< Yoshua 17 >

1 Huu ndio mgawo wa kabila la Manase kama mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, yaani kwa ajili ya Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase. Makiri alikuwa baba wa Wagileadi, ambao walipokea Gileadi na Bashani kwa sababu Wamakiri walikuwa askari wakuu.
Et le lot échut à la tribu de Manassé (or il était le premier-né de Joseph), à Makir, premier-né de Manassé, père de Galaad; comme il était un homme de guerre, Galaad et Basan furent à lui.
2 Kwa hiyo mgawo huu ulikuwa kwa ajili ya watu wa Manase waliokuwa wamebaki, ambao ni koo za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Shekemu, Heferi na Shemida. Hawa ndio wanaume wale wengine wa uzao wa Manase mwana wa Yosefu kwa koo zao.
Et [le lot] échut aux autres fils de Manassé, selon leurs familles, aux fils d’Abiézer, et aux fils de Hélek, et aux fils d’Asriel, et aux fils de Sichem, et aux fils de Hépher, et aux fils de Shemida. Ce sont là les fils de Manassé, fils de Joseph, les mâles, selon leurs familles.
3 Basi Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase hakuwa na wana waume ila mabinti tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.
Et Tselophkhad, fils de Hépher, fils de Galaad, fils de Makir, fils de Manassé, n’eut point de fils, mais seulement des filles; et ce sont ici les noms de ses filles: Makhla, et Noa, Hogla, Milca, et Thirtsa;
4 Wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi, wakasema: “Bwana alimwagiza Mose atupatie urithi miongoni mwa ndugu zetu.” Kwa hiyo Yoshua akawapa urithi pamoja na ndugu wa baba yao, kufuatana na agizo la Bwana.
et elles se présentèrent devant Éléazar, le sacrificateur, et devant Josué, fils de Nun, et devant les princes, disant: L’Éternel a commandé à Moïse de nous donner un héritage au milieu de nos frères. Et [Josué] leur donna, selon le commandement de l’Éternel, un héritage au milieu des frères de leur père.
5 Fungu la Manase lilikuwa na sehemu kumi za nchi, licha ya Gileadi na Bashani mashariki mwa Yordani,
Et il échut dix parts à Manassé, outre le pays de Galaad et de Basan, qui est au-delà du Jourdain;
6 kwa sababu wale binti za kabila la Manase walipokea urithi miongoni mwa wana wa kiume. Nchi ya Gileadi ilikuwa mali ya wazao wa Manase waliobaki.
car les filles de Manassé reçurent un héritage au milieu de ses fils; et le pays de Galaad fut pour les autres fils de Manassé.
7 Eneo la Manase lilienea kuanzia Asheri hadi Mikmeta mashariki mwa Shekemu. Mpaka ule ulielekea upande wa kusini kutoka pale kujumuisha watu walioishi En-Tapua.
Et le territoire de Manassé allait d’Aser à Micmethath, qui est devant Sichem; et la frontière allait à droite vers les habitants d’En-Tappuakh.
8 (Nchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini Tapua yenyewe iliyo mpakani mwa nchi ya Manase ilikuwa ya Waefraimu.)
La campagne de Tappuakh était à Manassé; mais Tappuakh, sur la frontière de Manassé, était aux fils d’Éphraïm.
9 Kisha mpaka ule uliendelea kuelekea kusini hadi Bonde la Kana. Kulikuwepo miji ya Efraimu iliyokuwa miongoni mwa miji ya Manase, lakini mpaka wa Manase ulikuwa upande wa kaskazini wa lile bonde na kuishia kwenye bahari.
Et la frontière descendait au torrent de Kana, au midi du torrent. Ces villes-là étaient à Éphraïm, au milieu des villes de Manassé. Et le territoire de Manassé était au nord du torrent, et aboutissait à la mer.
10 Nchi ya kusini ilikuwa ya Efraimu, na ile iliyokuwa upande wa kaskazini ilikuwa ya Manase. Eneo la Manase lilifika bahari na ikapakana na Asheri upande wa kaskazini, na Isakari upande wa mashariki.
