< Yoshua 17 >

1 Huu ndio mgawo wa kabila la Manase kama mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, yaani kwa ajili ya Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase. Makiri alikuwa baba wa Wagileadi, ambao walipokea Gileadi na Bashani kwa sababu Wamakiri walikuwa askari wakuu.
Il y eut aussi un sort pour la Tribu de Manassé qui fut le premier-né de Joseph. Quant à Makir premier-né de Manassé, [et] père de Galaad, parce qu'il fut un homme belliqueux, il eut Galaad et Basan.
2 Kwa hiyo mgawo huu ulikuwa kwa ajili ya watu wa Manase waliokuwa wamebaki, ambao ni koo za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Shekemu, Heferi na Shemida. Hawa ndio wanaume wale wengine wa uzao wa Manase mwana wa Yosefu kwa koo zao.
Puis le reste des enfants de Manassé eut [ce sort], selon ses familles; [savoir] les enfants d'Abihézer, les enfants de Helek, les enfants d'Asriël, les enfants de Sekem, les enfants de Hépher, et les enfants de Semidah. Ce sont là les enfants mâles de Manassé fils de Joseph, selon leurs familles.
3 Basi Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase hakuwa na wana waume ila mabinti tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.
Or Tselophcad fils de Hépher fils de Galaad, fils de Makir, fils de Manassé, n'eut point de fils, mais des filles; et ce sont ici leurs noms, Mahla, Noha, Hogla, Milca et Tirtsa;
4 Wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi, wakasema: “Bwana alimwagiza Mose atupatie urithi miongoni mwa ndugu zetu.” Kwa hiyo Yoshua akawapa urithi pamoja na ndugu wa baba yao, kufuatana na agizo la Bwana.
Lesquelles vinrent se présenter devant Eléazar le Sacrificateur, et devant Josué, fils de Nun, et devant les principaux [du peuple], en disant: L'Eternel a commandé à Moïse qu'on nous donnât un héritage parmi nos frères; c'est pourquoi on leur donna un héritage parmi les frères de leur père, selon le commandement de l'Eternel.
5 Fungu la Manase lilikuwa na sehemu kumi za nchi, licha ya Gileadi na Bashani mashariki mwa Yordani,
Et dix portions échurent à Manassé, outre le pays de Galaad et de Basan, qui étaient au delà du Jourdain.
6 kwa sababu wale binti za kabila la Manase walipokea urithi miongoni mwa wana wa kiume. Nchi ya Gileadi ilikuwa mali ya wazao wa Manase waliobaki.
Car les filles de Manassé eurent un héritage parmi ses enfants; et le pays de Galaad fut pour le reste des enfants de Manassé.
7 Eneo la Manase lilienea kuanzia Asheri hadi Mikmeta mashariki mwa Shekemu. Mpaka ule ulielekea upande wa kusini kutoka pale kujumuisha watu walioishi En-Tapua.
Or la frontière de Manassé fut du côté d'Aser, venant à Micmethah, qui était au devant de Sichem; puis cette frontière devait aller à main droite vers les habitants de Hen-Tappuah.
8 (Nchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini Tapua yenyewe iliyo mpakani mwa nchi ya Manase ilikuwa ya Waefraimu.)
Or le pays de Tappuah appartenait à Manassé; mais Tappuah qui était près des confins de Manassé, appartenait aux enfants d'Ephraïm.
9 Kisha mpaka ule uliendelea kuelekea kusini hadi Bonde la Kana. Kulikuwepo miji ya Efraimu iliyokuwa miongoni mwa miji ya Manase, lakini mpaka wa Manase ulikuwa upande wa kaskazini wa lile bonde na kuishia kwenye bahari.
De là cette frontière devait descendre au torrent de Kana, tirant vers le Midi du torrent. Ces villes-là sont à Ephraïm parmi les villes de Manassé. Au reste, la frontière de Manassé était au côté du Septentrion du torrent, et ses extrémités se devaient rendre à la mer.
10 Nchi ya kusini ilikuwa ya Efraimu, na ile iliyokuwa upande wa kaskazini ilikuwa ya Manase. Eneo la Manase lilifika bahari na ikapakana na Asheri upande wa kaskazini, na Isakari upande wa mashariki.
