< Yoshua 14 >

1 Basi haya ndiyo maeneo Waisraeli waliyopokea kama urithi katika nchi ya Kanaani, ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliwagawia.
and these which to inherit son: descendant/people Israel in/on/with land: country/planet Canaan which to inherit [obj] them Eleazar [the] priest and Joshua son: child Nun and head: leader father [the] tribe to/for son: descendant/people Israel
2 Urithi wao uligawanywa kwa kura kwa yale makabila tisa na nusu, kama Bwana alivyoamuru Mose.
in/on/with allotted inheritance their like/as as which to command LORD in/on/with hand Moses to/for nine [the] tribe and half [the] tribe
3 Mose alikuwa amewapa yale makabila mawili na nusu urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, lakini Walawi hawakupewa urithi miongoni mwa hao wengine,
for to give: give Moses inheritance two [the] tribe and half [the] tribe from side: beyond to/for Jordan and to/for Levi not to give: give inheritance in/on/with midst their
4 kwa kuwa wana wa Yosefu walikuwa makabila mawili; Manase na Efraimu. Walawi hawakupata mgawo wa ardhi, bali walipewa miji tu kwa ajili ya kuishi, pamoja na maeneo ya malisho kwa ajili ya makundi yao ya kondoo, mbuzi na ngʼombe wao.
for to be son: descendant/people Joseph two tribe Manasseh and Ephraim and not to give: give portion to/for Levi in/on/with land: country/planet that if: except if: except city to/for to dwell and pasture their to/for livestock their and to/for acquisition their
5 Kwa hiyo Waisraeli wakagawana ile nchi, kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
like/as as which to command LORD [obj] Moses so to make: do son: descendant/people Israel and to divide [obj] [the] land: country/planet
6 Kisha watu wa Yuda wakamwendea Yoshua huko Gilgali, naye Kalebu mwana wa Yefune yule Mkenizi, akamwambia, “Unajua jambo ambalo Bwana alimwambia Mose mtu wa Mungu huko Kadesh-Barnea kukuhusu wewe na mimi.
and to approach: approach son: descendant/people Judah to(wards) Joshua in/on/with Gilgal and to say to(wards) him Caleb son: child Jephunneh [the] Kenizzite you(m. s.) to know [obj] [the] word: thing which to speak: speak LORD to(wards) Moses man [the] God upon because my and upon because your in/on/with Kadesh-barnea Kadesh-barnea
7 Nilikuwa na umri wa miaka arobaini, wakati Mose mtumishi wa Bwana, aliponituma kutoka Kadesh-Barnea kuipeleleza hiyo nchi. Nami nikamletea taarifa kama kulingana na nilivyosadiki moyoni.
son: aged forty year I in/on/with to send: depart Moses servant/slave LORD [obj] me from Kadesh-barnea Kadesh-barnea to/for to spy [obj] [the] land: country/planet and to return: return [obj] him word like/as as which with heart my
8 Lakini ndugu zangu tuliopanda nao waliifanya mioyo ya watu iyeyuke kwa hofu. Bali mimi, nilimfuata Bwana Mungu wangu kwa moyo wote.
and brother: compatriot my which to ascend: rise with me to liquefy [obj] heart [the] people and I to fill after LORD God my
9 Hivyo katika siku ile, Mose akaniapia, ‘Nchi ambayo umeikanyaga kwa miguu yako itakuwa urithi wako na wa watoto wako milele, kwa sababu umemfuata Bwana Mungu wangu kwa moyo wote.’
and to swear Moses in/on/with day [the] he/she/it to/for to say if: surely yes not [the] land: country/planet which to tread foot your in/on/with her to/for you to be to/for inheritance and to/for son: child your till forever: enduring for to fill after LORD God my
10 “Sasa basi, kama vile Bwana alivyoahidi, ameniweka hai kwa miaka arobaini na mitano tangu wakati alipomwambia Mose jambo hili, wakati Waisraeli wakiwa wanazunguka jangwani. Hivyo mimi hapa leo, nina umri wa miaka themanini na mitano!
and now behold to live LORD [obj] me like/as as which to speak: speak this forty and five year from the past to speak: speak LORD [obj] [the] word [the] this to(wards) Moses which to go: walk Israel in/on/with wilderness and now behold I [the] day: today son: aged five and eighty year
11 Bado ninazo nguvu kama siku ile Mose aliponituma. Bado ninazo nguvu za kwenda vitani sasa kama vile nilivyokuwa wakati ule.
still I [the] day strong like/as as which in/on/with day to send: depart [obj] me Moses like/as strength my then and like/as strength my now to/for battle and to/for to come out: come and to/for to come (in): come
12 Basi nipe nchi hii ya vilima, ambayo Bwana aliniahidi siku ile. Wewe mwenyewe ulisikia wakati ule kwamba Waanaki walikuwako huko na miji yao ilikuwa mikubwa na yenye maboma, lakini, kwa msaada wa Bwana, nitawafukuza watoke huko kama vile alivyonena.”
and now to give: give [emph?] to/for me [obj] [the] mountain: hill country [the] this which to speak: speak LORD in/on/with day [the] he/she/it for you(m. s.) to hear: hear in/on/with day [the] he/she/it for Anakite there and city great: large to gather/restrain/fortify perhaps LORD with me and to possess: take them like/as as which to speak: speak LORD
13 Ndipo Yoshua akambariki Kalebu mwana wa Yefune, na akampa Hebroni kama urithi wake.
and to bless him Joshua and to give: give [obj] Hebron to/for Caleb son: child Jephunneh to/for inheritance
14 Hivyo Hebroni imekuwa mali ya Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi tangu wakati ule, kwa sababu alimwandama Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wote.
upon so to be Hebron to/for Caleb son: child Jephunneh [the] Kenizzite to/for inheritance till [the] day: today [the] this because which to fill after LORD God Israel
15 (Hebroni uliitwa Kiriath-Arba hapo mwanzo, kutokana na huyo Arba ambaye alikuwa mtu mkuu kupita wote miongoni mwa Waanaki.) Kisha nchi ikawa na amani bila vita.
and name Hebron to/for face: before Kiriath-arba Kiriath-arba [the] man [the] great: large in/on/with Anakite he/she/it and [the] land: country/planet to quiet from battle

< Yoshua 14 >