< Yoshua 16 >
1 Mgawanyo wa Yosefu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli.
And the limit of the land marked out for the children of Joseph went out from Jordan at Jericho, at the waters of Jericho on the east, in the waste land, going up from Jericho through the hill-country to Beth-el;
2 Ukaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waariki huko Atarothi,
And it goes out from Beth-el to Luz, and on as far as the limit of the Archites to Ataroth;
3 ukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
And it goes down to the west to the limit of the Japhletites, to the limit of Beth-horon the lower, as far as Gezer; ending at the sea.
4 Kwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yosefu, walipokea urithi wao.
And the children of Joseph, Manasseh and Ephraim, took their heritage.
5 Hili ndilo lilikuwa eneo la Efraimu, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao ulianzia Ataroth-Adari upande wa mashariki hadi Beth-Horoni ya Juu,
And the limit of the land of the children of Ephraim by their families was marked out in this way: the limit of their heritage to the east was Ataroth-addar, to Beth-horon the higher;
6 na kuendelea mpaka baharini. Kutoka Mikmeta upande wa kaskazini ulipinda kuelekea mashariki hadi Taanath-Shilo, ukiupita hadi Yanoa upande wa mashariki.
The line goes out to the west at Michmethath on the north; then turning to the east to Taanath-shiloh, going past it on the east of Janoah;
7 Kisha uliteremka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara, ukagusa Yeriko na kutokea katika Mto Yordani.
And from Janoah down to Ataroth, and to Naarah, and touching Jericho, it goes on to Jordan.
8 Kutoka Tapua mpaka ulikwenda magharibi hadi Bonde la Kana na kuishia baharini. Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Waefraimu, ukoo kwa ukoo.
From Tappuah the line goes on to the west to the river of Kanah; ending at the sea. This is the heritage of the children of Ephraim by their families;
9 Pia ulijumuisha miji yote na vijiji vyake ambavyo vilitengwa kwa ajili ya Waefraimu ndani ya urithi wa kabila la Manase.
Together with the towns marked out for the children of Ephraim in the heritage of Manasseh, all the towns with their unwalled places.
10 Hawakuwatoa Wakanaani waishio Gezeri; mpaka leo Wakanaani wanaishi miongoni mwa watu wa Efraimu lakini wanatakiwa kufanya kazi ngumu za kulazimishwa.
And the Canaanites who were living in Gezer were not forced out; but the Canaanites have been living among Ephraim, to this day, as servants, doing forced work.