< Yoshua 17 >

1 Huu ndio mgawo wa kabila la Manase kama mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, yaani kwa ajili ya Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase. Makiri alikuwa baba wa Wagileadi, ambao walipokea Gileadi na Bashani kwa sababu Wamakiri walikuwa askari wakuu.
And it belonged the lot to [the] tribe of Manasseh for he [was] [the] firstborn of Joseph to Makir [the] firstborn of Manasseh [the] father of Gilead for he he was a man of war and it belonged to him Gilead and Bashan.
2 Kwa hiyo mgawo huu ulikuwa kwa ajili ya watu wa Manase waliokuwa wamebaki, ambao ni koo za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Shekemu, Heferi na Shemida. Hawa ndio wanaume wale wengine wa uzao wa Manase mwana wa Yosefu kwa koo zao.
And it belonged to [the] descendants of Manasseh who remained to clans their to [the] descendants of Abiezer and to [the] descendants of Helek and to [the] descendants of Asriel and to [the] descendants of Shechem and to [the] descendants of Hepher and to [the] descendants of Shemida these [were] [the] descendants of Manasseh [the] son of Joseph the males to clans their.
3 Basi Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase hakuwa na wana waume ila mabinti tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.
And to Zelophehad [the] son of Hepher [the] son of Gilead [the] son of Makir [the] son of Manasseh not they belonged to him sons that except daughters and these [are] [the] names of daughters his Mahlah and Noah Hoglah Milcah and Tirzah.
4 Wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi, wakasema: “Bwana alimwagiza Mose atupatie urithi miongoni mwa ndugu zetu.” Kwa hiyo Yoshua akawapa urithi pamoja na ndugu wa baba yao, kufuatana na agizo la Bwana.
And they drew near before Eleazar the priest and before - Joshua [the] son of Nun and before the leaders saying Yahweh he commanded Moses to give to us an inheritance in among brothers our and he gave to them to [the] mouth of Yahweh an inheritance in among [the] brothers of father their.
5 Fungu la Manase lilikuwa na sehemu kumi za nchi, licha ya Gileadi na Bashani mashariki mwa Yordani,
And they fell [the] allotted portions of Manasseh ten apart from [the] land of Gilead and Bashan which [is] from [the] other side of the Jordan.
6 kwa sababu wale binti za kabila la Manase walipokea urithi miongoni mwa wana wa kiume. Nchi ya Gileadi ilikuwa mali ya wazao wa Manase waliobaki.
For [the] daughters of Manasseh they inherited an inheritance in among sons his and [the] land of Gilead it belonged to [the] descendants of Manasseh who remained.
7 Eneo la Manase lilienea kuanzia Asheri hadi Mikmeta mashariki mwa Shekemu. Mpaka ule ulielekea upande wa kusini kutoka pale kujumuisha watu walioishi En-Tapua.
And it was [the] border of Manasseh from Asher Micmethath which [is] on [the] face of Shechem and it goes the border to the south to [the] inhabitants of En Tappuah.
8 (Nchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini Tapua yenyewe iliyo mpakani mwa nchi ya Manase ilikuwa ya Waefraimu.)
To Manasseh it belonged [the] land of Tappuah and Tappuah to [the] border of Manasseh [belonged] to [the] descendants of Ephraim.
9 Kisha mpaka ule uliendelea kuelekea kusini hadi Bonde la Kana. Kulikuwepo miji ya Efraimu iliyokuwa miongoni mwa miji ya Manase, lakini mpaka wa Manase ulikuwa upande wa kaskazini wa lile bonde na kuishia kwenye bahari.
And it goes down the border [the] wadi of Kanah [the] south towards to the wadi cities these [belonged] to Ephraim in among [the] cities of Manasseh and [the] border of Manasseh [was] from [the] north of the wadi and it was extremities its the sea towards.
