< Yoshua 18 >
1 Kusanyiko lote la Waisraeli likakusanyika huko Shilo na kusimamisha Hema la Kukutania. Nchi ikawa chini ya utawala wao,
Then the whole assembly of the people of Israel met together at Shiloh. They set up the tent of meeting there and they conquered the land before them.
2 lakini palikuwa bado makabila saba ya Israeli ambayo yalikuwa hayajapokea urithi wao.
There were still seven tribes among the people of Israel whose inheritance had not been assigned.
3 Hivyo Yoshua akawaambia Waisraeli, “Je, mtasubiri hata lini ili kuingia kumiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa?
Joshua said to the people of Israel, “How long will you put off going into the land that Yahweh, the God of your ancestors, has given you?
4 Chagueni watu watatu kutoka kwenye kila kabila. Nitawatuma hao watu kukagua hiyo nchi na kuniandikia mapendekezo ya mgawanyo wa urithi wa kila kabila. Nao watanirudia.
Appoint for yourselves three men from each tribe, and I will send them out. They will set out and survey the land up and down. They will write out a description of it with a view to their inheritances, and then they will come back to me.
5 Mtaigawanya hiyo nchi katika sehemu saba. Yuda atabaki katika eneo lake upande wa kusini na nyumba ya Yosefu katika nchi yake upande wa kaskazini.
They will divide it into seven sections. Judah will remain in their territory on the south, and the house of Joseph will continue in their territory in the north.
6 Baada ya kuandika maelezo ya hizo sehemu saba za nchi, yaleteni kwangu, nami nitawapigia kura kwa kura mbele za Bwana Mungu wetu.
You will describe the land in seven sections and bring the description here to me. I will cast lots for you here before Yahweh our God.
7 Hata hivyo, Walawi hawatakuwa na sehemu miongoni mwenu, kwa maana huduma ya ukuhani kwa Bwana ndio urithi wao. Nao Gadi, Reubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapata urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, ambako Mose mtumishi wa Bwana aliwapa.”
The Levites have no portion among you, for the priesthood of Yahweh is their inheritance. Gad, Reuben, and the half tribe of Manasseh have received their inheritance, beyond Jordan. This is the inheritance that Moses the servant of Yahweh gave them.”
8 Watu hao walipokuwa wanaondoka kwenda kuandika vizuri kuhusu hiyo nchi, Yoshua akawaagiza, “Nendeni mkakague hiyo nchi na mwandike maelezo kuihusu. Kisha mrudi kwangu, nami nitawapigia kura hapa Shilo mbele za Bwana.”
So the men got up and went. Joshua commanded those who went to write the description of the land, saying, “Go up and down in the land and write a description of it and return to me. I will cast lots for you here before Yahweh at Shiloh.”
9 Ndipo hao watu walipoondoka na kupita katika ile nchi. Wakaandika maelezo yake kwenye kitabu, mji kwa mji, katika sehemu saba na kurudisha taarifa kwa Yoshua huko kambini Shilo.
The men left and walked up and down in the land and wrote a description of it in a scroll by its cities in seven sections, listing the cities in each section. Then they returned to Joshua in the camp at Shiloh.
10 Basi Yoshua akawapigia kura huko Shilo mbele za Bwana, na hapo akagawanya ile nchi kwa Waisraeli kufuatana na mgawanyo wa kabila zao.
Then Joshua cast lots for them at Shiloh before Yahweh. It was there that Joshua assigned the land to the people of Israel, and to each was given his portion of the land.
11 Kura iliangukia kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo. Eneo lao walilogawiwa lilikuwa kati ya kabila la Yuda na la Yosefu.
The assignment of land for the tribe of Benjamin clan by clan. The territory of their assigned land was located between the descendants of Judah and the descendants of Joseph.
12 Upande wa kaskazini mpaka wao ulianzia pale Yordani, kupitia kaskazini ya mteremko wa Yeriko na kuendelea magharibi kuingia katika nchi ya vilima, ukitokea kwenye jangwa la Beth-Aveni.
On the north side, their border began at the Jordan. The border went up to the ridge north of Jericho, and then up through the hill country westward. There it reached the wilderness of Beth Aven.