Ce qui était vers le Midi était à Ephraïm, et ce qui était vers le Septentrion, était à Manassé, et il avait la mer pour sa borne; et, du côté du Septentrion [les frontières] se rencontraient en Aser, et en Issacar, du côté d'Orient.
11 Katika Isakari na Asheri Manase alikuwa na miji pia: Beth-Shani, Ibleamu na watu wa Dori, Endori, Taanaki na Megido, pamoja na vijiji vyote vinavyohusika na miji hiyo (ya tatu katika orodha ni Nafothi).
Car Manassé eut aux quartiers d'Issacar et d'Aser, Beth-séan, et les villes de son ressort; et Jibléham, et les villes de son ressort; et les habitants de Dor, et les villes de son ressort; et les habitants de Hendor, et les villes de son ressort; et les habitants de Tahanac, et les villes de son ressort; et les habitants de Meguiddo, et les villes de son ressort, qui sont trois contrées.
12 Lakini Wamanase hawakuweza kuimiliki miji hii, kwa kuwa Wakanaani walikazana kuishi katika maeneo hayo.
Au reste, les enfants de Manassé ne purent point déposséder [les habitants] de ces villes-là, mais les Cananéens osèrent demeurer dans le même pays.
13 Hata hivyo, Waisraeli walivyoendelea kupata nguvu waliwatumikisha Wakanaani na kuwatia katika kazi za kulazimishwa, lakini hawakuwafukuza kabisa.
Mais depuis que les enfants d'Israël se furent fortifiés, ils rendirent les Cananéens tributaires; toutefois ils ne les dépossédèrent point entièrement.
14 Watu wa Yosefu wakamwambia Yoshua, “Kwa nini umetupa sisi mgawo mmoja tu na sehemu moja tu kuwa urithi? Sisi tu watu wengi sana, na Bwana ametubariki kwa wingi.”
Or les enfants de Joseph parlèrent à Josué, en disant: Pourquoi m'as-tu donné en héritage un seul lot, et une seule portion, vu que je suis un grand peuple, tant l'Eternel m'a béni jusqu'à présent?
15 Yoshua akajibu, “Kama ninyi ni wengi sana, na kama nchi ya vilima ya Efraimu ni ndogo sana kwenu, pandeni msituni mkafyeke eneo kwa ajili yenu wenyewe huko kwenye nchi ya Waperizi na Warefai.”
Et Josué leur dit: Si tu es un si grand peuple, monte à la forêt, et coupe-la, pour te faire place au pays des Phéréziens et des Réphaïms, si la montagne d'Ephraïm est trop étroite pour toi.
16 Watu wa Yosefu wakajibu, “Hiyo nchi ya vilima haitutoshi, nao Wakanaani wote wanaoishi katika tambarare wanayo magari ya vita ya chuma, wote wa Beth-Shani na miji yake, na wale walio katika Bonde la Yezreeli.”
Et les enfants de Joseph répondirent: Cette montagne ne sera pas suffisante pour nous, et tous les Cananéens qui habitent au pays de la vallée, ont des chariots de fer, pour ceux qui habitent à Beth-séan, et aux villes de son ressort, et pour ceux qui habitent dans la vallée de Jizrehel.
17 Lakini Yoshua akanena na nyumba ya Yosefu, yaani Efraimu na Manase: “Ninyi ni wengi sana na wenye nguvu sana. Hamtakuwa na mgawo mmoja tu,
Josué donc parla à la maison de Joseph, [savoir] à Ephraïm et à Manassé, en disant: Tu es un grand peuple, et tu as de grandes forces, tu n'auras pas une portion seule.
18 bali pia nchi hii ya kilima yenye msitu. Ifyekeni, nayo mipaka yake itakuwa yenu umbali mtakaoweza kufika. Ingawa Wakanaani wana magari ya chuma, nao wana nguvu, mwaweza kuwafukuza humo.”
Car tu auras la montagne; [et] parce que c'est une forêt, tu la couperas, et ses extrémités t'appartiendront; car tu en déposséderas les Cananéens, quoiqu'ils aient des chariots de fer, et qu ils soient puissants.

< Yoshua 17 >