10 Nchi ya kusini ilikuwa ya Efraimu, na ile iliyokuwa upande wa kaskazini ilikuwa ya Manase. Eneo la Manase lilifika bahari na ikapakana na Asheri upande wa kaskazini, na Isakari upande wa mashariki.
South-ward [belonged] to Ephraim and north-ward [belonged] to Manasseh and it was the sea border its and Asher they touch! from [the] north and Issachar from [the] east.
11 Katika Isakari na Asheri Manase alikuwa na miji pia: Beth-Shani, Ibleamu na watu wa Dori, Endori, Taanaki na Megido, pamoja na vijiji vyote vinavyohusika na miji hiyo (ya tatu katika orodha ni Nafothi).
And it belonged to Manasseh in Issachar and in Asher Beth Shean and daughters its and Ibleam and daughters its and [the] inhabitants of Dor and daughters its and [the] inhabitants of En-dor and daughters its and [the] inhabitants of Taanach and daughters its and [the] inhabitants of Megiddo and daughters its [the] three of Napheth.
12 Lakini Wamanase hawakuweza kuimiliki miji hii, kwa kuwa Wakanaani walikazana kuishi katika maeneo hayo.
And not they were able [the] descendants of Manasseh to take possession of the cities these and he was determined the Canaanite[s] to dwell in the land this.
13 Hata hivyo, Waisraeli walivyoendelea kupata nguvu waliwatumikisha Wakanaani na kuwatia katika kazi za kulazimishwa, lakini hawakuwafukuza kabisa.
And it was that they became strong [the] people of Israel and they made the Canaanite[s] forced labor and certainly not he dispossessed him.
14 Watu wa Yosefu wakamwambia Yoshua, “Kwa nini umetupa sisi mgawo mmoja tu na sehemu moja tu kuwa urithi? Sisi tu watu wengi sana, na Bwana ametubariki kwa wingi.”
And they spoke [the] descendants of Joseph with Joshua saying why? have you given to me an inheritance a lot one and a portion one and I [am] a people numerous to that until thus he has blessed me Yahweh.
15 Yoshua akajibu, “Kama ninyi ni wengi sana, na kama nchi ya vilima ya Efraimu ni ndogo sana kwenu, pandeni msituni mkafyeke eneo kwa ajili yenu wenyewe huko kwenye nchi ya Waperizi na Warefai.”
And he said to them Joshua if [are] a people numerous you go up for yourself the forest towards and you will cut down for yourself there in [the] land of the Perizzite[s] and the Rephaites that it is narrow for you [the] hill country of Ephraim.
16 Watu wa Yosefu wakajibu, “Hiyo nchi ya vilima haitutoshi, nao Wakanaani wote wanaoishi katika tambarare wanayo magari ya vita ya chuma, wote wa Beth-Shani na miji yake, na wale walio katika Bonde la Yezreeli.”
And they said [the] descendants of Joseph not it will be found for us the hill country and chariotry of iron [is] among all the Canaanite[s] who dwells in [the] land of the valley to [those] who [are] in Beth Shean and daughters its and to [those] who [are] in [the] valley of Jezreel.
17 Lakini Yoshua akanena na nyumba ya Yosefu, yaani Efraimu na Manase: “Ninyi ni wengi sana na wenye nguvu sana. Hamtakuwa na mgawo mmoja tu,
And he said Joshua to [the] house of Joseph to Ephraim and to Manasseh saying [are] a people numerous you and strength great [belongs] to you not it will belong to you a lot one.
18 bali pia nchi hii ya kilima yenye msitu. Ifyekeni, nayo mipaka yake itakuwa yenu umbali mtakaoweza kufika. Ingawa Wakanaani wana magari ya chuma, nao wana nguvu, mwaweza kuwafukuza humo.”
For [the] hill country it will belong to you for [is] forest it and you will cut down it and it will belong to you extremities its for you will dispossess the Canaanite[s] for chariotry of iron [belongs] to him that [is] strong he.

< Yoshua 17 >