13 Kutoka hapo ulikatiza kwenye mteremko wa kusini mwa Luzu (yaani Betheli) na kushuka hadi Ataroth-Adari katika kilima kusini mwa Beth-Horoni ya Chini.
From there the border passed along south in the direction of Luz (the same place as Bethel). Then the border went down to Ataroth Addar, by the mountain that lies south of Beth Horon.
14 Kutoka kilima kinachotazamana na Beth-Horoni upande wa kusini mpaka ule ukazunguka kusini kufuatia upande wa magharibi, na ukatokezea Kiriath-Baali (yaani Kiriath-Yearimu), mji wa watu wa Yuda. Huu ndio uliokuwa upande wa magharibi.
The boundary then went in another direction: On the western side it turned toward the south, heading toward the mountain across from Beth Horon. This boundary ended at Kiriath Baal (that is, Kiriath Jearim), a city that belonged to the tribe of Judah. This formed the border on the western side.
15 Upande wa kusini mpaka ulianzia kwenye viunga vya Kiriath-Yearimu kwa upande wa magharibi, nao ukatokeza kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa.
The south side began just outside of Kiriath Jearim. The border went from there to Ephron, to the spring of the waters of Nephtoah.
16 Mpaka ukateremka hadi shefela inayotazamana na Bonde la Ben-Hinomu, kaskazini mwa Bonde la Refaimu. Ukaendelea chini kwenye Bonde la Hinomu sambamba na mteremko wa kusini mwa mji mkubwa wa Wayebusi na kisha hadi En-Rogeli.
The boundary then went down to the border of the mountain which was opposite the Valley of Ben Hinnom, which was at the northern end of the Valley of Rephaim. It then went down to the Valley of Hinnom, south of the slope of the Jebusites, and continued down to En Rogel.
17 Kisha ukapinda kuelekea kaskazini, ukaenda hadi En-Shemeshi na kuendelea mpaka Gelilothi, inayotazamana na Njia ya Adumimu, ukateremka hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni.
It turned northward, going in the direction of En Shemesh, and from there it went out to Geliloth, which was opposite the ascent of Adummim. Then it went down to the Stone of Bohan the son of Reuben.
18 Ukaendelea upande wa mteremko wa kaskazini wa Beth-Araba ukateremka hadi Araba.
It passed on to the north of the shoulder of Beth Arabah and down to the Arabah.
19 Kisha ukaenda mpaka kwenye mteremko wa kaskazini wa Beth-Hogla na kujitokeza kwenye ghuba ya kaskazini ya Bahari ya Chumvi, kwenye maingilio ya Yordani upande wa kusini. Huo ulikuwa mpaka wa kusini.
The border passed on to the north shoulder of Beth Hoglah. The border ended at the north bay of the Salt Sea, at the southern end of the Jordan. This was the boundary on the south.
20 Nayo Yordani ikawa ndio mpaka wa upande wa mashariki. Hii ilikuwa ndiyo mipaka iliyoonyesha urithi wa koo za Benyamini pande zote.
The Jordan formed its border on the eastern side. This was the inheritance of the tribe of Benjamin, and it was given clan by clan, border after border, all around.
21 Kabila ya Benyamini, ukoo kwa ukoo, ilikuwa na miji mikubwa ifuatayo: Yeriko, Beth-Hogla, Emeki-Kesisi,
Now the cities of the tribe of Benjamin, clan by clan, had these cities: Jericho, Beth Hoglah, Emek Keziz,
22 Beth-Araba, Semaraimu, Betheli,
Beth Arabah, Zemaraim, Bethel,
24 Kefar-Amoni, Ofni, na Geba; miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
Kephar Ammoni, Ophni, and Geba. There were twelve cities, including their villages.
25 Gibeoni, Rama na Beerothi,
There were also the cities of Gibeon, Ramah, Beeroth,
27 Rekemu, Irpeeli, Tarala,
Rekem, Irpeel, Taralah,
28 Zela, Elefu, mji wa Wayebusi (yaani Yerusalemu), Gibea na Kiriathi; miji kumi na minne pamoja na vijiji vyake. Huu ndio uliokuwa urithi wa Benyamini kwa ajili ya koo zake.
Zelah, Haeleph, Jebus (the same as Jerusalem), Gibeah, and Kiriath. There were fourteen cities, including their villages. This was the inheritance of Benjamin for their clans.