< Yoshua 16 >

1 Mgawanyo wa Yosefu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli.
and to come out: extends [the] allotted to/for son: descendant/people Joseph from Jordan Jericho to/for water Jericho east [to] [the] wilderness to ascend: rise from Jericho in/on/with mountain: hill country Bethel Bethel
2 Ukaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waariki huko Atarothi,
and to come out: extends from Bethel Bethel Luz [to] and to pass to(wards) border: area [the] Archite Ataroth
3 ukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
and to go down sea: west [to] to(wards) border: area [the] Japhletite till border: area (Lower) Beth-horon (Lower) Beth-horon Lower (Beth Horon) and till Gezer and to be (outgoing his *Q(K)*) sea [to]
4 Kwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yosefu, walipokea urithi wao.
and to inherit son: descendant/people Joseph Manasseh and Ephraim
5 Hili ndilo lilikuwa eneo la Efraimu, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao ulianzia Ataroth-Adari upande wa mashariki hadi Beth-Horoni ya Juu,
and to be border: area son: descendant/people Ephraim to/for family their and to be border: boundary inheritance their east [to] Ataroth-addar Ataroth-addar till (Upper) Beth-horon (Upper) Beth-horon Upper (Beth Horon)
6 na kuendelea mpaka baharini. Kutoka Mikmeta upande wa kaskazini ulipinda kuelekea mashariki hadi Taanath-Shilo, ukiupita hadi Yanoa upande wa mashariki.
and to come out: extends [the] border: boundary [the] sea [to] [the] Michmethath from north and to turn: turn [the] border: boundary east [to] Taanath-shiloh Taanath-shiloh and to pass [obj] him from east Janoah
7 Kisha uliteremka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara, ukagusa Yeriko na kutokea katika Mto Yordani.
and to go down from Janoah Ataroth and Naarah [to] and to fall on in/on/with Jericho and to come out: extends [the] Jordan
8 Kutoka Tapua mpaka ulikwenda magharibi hadi Bonde la Kana na kuishia baharini. Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Waefraimu, ukoo kwa ukoo.
from Tappuah to go: went [the] border: boundary sea: west [to] torrent: river Kanah and to be outgoing his [the] sea [to] this inheritance tribe son: descendant/people Ephraim to/for family their
9 Pia ulijumuisha miji yote na vijiji vyake ambavyo vilitengwa kwa ajili ya Waefraimu ndani ya urithi wa kabila la Manase.
and [the] city [the] separate place to/for son: descendant/people Ephraim in/on/with midst inheritance son: descendant/people Manasseh all [the] city and village their
10 Hawakuwatoa Wakanaani waishio Gezeri; mpaka leo Wakanaani wanaishi miongoni mwa watu wa Efraimu lakini wanatakiwa kufanya kazi ngumu za kulazimishwa.
and not to possess: take [obj] [the] Canaanite [the] to dwell in/on/with Gezer and to dwell [the] Canaanite in/on/with entrails: among Ephraim till [the] day: today [the] this and to be to/for taskworker to serve: labour

< Yoshua 16 >