< Yoshua 13 >

1 Yoshua alipokuwa mzee na umri wake ukiwa umesogea sana, Bwana akamwambia, “Wewe ni mzee sana, na bado kumesalia sehemu kubwa sana za nchi ambazo ni za kutwaliwa.
Et Josué était vieux, avancé en âge, et l’Éternel lui dit: Tu es devenu vieux, tu avances en âge, et il reste un très grand pays à posséder.
2 “Nchi iliyosalia ni hii: maeneo yote ya Wafilisti na Wageshuri:
C’est ici le pays qui reste: tous les districts des Philistins et tous les Gueshuriens,
3 kutoka Mto Shihori ulioko mashariki mwa Misri, kuelekea kaskazini kwenye eneo la Ekroni, ambayo yote ilihesabika kama ya Wakanaani (maeneo yale matano ya watawala wa Kifilisti, ambayo ni Gaza, Ashdodi, Ashkeloni, Gathi na Ekroni: ndiyo nchi ya Waavi);
depuis le Shikhor qui est devant l’Égypte, jusqu’à la frontière d’Ékron, vers le nord; il est réputé appartenir aux Cananéens: cinq princes des Philistins, celui de Gaza, et celui d’Asdod, celui d’Askalon, celui de Gath, et celui d’Ékron, et les Avviens;
4 kuanzia kusini, nchi yote ya Wakanaani, kuanzia Ara ambayo ni ya Wasidoni, ikienea hadi Afeki, na eneo la Waamori,
au sud, tout le pays des Cananéens, et Méara, qui est aux Sidoniens, jusqu’à Aphek, jusqu’à la frontière de l’Amoréen;
5 eneo la Wagebali; Lebanoni yote kuelekea mashariki, kuanzia Baal-Gadi chini ya Mlima Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
et le pays des Guibliens, et tout le Liban, vers le soleil levant, depuis Baal-Gad, au pied de la montagne de l’Hermon, jusqu’à l’entrée de Hamath;
6 “Na kuhusu wakaaji wote katika maeneo ya milima, kuanzia Lebanoni hadi Misrefoth-Maimu, pamoja na eneo lote la Wasidoni, mimi mwenyewe nitawafukuza watoke mbele ya Waisraeli. Hakikisha umegawa nchi hii kwa Israeli kuwa urithi, kama nilivyokuagiza,
tous les habitants de la montagne, depuis le Liban jusqu’à Misrephoth-Maïm, tous les Sidoniens. Moi, je les déposséderai devant les fils d’Israël. Seulement, répartis par le sort [ce pays] en héritage à Israël, comme je te l’ai commandé.
7 sasa basi, ligawanye eneo hili kwa yale makabila tisa na ile nusu ya kabila la Manase kuwa urithi.”
Et maintenant, distribue ce pays en héritage aux neuf tribus, et à la demi-tribu de Manassé.
8 Ile nusu nyingine ya Manase, Wareubeni na Wagadi, walishapokea urithi Mose aliokuwa amewapa mashariki mwa Yordani, sawasawa na mtumishi wa Bwana alivyowagawia.
Avec l’autre moitié de Manassé, les Rubénites et les Gadites ont reçu leur héritage, que Moïse leur a donné au-delà du Jourdain, vers le levant, selon ce que Moïse, serviteur de l’Éternel, leur a donné,
9 Eneo lao lilienea toka Aroeri, iliyoko ukingoni mwa Bonde la Arnoni kuanzia mji ulio katikati ya bonde, likijumlisha nchi ya uwanda wa juu wote wa Medeba mpaka Diboni,
depuis Aroër, qui est sur le bord du torrent de l’Arnon, et la ville qui est au milieu du torrent, et tout le plateau de Médeba, jusqu’à Dibon;
10 nayo miji yote ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi mpakani mwa Waamoni.
et toutes les villes de Sihon, roi des Amoréens, qui régnait à Hesbon, jusqu’à la frontière des fils d’Ammon;
11 Vilevile ilijumlisha Gileadi, eneo la Wageshuri na Wamaaka, mlima wote wa Hermoni na Bashani yote ikienea hadi Saleka:
et Galaad, et les confins des Gueshuriens et des Maacathiens, et toute la montagne de l’Hermon; et tout Basan, jusqu’à Salca,
12 yaani ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyekuwa ametawala katika Ashtarothi na Edrei, na ndiye pekee alisalia kwa Warefai. Mose alikuwa amewashinda na kuteka nchi yao.
tout le royaume d’Og, en Basan, qui régnait à Ashtaroth et à Édréhi; (il était demeuré du reste des Rephaïm); et Moïse les frappa et les déposséda.
13 Lakini Waisraeli hawakuwafukuza watu wa Geshuri na wa Maaka, kwa hiyo wanaendelea kuishi miongoni mwa Waisraeli mpaka leo hii.
– Mais les fils d’Israël ne dépossédèrent pas les Gueshuriens et les Maacathiens; et Gueshur et Maaca habitent au milieu d’Israël jusqu’à ce jour.
14 Lakini kwa kabila la Lawi, Mose hakupeana urithi, kwa kuwa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizotolewa kwa Bwana, Mungu wa Israeli, ndizo zilizokuwa urithi wao, kama alivyowaahidi.
À la tribu de Lévi seule il ne donna point d’héritage; les sacrifices de l’Éternel, le Dieu d’Israël, faits par feu, c’est là son héritage, comme il le lui avait dit.
15 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Reubeni ukoo kwa ukoo:
Et Moïse donna [une part] à la tribu des fils de Ruben, selon leurs familles.
