< Yoshua 16 >

1 Mgawanyo wa Yosefu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli.
And the lot fell to the children of Ioseph from Iorden by Iericho vnto the water of Iericho Eastward, and to the wildernes that goeth vp from Iericho by the mount Beth-el:
2 Ukaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waariki huko Atarothi,
And goeth out from Beth-el to Luz, and runneth along vnto the borders of Archiataroth,
3 ukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
And goeth down Westward to the coast of Iaphleti, vnto the coast of Beth-horon the nether, and to Gezer: and the endes thereof are at the Sea.
4 Kwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yosefu, walipokea urithi wao.
So the children of Ioseph, Manasseh and Ephraim tooke their inheritance.
5 Hili ndilo lilikuwa eneo la Efraimu, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao ulianzia Ataroth-Adari upande wa mashariki hadi Beth-Horoni ya Juu,
Also the borders of the children of Ephraim according to their families, euen the borders of their inheritance on the Eastside were Atroth-addar, vnto Beth-horon the vpper.
6 na kuendelea mpaka baharini. Kutoka Mikmeta upande wa kaskazini ulipinda kuelekea mashariki hadi Taanath-Shilo, ukiupita hadi Yanoa upande wa mashariki.
And this border goeth out to the Sea vnto Michmethah on the Northside, and this border returneth Eastward vnto Taanathshiloh, and passeth it on the Eastside vnto Ianohah,
7 Kisha uliteremka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara, ukagusa Yeriko na kutokea katika Mto Yordani.
And goeth downe from Ianohah to Ataroth, and Naarath, and commeth to Iericho, and goeth out at Iorden.
8 Kutoka Tapua mpaka ulikwenda magharibi hadi Bonde la Kana na kuishia baharini. Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Waefraimu, ukoo kwa ukoo.
And this border goeth from Tappuah Westward vnto the riuer Kanah, and the endes thereof are at the Sea: this is the inheritance of the tribe of the children of Ephraim by their families.
9 Pia ulijumuisha miji yote na vijiji vyake ambavyo vilitengwa kwa ajili ya Waefraimu ndani ya urithi wa kabila la Manase.
And the separate cities for the children of Ephraim were among the inheritance of the children of Manasseh: all the cities with their villages.
10 Hawakuwatoa Wakanaani waishio Gezeri; mpaka leo Wakanaani wanaishi miongoni mwa watu wa Efraimu lakini wanatakiwa kufanya kazi ngumu za kulazimishwa.
And they cast not out the Canaanite that dwelt in Gezer, but the Canaanite dwelt among the Ephraimites vnto this day, and serued vnder tribute.

< Yoshua 16 >