Le midi était à Éphraïm, et le nord à Manassé, et la mer était sa frontière; et au nord, ils touchaient à Aser, et à l’orient, à Issacar.
11 Katika Isakari na Asheri Manase alikuwa na miji pia: Beth-Shani, Ibleamu na watu wa Dori, Endori, Taanaki na Megido, pamoja na vijiji vyote vinavyohusika na miji hiyo (ya tatu katika orodha ni Nafothi).
Et Manassé avait, dans Issacar et dans Aser, Beth-Shean et les villages de son ressort, et Jibleam et les villages de son ressort, et les habitants de Dor et les villages de son ressort, et les habitants d’En-Dor et les villages de son ressort, et les habitants de Thaanac et les villages de son ressort, et les habitants de Meguiddo et les villages de son ressort: les trois districts montueux.
12 Lakini Wamanase hawakuweza kuimiliki miji hii, kwa kuwa Wakanaani walikazana kuishi katika maeneo hayo.
Mais les fils de Manassé ne purent pas déposséder [les habitants de] ces villes-là, et le Cananéen voulut habiter dans ce pays.
13 Hata hivyo, Waisraeli walivyoendelea kupata nguvu waliwatumikisha Wakanaani na kuwatia katika kazi za kulazimishwa, lakini hawakuwafukuza kabisa.
Et il arriva que, quand les fils d’Israël furent devenus forts, ils rendirent le Cananéen tributaire; mais ils ne le dépossédèrent pas entièrement.
14 Watu wa Yosefu wakamwambia Yoshua, “Kwa nini umetupa sisi mgawo mmoja tu na sehemu moja tu kuwa urithi? Sisi tu watu wengi sana, na Bwana ametubariki kwa wingi.”
Et les fils de Joseph parlèrent à Josué, disant: Pourquoi m’as-tu donné en héritage un seul lot et une seule part, à moi qui suis un peuple nombreux, selon que l’Éternel m’a béni jusqu’à présent?
15 Yoshua akajibu, “Kama ninyi ni wengi sana, na kama nchi ya vilima ya Efraimu ni ndogo sana kwenu, pandeni msituni mkafyeke eneo kwa ajili yenu wenyewe huko kwenye nchi ya Waperizi na Warefai.”
Et Josué leur dit: Si tu es un peuple nombreux, monte à la forêt, et coupe-la pour t’y [faire de la place] dans le pays des Phéréziens et des Rephaïm, si la montagne d’Éphraïm est trop étroite pour toi.
16 Watu wa Yosefu wakajibu, “Hiyo nchi ya vilima haitutoshi, nao Wakanaani wote wanaoishi katika tambarare wanayo magari ya vita ya chuma, wote wa Beth-Shani na miji yake, na wale walio katika Bonde la Yezreeli.”
Et les fils de Joseph dirent: Nous ne pouvons pas acquérir la montagne, et il y a des chars de fer chez tous les Cananéens qui habitent le pays de la vallée, chez ceux de Beth-Shean et des villages de son ressort, et chez ceux de la vallée de Jizreël.
17 Lakini Yoshua akanena na nyumba ya Yosefu, yaani Efraimu na Manase: “Ninyi ni wengi sana na wenye nguvu sana. Hamtakuwa na mgawo mmoja tu,
Et Josué parla à la maison de Joseph, à Éphraïm et à Manassé, disant: Tu es un peuple nombreux, et tu as une grande puissance; tu n’auras pas un seul lot,
18 bali pia nchi hii ya kilima yenye msitu. Ifyekeni, nayo mipaka yake itakuwa yenu umbali mtakaoweza kufika. Ingawa Wakanaani wana magari ya chuma, nao wana nguvu, mwaweza kuwafukuza humo.”
mais la montagne sera à toi; comme c’est une forêt, tu la couperas, et elle sera à toi jusqu’à ses extrémités; car tu déposséderas le Cananéen, quoiqu’il ait des chars de fer [et] qu’il soit fort.

< Yoshua 17 >