< Yoshua 16 >
1 Mgawanyo wa Yosefu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli.
Le sort échut aux enfants de Joseph à partir du Jourdain de Jérico, aux eaux de Jérico vers l'orient, le désert montant de Jérico vers la montagne de Béthel.
2 Ukaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waariki huko Atarothi,
La frontière sortait de Béthel vers Luz, passait par la frontière des Arkiens à Ataroth,
3 ukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
Et descendait à l'occident vers la frontière des Japhlétiens, jusqu'à la frontière de Beth-Horon la basse et jusqu'à Guézer, et aboutissait à la mer.
4 Kwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yosefu, walipokea urithi wao.
Et les enfants de Joseph, Manassé et Éphraïm reçurent leur héritage.
5 Hili ndilo lilikuwa eneo la Efraimu, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao ulianzia Ataroth-Adari upande wa mashariki hadi Beth-Horoni ya Juu,
Or, la frontière des enfants d'Éphraïm, selon leurs familles, la frontière de leur héritage était, à l'orient, Ateroth-Addar, jusqu'à Beth-Horon la haute.
6 na kuendelea mpaka baharini. Kutoka Mikmeta upande wa kaskazini ulipinda kuelekea mashariki hadi Taanath-Shilo, ukiupita hadi Yanoa upande wa mashariki.
Et la frontière sortait vers l'occident à Micmethath, du côté du nord; puis la frontière tournait à l'orient vers Thaanath-Silo, et la dépassait dans la direction de l'orient jusqu'à Janoach.
7 Kisha uliteremka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara, ukagusa Yeriko na kutokea katika Mto Yordani.
Elle descendait ensuite de Janoach à Ataroth, et à Naaratha, touchait à Jérico, et aboutissait au Jourdain.
8 Kutoka Tapua mpaka ulikwenda magharibi hadi Bonde la Kana na kuishia baharini. Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Waefraimu, ukoo kwa ukoo.
De Thappuach la frontière allait vers l'occident jusqu'au torrent de Kana, et aboutissait à la mer. Tel fut l'héritage de la tribu des enfants d'Éphraïm, selon leurs familles,
9 Pia ulijumuisha miji yote na vijiji vyake ambavyo vilitengwa kwa ajili ya Waefraimu ndani ya urithi wa kabila la Manase.
Avec les villes qui furent séparées, pour les enfants d'Éphraïm, au milieu de l'héritage des enfants de Manassé, toutes ces villes et leurs villages.
10 Hawakuwatoa Wakanaani waishio Gezeri; mpaka leo Wakanaani wanaishi miongoni mwa watu wa Efraimu lakini wanatakiwa kufanya kazi ngumu za kulazimishwa.
Toutefois ils ne dépossédèrent point les Cananéens qui habitaient à Guézer; et les Cananéens ont habité au milieu d'Éphraïm jusqu'à ce jour; mais ils ont été rendus tributaires.