kura huko Shilo mbele za Bwana, na hapo akagawanya ile nchi kwa Waisraeli kufuatana na mgawanyo wa kabila zao.
یوشع در حضور خداوند قرعه انداخت و زمینها را بین آن هفت قبیله تقسیم کرد.
11 Kura iliangukia kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo. Eneo lao walilogawiwa lilikuwa kati ya kabila la Yuda na la Yosefu.
اولین قرعه به نام بنیامین درآمد. زمین خاندانهای این قبیله، بین زمینهای دو قبیلهٔ یهودا و یوسف قرار داشت.
12 Upande wa kaskazini mpaka wao ulianzia pale Yordani, kupitia kaskazini ya mteremko wa Yeriko na kuendelea magharibi kuingia katika nchi ya vilima, ukitokea kwenye jangwa la Beth-Aveni.
مرز آنها در شمال از رود اردن شروع شده، به طرف شمال اریحا بالا می‌رفت. سپس از وسط کوهستان گذشته، به صحرای بیت‌آون در غرب می‌رسید.
13 Kutoka hapo ulikatiza kwenye mteremko wa kusini mwa Luzu (yaani Betheli) na kushuka hadi Ataroth-Adari katika kilima kusini mwa Beth-Horoni ya Chini.
بعد به طرف جنوب لوز (که همان بیت‌ئیل است) کشیده شده، به طرف عطاروت ادار که در منطقهٔ کوهستانی جنوب بیت‌حورون پایین واقع است سرازیر می‌شد.
14 Kutoka kilima kinachotazamana na Beth-Horoni upande wa kusini mpaka ule ukazunguka kusini kufuatia upande wa magharibi, na ukatokezea Kiriath-Baali (yaani Kiriath-Yearimu), mji wa watu wa Yuda. Huu ndio uliokuwa upande wa magharibi.
مرز غربی از کوهستان جنوب بیت‌حورون به طرف جنوب کشیده شده، به قریۀ بعل (همان قریهٔ یعاریم) که یکی از شهرهای یهوداست می‌رسید.
15 Upande wa kusini mpaka ulianzia kwenye viunga vya Kiriath-Yearimu kwa upande wa magharibi, nao ukatokeza kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa.
مرز جنوبی از انتهای قریهٔ بعل در غرب شروع می‌شد و به طرف چشمه‌های نفتوح کشیده شده،
16 Mpaka ukateremka hadi shefela inayotazamana na Bonde la Ben-Hinomu, kaskazini mwa Bonde la Refaimu. Ukaendelea chini kwenye Bonde la Hinomu sambamba na mteremko wa kusini mwa mji mkubwa wa Wayebusi na kisha hadi En-Rogeli.
از آنجا به دامنهٔ کوهی که مقابل درهٔ هنوم (واقع در شمال درهٔ رفائیم) است، امتداد می‌یافت. سپس، از درهٔ هنوم می‌گذشت و جنوب سرزمین یبوسیان را قطع می‌کرد و به عین روجل می‌رسید.
17 Kisha ukapinda kuelekea kaskazini, ukaenda hadi En-Shemeshi na kuendelea mpaka Gelilothi, inayotazamana na Njia ya Adumimu, ukateremka hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni.
این خط مرزی از عین روجل به طرف شمال به عین شمس می‌رفت و بعد به جلیلوت که در مقابل گذرگاه ادومیم قرار دارد، می‌رسید. سپس به طرف سنگ بوهن (بوهن پسر رئوبین بود) سرازیر شده،
18 Ukaendelea upande wa mteremko wa kaskazini wa Beth-Araba ukateremka hadi Araba.
از شمال زمینی که مقابل درهٔ اردن است می‌گذشت. سپس به درهٔ اردن سرازیر می‌شد
19 Kisha ukaenda mpaka kwenye mteremko wa kaskazini wa Beth-Hogla na kujitokeza kwenye ghuba ya kaskazini ya Bahari ya Chumvi, kwenye maingilio ya Yordani upande wa kusini. Huo ulikuwa mpaka wa kusini.
و از آنجا به سمت شمال بیت‌حجله کشیده می‌شد و به خلیج شمالی دریای مرده که در انتهای جنوبی رود اردن است، منتهی می‌شد. این بود مرز جنوبی.
20 Nayo Yordani ikawa ndio mpaka wa upande wa mashariki. Hii ilikuwa ndiyo mipaka iliyoonyesha urithi wa koo za Benyamini pande zote.
رود اردن، مرز شرقی زمین بنیامین را تشکیل می‌داد. این زمینی است که برای خاندانهای قبیلهٔ بنیامین تعیین گردید.
21 Kabila ya Benyamini, ukoo kwa ukoo, ilikuwa na miji mikubwa ifuatayo: Yeriko, Beth-Hogla, Emeki-Kesisi,
شهرهایی که به خاندانهای قبیلهٔ بنیامین تعلق داشت، از این قرارند: اریحا، بیت‌حُجله، عِیمَق قصیص،
22 Beth-Araba, Semaraimu, Betheli,
بیت‌عربه، صمارایم، بیت‌ئیل،
23 Avimu, Para na Ofra,
عَویم، فاره، عُفرَت،
24 Kefar-Amoni, Ofni, na Geba; miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
کَفَرعمونی، عُفنی و جابع، جمعاً دوازده شهر با روستاهای اطراف.
25 Gibeoni, Rama na Beerothi,
جبعون، رامه، بئیروت،
26 Mispa, Kefira, Moza,
مصفه، کفیره، موصه،
27 Rekemu, Irpeeli, Tarala,
راقم، یرفئیل، تراله،
28 Zela, Elefu, mji wa Wayebusi (yaani Yerusalemu), Gibea na Kiriathi; miji kumi na minne pamoja na vijiji vyake. Huu ndio uliokuwa urithi wa Benyamini kwa ajili ya koo zake.
صیله، آلف، یبوسی (اورشلیم)، جِبعه و قریهٔ یعاریم، جمعاً چهارده شهر با روستاهای اطراف. این بود ملکی که به خاندانهای قبیلهٔ بنیامین داده شد.

< Yoshua 18 >