< Yoshua 17 >

1 Huu ndio mgawo wa kabila la Manase kama mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, yaani kwa ajili ya Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase. Makiri alikuwa baba wa Wagileadi, ambao walipokea Gileadi na Bashani kwa sababu Wamakiri walikuwa askari wakuu.
Tel fut le sort de la tribu de Manassé, car il était le premier-né de Joseph. Quant à Makir, premier-né de Manassé, père de Galaad, car il était homme de guerre, il eut Galaad et Basan.
2 Kwa hiyo mgawo huu ulikuwa kwa ajili ya watu wa Manase waliokuwa wamebaki, ambao ni koo za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Shekemu, Heferi na Shemida. Hawa ndio wanaume wale wengine wa uzao wa Manase mwana wa Yosefu kwa koo zao.
Ainsi en fut-il pour le reste des fils de Manassé, selon leurs familles: pour les fils d'Abiezer, pour les fils de Helek, pour les fils d'Asriel, pour les fils de Sichem, pour les fils de Hepher, et pour les fils de Shemida. Tels furent les fils mâles de Manassé, fils de Joseph, selon leurs familles.
3 Basi Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase hakuwa na wana waume ila mabinti tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.
Mais Zelophehad, fils de Hépher, fils de Galaad, fils de Makir, fils de Manassé, n'eut pas de fils, mais des filles. Voici les noms de ses filles: Mahla, Noé, Hogla, Milca et Tirza.
4 Wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi, wakasema: “Bwana alimwagiza Mose atupatie urithi miongoni mwa ndugu zetu.” Kwa hiyo Yoshua akawapa urithi pamoja na ndugu wa baba yao, kufuatana na agizo la Bwana.
Elles se présentèrent au sacrificateur Éléazar, à Josué, fils de Nun, et aux princes, en disant: « L'Éternel a ordonné à Moïse de nous donner un héritage parmi nos frères. » C'est pourquoi, selon le commandement de Yahvé, il leur donna un héritage parmi les frères de leur père.
5 Fungu la Manase lilikuwa na sehemu kumi za nchi, licha ya Gileadi na Bashani mashariki mwa Yordani,
Dix parts échurent à Manassé, en plus du pays de Galaad et de Basan, qui est au-delà du Jourdain,
6 kwa sababu wale binti za kabila la Manase walipokea urithi miongoni mwa wana wa kiume. Nchi ya Gileadi ilikuwa mali ya wazao wa Manase waliobaki.
car les filles de Manassé avaient un héritage parmi ses fils. Le pays de Galaad appartenait au reste des fils de Manassé.
7 Eneo la Manase lilienea kuanzia Asheri hadi Mikmeta mashariki mwa Shekemu. Mpaka ule ulielekea upande wa kusini kutoka pale kujumuisha watu walioishi En-Tapua.
La frontière de Manassé allait d'Aser à Micmethath, qui est en face de Sichem. La limite passait à droite, vers les habitants de En Tappuach.
8 (Nchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini Tapua yenyewe iliyo mpakani mwa nchi ya Manase ilikuwa ya Waefraimu.)
Le pays de Tappuach appartenait à Manassé; mais Tappuach, sur la frontière de Manassé, appartenait aux fils d'Éphraïm.
9 Kisha mpaka ule uliendelea kuelekea kusini hadi Bonde la Kana. Kulikuwepo miji ya Efraimu iliyokuwa miongoni mwa miji ya Manase, lakini mpaka wa Manase ulikuwa upande wa kaskazini wa lile bonde na kuishia kwenye bahari.
La limite descendait jusqu'au torrent de Kana, au sud du torrent. Ces villes appartenaient à Éphraïm parmi les villes de Manassé. La limite de Manassé était au nord du torrent, et se terminait à la mer.
10 Nchi ya kusini ilikuwa ya Efraimu, na ile iliyokuwa upande wa kaskazini ilikuwa ya Manase. Eneo la Manase lilifika bahari na ikapakana na Asheri upande wa kaskazini, na Isakari upande wa mashariki.
