< Yoshua 16 >

1 Mgawanyo wa Yosefu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli.
And the lot came forth for the children of Joseph from the Jordan of Jericho as far as the waters of Jericho eastwards, to the wilderness which goes up from Jericho to the hill-country of Bethel.
2 Ukaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waariki huko Atarothi,
And [the border] went from Bethel to Luz, and passed to the border of the Archites to Ataroth,
3 ukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
and went down westward to the border of the Japhletites, as far as the border of the lower Beth-horon, and to Gezer; and ended at the sea.
4 Kwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yosefu, walipokea urithi wao.
And the children of Joseph, Manasseh and Ephraim, took their inheritance.
5 Hili ndilo lilikuwa eneo la Efraimu, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao ulianzia Ataroth-Adari upande wa mashariki hadi Beth-Horoni ya Juu,
And the border of the children of Ephraim was according to their families; the border of their inheritance eastwards was Ataroth-Addar as far as the upper Beth-horon;
6 na kuendelea mpaka baharini. Kutoka Mikmeta upande wa kaskazini ulipinda kuelekea mashariki hadi Taanath-Shilo, ukiupita hadi Yanoa upande wa mashariki.
and the border went forth westwards to Micmethath on the north; and the border turned eastwards to Taanath-Shiloh, and passed by it eastwards to Janohah,
7 Kisha uliteremka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara, ukagusa Yeriko na kutokea katika Mto Yordani.
and went down from Janohah to Ataroth and Naarath, and touched upon Jericho, and went out to the Jordan.
8 Kutoka Tapua mpaka ulikwenda magharibi hadi Bonde la Kana na kuishia baharini. Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Waefraimu, ukoo kwa ukoo.
From Tappuah the border went westwards to the torrent Kanah, and ended at the sea. This is the inheritance of the tribe of the children of Ephraim according to their families,
9 Pia ulijumuisha miji yote na vijiji vyake ambavyo vilitengwa kwa ajili ya Waefraimu ndani ya urithi wa kabila la Manase.
with the cities that were set apart for the children of Ephraim in the midst of the inheritance of the children of Manasseh, all the cities and their hamlets.
10 Hawakuwatoa Wakanaani waishio Gezeri; mpaka leo Wakanaani wanaishi miongoni mwa watu wa Efraimu lakini wanatakiwa kufanya kazi ngumu za kulazimishwa.
But they did not dispossess the Canaanites that dwelt at Gezer; and the Canaanites dwell in the midst of Ephraim to this day, and serve under tribute.

< Yoshua 16 >