16 Eneo la Aroeri lililo ukingoni mwa Bonde la Arnoni, na kuanzia mji ulio katikati ya bonde, pia uwanda wote wa juu kupita Medeba
Et leur territoire était depuis Aroër, qui est sur le bord du torrent de l’Arnon, et la ville qui est au milieu du torrent, et tout le plateau près de Médeba;
17 hadi Heshboni na miji yake yote kwenye uwanda wa juu, ikijumlishwa miji ya Diboni, Bamoth-Baali, Beth-Baal-Meoni,
Hesbon et toutes ses villes, qui étaient sur le plateau: Dibon, et Bamoth-Baal, et Beth-Baal-Méon,
18 Yahasa, Kedemothi, Mefaathi,
et Jahtsa, et Kedémoth, et Méphaath,
19 Kiriathaimu, Sibma, Sereth-Shahari juu ya kilima kilicho katika bonde,
et Kiriathaïm, et Sibma, et Tséreth-Shakhar dans la montagne de la vallée,
20 Beth-Peori, materemko ya Pisga na Beth-Yeshimothi:
et Beth-Péor, et les pentes du Pisga, et Beth-Jeshimoth,
21 miji yote ya uwanda wa juu na eneo lote la utawala wa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala katika Heshboni. Mose alikuwa amemshinda Sihoni, pia watawala wakuu wa Wamidiani, ambao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba, waliokuwa wameungana na Sihoni, ambao waliishi katika nchi ile.
toutes les villes du plateau et tout le royaume de Sihon, roi des Amoréens, qui régnait à Hesbon, que Moïse frappa, lui et les princes de Madian: Évi, et Rékem, et Tsur, et Hur, et Réba, seigneurs de Sihon, habitants du pays.
22 Pamoja na wale waliouawa katika vita, Waisraeli walikuwa wamemuua kwa upanga Balaamu mwana wa Beori aliyekuwa mchawi.
Et les fils d’Israël tuèrent par l’épée Balaam, fils de Béor, le devin, avec les autres qui furent tués.
23 Mpaka wa Wareubeni ulikuwa ni ukingo wa Mto Yordani. Miji hii na vijiji vyake ndiyo iliyokuwa urithi wa Wareubeni ukoo kwa ukoo.
Et la frontière des fils de Ruben fut le Jourdain et [sa] rive. Ce fut là l’héritage des fils de Ruben, selon leurs familles: les villes et leurs hameaux.
24 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
Et Moïse donna [une part] à la tribu de Gad, aux fils de Gad, selon leurs familles.
25 Nchi ya Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Amoni iliyoenea hadi Aroeri, karibu na Raba;
Et leur territoire était Jahzer, et toutes les villes de Galaad, et la moitié du pays des fils d’Ammon, jusqu’à Aroër, qui est vis-à-vis de Rabba;
26 na kuanzia Heshboni mpaka Ramath-Mispa na Betonimu, na kutoka Mahanaimu hadi eneo la Debiri;
et depuis Hesbon jusqu’à Ramath-Mitspé et Betonim, et depuis Mahanaïm jusqu’à la frontière de Debir;
27 na katika bonde, Beth-Haramu, Beth-Nimra, Sukothi na Safoni na sehemu iliyobaki ya eneo la utawala wa Sihoni mfalme wa Heshboni (upande wa mashariki mwa Mto Yordani, eneo inayoishia kwenye Bahari ya Kinerethi).
et, dans la vallée, Beth-Haram, et Beth-Nimra, et Succoth, et Tsaphon, le reste du royaume de Sihon, roi de Hesbon, le Jourdain et [sa] rive, jusqu’au bout de la mer de Kinnéreth, au-delà du Jourdain, vers le levant.
28 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Gadi ukoo kwa ukoo.
Ce fut là l’héritage des fils de Gad, selon leurs familles: les villes et leurs hameaux.
29 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa hiyo nusu ya kabila la Manase, yaani kwa nusu ya jamaa ya uzao wa Manase, ukoo kwa ukoo:
Et Moïse donna [une part] à la demi-tribu de Manassé; et pour la demi-tribu des fils de Manassé, selon leurs familles,
30 Eneo lililoenea kuanzia Mahanaimu, na kujumlisha Bashani yote, ufalme wote wa Ogu mfalme wa Bashani, makazi yote ya Yairi huko Bashani, miji sitini,
leur territoire était depuis Mahanaïm: tout Basan, tout le royaume d’Og, roi de Basan, et tous les bourgs de Jaïr, qui sont en Basan, 60 villes;
31 nusu ya Gileadi, na Ashtarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Hii ilikuwa kwa ajili ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, kwa ajili ya nusu ya wana wa Makiri, ukoo kwa ukoo.
et la moitié de Galaad, et Ashtaroth, et Édréhi, villes du royaume d’Og, en Basan, furent aux fils de Makir, fils de Manassé, à la moitié des fils de Makir, selon leurs familles.
32 Huu ndio urithi alioupeana Mose wakati alipokuwa katika tambarare za Moabu, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
C’est là ce que Moïse distribua en héritage dans les plaines de Moab, au-delà du Jourdain de Jéricho, vers le levant.
33 Lakini kwa kabila la Walawi, Mose hakuwapa urithi; Bwana Mungu, Mungu wa Israeli ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
Mais Moïse ne donna point d’héritage à la tribu de Lévi; l’Éternel, le Dieu d’Israël, était leur héritage, comme il le leur avait dit.

< Yoshua 13 >