Au sud, elle appartenait à Éphraïm, au nord, à Manassé, et la mer était sa limite. Ils s'étendaient jusqu'à Aser au nord, et jusqu'à Issacar à l'est.
11 Katika Isakari na Asheri Manase alikuwa na miji pia: Beth-Shani, Ibleamu na watu wa Dori, Endori, Taanaki na Megido, pamoja na vijiji vyote vinavyohusika na miji hiyo (ya tatu katika orodha ni Nafothi).
Manassé avait trois hauteurs dans Issachar, à Asher Beth Shean et ses villes, et Ibleam et ses villes, et les habitants de Dor et ses villes, et les habitants d'Endor et ses villes, et les habitants de Taanach et ses villes, et les habitants de Megiddo et ses villes.
12 Lakini Wamanase hawakuweza kuimiliki miji hii, kwa kuwa Wakanaani walikazana kuishi katika maeneo hayo.
Les enfants de Manassé ne purent pas chasser les habitants de ces villes, mais les Cananéens demeurèrent dans ce pays.
13 Hata hivyo, Waisraeli walivyoendelea kupata nguvu waliwatumikisha Wakanaani na kuwatia katika kazi za kulazimishwa, lakini hawakuwafukuza kabisa.
Lorsque les enfants d'Israël furent devenus forts, ils soumirent les Cananéens au travail forcé et ne les chassèrent pas complètement.
14 Watu wa Yosefu wakamwambia Yoshua, “Kwa nini umetupa sisi mgawo mmoja tu na sehemu moja tu kuwa urithi? Sisi tu watu wengi sana, na Bwana ametubariki kwa wingi.”
Les fils de Joseph parlèrent à Josué et lui dirent: « Pourquoi m'as-tu donné en héritage un seul lot et une seule part, puisque nous sommes un peuple nombreux et que l'Éternel nous a bénis jusqu'ici? »
15 Yoshua akajibu, “Kama ninyi ni wengi sana, na kama nchi ya vilima ya Efraimu ni ndogo sana kwenu, pandeni msituni mkafyeke eneo kwa ajili yenu wenyewe huko kwenye nchi ya Waperizi na Warefai.”
Josué leur dit: « Si vous êtes un peuple nombreux, montez dans la forêt et défrichez-vous là, dans le pays des Phéréziens et des Rephaïm, car la montagne d'Ephraïm est trop étroite pour vous. »
16 Watu wa Yosefu wakajibu, “Hiyo nchi ya vilima haitutoshi, nao Wakanaani wote wanaoishi katika tambarare wanayo magari ya vita ya chuma, wote wa Beth-Shani na miji yake, na wale walio katika Bonde la Yezreeli.”
Les fils de Joseph dirent: « La montagne ne nous suffit pas. Tous les Cananéens qui habitent le pays de la vallée ont des chars de fer, tant ceux qui sont à Beth-Shean et dans ses villes que ceux qui sont dans la vallée de Jizréel. »
17 Lakini Yoshua akanena na nyumba ya Yosefu, yaani Efraimu na Manase: “Ninyi ni wengi sana na wenye nguvu sana. Hamtakuwa na mgawo mmoja tu,
Josué parla à la maison de Joseph, c'est-à-dire à Ephraïm et à Manassé, et dit: « Vous êtes un peuple nombreux, et vous avez une grande force. Vous n'aurez pas un seul lot,
18 bali pia nchi hii ya kilima yenye msitu. Ifyekeni, nayo mipaka yake itakuwa yenu umbali mtakaoweza kufika. Ingawa Wakanaani wana magari ya chuma, nao wana nguvu, mwaweza kuwafukuza humo.”
mais la montagne sera à vous. Même si c'est une forêt, vous l'abattrez, et son extrémité sera à vous, car vous chasserez les Cananéens, bien qu'ils aient des chars de fer et qu'ils soient puissants. »

< Yoshua 17 >