< Yoshua 16 >

1 Mgawanyo wa Yosefu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli.
Y el límite de la tierra señalada para los hijos de José salió del Jordán en Jericó, en las aguas de Jericó al este, en el desierto, subiendo desde Jericó a través de la región montañosa hasta Bet-el.
2 Ukaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waariki huko Atarothi,
Y sale de Bet-él, a Luz, y hasta el límite de los Arquitas a Atarot;
3 ukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
Y desciende hacia el oeste hasta el límite de los Jafletitas, hasta el límite de Bet-horon, de abajo, hasta Gezer; terminando en el mar.
4 Kwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yosefu, walipokea urithi wao.
Y los hijos de José, Manasés y Efraín, tomaron su heredad.
5 Hili ndilo lilikuwa eneo la Efraimu, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao ulianzia Ataroth-Adari upande wa mashariki hadi Beth-Horoni ya Juu,
Y el límite de la tierra de los hijos de Efraín por parte de sus familias se marcó de esta manera: el límite de su herencia al este era Atarot-adar, a Bet-horon hasta lo más alto;
6 na kuendelea mpaka baharini. Kutoka Mikmeta upande wa kaskazini ulipinda kuelekea mashariki hadi Taanath-Shilo, ukiupita hadi Yanoa upande wa mashariki.
La línea sale hacia el oeste en Micmetat, al norte; luego girando hacia el este hacia Taanat-silo, pasando por el este de Janoa;
7 Kisha uliteremka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara, ukagusa Yeriko na kutokea katika Mto Yordani.
Y desde Janoa hasta Atarot y Naarat, y tocando a Jericó, continúa hasta el río Jordán.
8 Kutoka Tapua mpaka ulikwenda magharibi hadi Bonde la Kana na kuishia baharini. Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Waefraimu, ukoo kwa ukoo.
Desde Tapua, la línea continúa hacia el oeste hasta el río Cana; terminando en el mar. Esta es la herencia de los hijos de Efraín por sus familias;
9 Pia ulijumuisha miji yote na vijiji vyake ambavyo vilitengwa kwa ajili ya Waefraimu ndani ya urithi wa kabila la Manase.
Junto con los pueblos marcados para los hijos de Efraín en la herencia de Manasés, todos los pueblos con sus aldeas.
10 Hawakuwatoa Wakanaani waishio Gezeri; mpaka leo Wakanaani wanaishi miongoni mwa watu wa Efraimu lakini wanatakiwa kufanya kazi ngumu za kulazimishwa.
Y los cananeos que vivían en Gezer no fueron expulsados; pero los cananeos han estado viviendo entre Efraín, hasta hoy, como siervos, haciendo trabajo forzado.

< Yoshua 16 >