< Yoshua 14 >

1 Basi haya ndiyo maeneo Waisraeli waliyopokea kama urithi katika nchi ya Kanaani, ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliwagawia.
And these are the inheritances which the children of Israel took in the land of Canaan, which Eleazar the priest, and Joshua the son of Nun, and the heads of the fathers' houses of the tribes of the children of Israel, distributed unto them,
2 Urithi wao uligawanywa kwa kura kwa yale makabila tisa na nusu, kama Bwana alivyoamuru Mose.
by the lot of their inheritance, as the LORD commanded by the hand of Moses, for the nine tribes, and for the half-tribe. —
3 Mose alikuwa amewapa yale makabila mawili na nusu urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, lakini Walawi hawakupewa urithi miongoni mwa hao wengine,
For Moses had given the inheritance of the two tribes and the half-tribe beyond the Jordan; but unto the Levites he gave no inheritance among them.
4 kwa kuwa wana wa Yosefu walikuwa makabila mawili; Manase na Efraimu. Walawi hawakupata mgawo wa ardhi, bali walipewa miji tu kwa ajili ya kuishi, pamoja na maeneo ya malisho kwa ajili ya makundi yao ya kondoo, mbuzi na ngʼombe wao.
For the children of Joseph were two tribes, Manasseh and Ephraim; and they gave no portion unto the Levites in the land, save cities to dwell in, with the open land about them for their cattle and for their substance. —
5 Kwa hiyo Waisraeli wakagawana ile nchi, kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
As the LORD commanded Moses, so the children of Israel did, and they divided the land.
6 Kisha watu wa Yuda wakamwendea Yoshua huko Gilgali, naye Kalebu mwana wa Yefune yule Mkenizi, akamwambia, “Unajua jambo ambalo Bwana alimwambia Mose mtu wa Mungu huko Kadesh-Barnea kukuhusu wewe na mimi.
Then the children of Judah drew nigh unto Joshua in Gilgal; and Caleb the son of Jephunneh the Kenizzite said unto him: 'Thou knowest the thing that the LORD spoke unto Moses the man of God concerning me and concerning thee in Kadesh-barnea.
7 Nilikuwa na umri wa miaka arobaini, wakati Mose mtumishi wa Bwana, aliponituma kutoka Kadesh-Barnea kuipeleleza hiyo nchi. Nami nikamletea taarifa kama kulingana na nilivyosadiki moyoni.
Forty years old was I when Moses the servant of the LORD sent me from Kadesh-barnea to spy out the land; and I brought him back word as it was in my heart.
8 Lakini ndugu zangu tuliopanda nao waliifanya mioyo ya watu iyeyuke kwa hofu. Bali mimi, nilimfuata Bwana Mungu wangu kwa moyo wote.
Nevertheless my brethren that went up with me made the heart of the people melt; but I wholly followed the LORD my God.
9 Hivyo katika siku ile, Mose akaniapia, ‘Nchi ambayo umeikanyaga kwa miguu yako itakuwa urithi wako na wa watoto wako milele, kwa sababu umemfuata Bwana Mungu wangu kwa moyo wote.’
And Moses swore on that day, saying: Surely the land whereon thy foot hath trodden shall be an inheritance to thee and to thy children for ever, because thou hast wholly followed the LORD my God.
10 “Sasa basi, kama vile Bwana alivyoahidi, ameniweka hai kwa miaka arobaini na mitano tangu wakati alipomwambia Mose jambo hili, wakati Waisraeli wakiwa wanazunguka jangwani. Hivyo mimi hapa leo, nina umri wa miaka themanini na mitano!
And now, behold, the LORD hath kept me alive, as He spoke, these forty and five years, from the time that the LORD spoke this word unto Moses, while Israel walked in the wilderness; and now, lo, I am this day fourscore and five years old.
11 Bado ninazo nguvu kama siku ile Mose aliponituma. Bado ninazo nguvu za kwenda vitani sasa kama vile nilivyokuwa wakati ule.
As yet I am as strong this day as I was in the day that Moses sent me; as my strength was then, even so is my strength now, for war, and to go out and to come in.
12 Basi nipe nchi hii ya vilima, ambayo Bwana aliniahidi siku ile. Wewe mwenyewe ulisikia wakati ule kwamba Waanaki walikuwako huko na miji yao ilikuwa mikubwa na yenye maboma, lakini, kwa msaada wa Bwana, nitawafukuza watoke huko kama vile alivyonena.”
Now therefore give me this mountain, whereof the LORD spoke in that day; for thou heardest in that day how the Anakim were there, and cities great and fortified; it may be that the LORD will be with me, and I shall drive them out, as the LORD spoke.'
13 Ndipo Yoshua akambariki Kalebu mwana wa Yefune, na akampa Hebroni kama urithi wake.
And Joshua blessed him; and he gave Hebron unto Caleb the son of Jephunneh for an inheritance.
14 Hivyo Hebroni imekuwa mali ya Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi tangu wakati ule, kwa sababu alimwandama Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wote.
Therefore Hebron became the inheritance of Caleb the son of Jephunneh the Kenizzite, unto this day; because that he wholly followed the LORD, the God of Israel.
15 (Hebroni uliitwa Kiriath-Arba hapo mwanzo, kutokana na huyo Arba ambaye alikuwa mtu mkuu kupita wote miongoni mwa Waanaki.) Kisha nchi ikawa na amani bila vita.
Now the name of Hebron beforetime was Kiriath-arba, which Arba was the greatest man among the Anakim. And the land had rest from war.

< Yoshua 14 >