< Yoshua 13 >

1 Yoshua alipokuwa mzee na umri wake ukiwa umesogea sana, Bwana akamwambia, “Wewe ni mzee sana, na bado kumesalia sehemu kubwa sana za nchi ambazo ni za kutwaliwa.
Josue was eld and of greet age; and the Lord seide to him, Thou hast woxe eld, and art of long tyme; and largeste lond is left, which is not yit departid bi lot;
2 “Nchi iliyosalia ni hii: maeneo yote ya Wafilisti na Wageshuri:
that is, al Galile, Filistiym, and al Gessuri,
3 kutoka Mto Shihori ulioko mashariki mwa Misri, kuelekea kaskazini kwenye eneo la Ekroni, ambayo yote ilihesabika kama ya Wakanaani (maeneo yale matano ya watawala wa Kifilisti, ambayo ni Gaza, Ashdodi, Ashkeloni, Gathi na Ekroni: ndiyo nchi ya Waavi);
fro the troblid flood that moistith Egipt, `til to the termes of Acaron ayenus the north; the lond of Chanaan, which is departid `in to fyue litle kyngis of Filistym, of Gaza, and of Azotus, of Ascolon, of Geth, and of Accaron.
4 kuanzia kusini, nchi yote ya Wakanaani, kuanzia Ara ambayo ni ya Wasidoni, ikienea hadi Afeki, na eneo la Waamori,
Forsothe at the south ben Eueis, al the lond of Canaan, and Maara of Sidonyes, `til to Affetha, and to the termes of Amorrei, and the coostis of hym;
5 eneo la Wagebali; Lebanoni yote kuelekea mashariki, kuanzia Baal-Gadi chini ya Mlima Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
and the cuntrei of Liban ayens the eest, fro Baalgath, vndur the hil of Hermon, til thou entrist into Emath,
6 “Na kuhusu wakaaji wote katika maeneo ya milima, kuanzia Lebanoni hadi Misrefoth-Maimu, pamoja na eneo lote la Wasidoni, mimi mwenyewe nitawafukuza watoke mbele ya Waisraeli. Hakikisha umegawa nchi hii kwa Israeli kuwa urithi, kama nilivyokuagiza,
of alle men that dwelliden in the hil, fro the Liban `til to the watris of Masserephoth, and alle men of Sidon; Y am, that schal do awei hem fro the face of the sones of Israel; therfor come it in to the part of eritage of Israel, as Y comaundide to thee.
7 sasa basi, ligawanye eneo hili kwa yale makabila tisa na ile nusu ya kabila la Manase kuwa urithi.”
And thou now departe the lond in to possessioun to the nyne lynagis, and to the half lynage of Manasses,
8 Ile nusu nyingine ya Manase, Wareubeni na Wagadi, walishapokea urithi Mose aliokuwa amewapa mashariki mwa Yordani, sawasawa na mtumishi wa Bwana alivyowagawia.
with which lynage Ruben and Gad weldiden the lond, which lond Moises, the `seruaunt of the Lord, yaf to hem biyende the flowyngis of Jordan, at the eest coost;
9 Eneo lao lilienea toka Aroeri, iliyoko ukingoni mwa Bonde la Arnoni kuanzia mji ulio katikati ya bonde, likijumlisha nchi ya uwanda wa juu wote wa Medeba mpaka Diboni,
fro Aroer, which is set in the brynke of the stronde of Arnon, in the middis of the valei, and alle the feeldi places of Medaba,
10 nayo miji yote ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi mpakani mwa Waamoni.
`til to Dibon, and alle the citees of Seon, kyng of Amorreis, that regnyde in Esebon, `til to the termes of the sones of Amon,
11 Vilevile ilijumlisha Gileadi, eneo la Wageshuri na Wamaaka, mlima wote wa Hermoni na Bashani yote ikienea hadi Saleka:
and of Galaad, and to the termes of Gessuri, and of Machati, and al the hil of Hermon, and al Basan, `til to Salecha;
12 yaani ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyekuwa ametawala katika Ashtarothi na Edrei, na ndiye pekee alisalia kwa Warefai. Mose alikuwa amewashinda na kuteka nchi yao.
al the rewme of Og in Basan, that regnede in Astoroth, and in Edraym; `he was of the relikis of Rafaym, `that is, of giauntis; and Moises smoot hem and dide awey hem.
13 Lakini Waisraeli hawakuwafukuza watu wa Geshuri na wa Maaka, kwa hiyo wanaendelea kuishi miongoni mwa Waisraeli mpaka leo hii.
And the sones of Israel nolden destrye Gessurri and Machati; and thei dwelliden in the myddis of Israel, `til in to present dai.
14 Lakini kwa kabila la Lawi, Mose hakupeana urithi, kwa kuwa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizotolewa kwa Bwana, Mungu wa Israeli, ndizo zilizokuwa urithi wao, kama alivyowaahidi.
Sotheli he yaf not possessioun to the lynage of Leuy, but sacrifices, and slayn sacrifices of the Lord God of Israel; that is `his eritage, as God spak to hym.
15 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Reubeni ukoo kwa ukoo:
Therfor Moises yaf possessioun to the lynage of the sones of Ruben, bi her kynredis;
16 Eneo la Aroeri lililo ukingoni mwa Bonde la Arnoni, na kuanzia mji ulio katikati ya bonde, pia uwanda wote wa juu kupita Medeba
and `the term of hem was fro Aroer, which is set in the brenke of the stronde of Arnon, and in the myddil valei of the same stronde, al the pleyn that ledith to Medaba,
17 hadi Heshboni na miji yake yote kwenye uwanda wa juu, ikijumlishwa miji ya Diboni, Bamoth-Baali, Beth-Baal-Meoni,
and Esebon, and alle the townes of tho, that ben in the feeldi places; and Dibon, and Baal Bamoth, and the citee of Baal Meon,
18 Yahasa, Kedemothi, Mefaathi,
and Gesa, and Sedymoth, and Mephe,
19 Kiriathaimu, Sibma, Sereth-Shahari juu ya kilima kilicho katika bonde,
and Cariathaym, and Sabana, and Sarathaphar, in the hil of the valey of Betheroeth,
20 Beth-Peori, materemko ya Pisga na Beth-Yeshimothi:
and of Asedoch, Phasca, and Bethaissymoth;
21 miji yote ya uwanda wa juu na eneo lote la utawala wa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala katika Heshboni. Mose alikuwa amemshinda Sihoni, pia watawala wakuu wa Wamidiani, ambao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba, waliokuwa wameungana na Sihoni, ambao waliishi katika nchi ile.
alle the feeldi citees, and alle the rewmes of Seon, kyng of Amorrey, that regnede in Esebon, whom Moyses smoot, with hise princes, Madian, Euey and Recten, and Sur, and Hur, and Rebee, duykis of Seon, enhabiters of the lond.
22 Pamoja na wale waliouawa katika vita, Waisraeli walikuwa wamemuua kwa upanga Balaamu mwana wa Beori aliyekuwa mchawi.
And the sones of Israel killiden bi swerd Balaam, the fals diuynour, the sone of Beor, with othere men slayn.
23 Mpaka wa Wareubeni ulikuwa ni ukingo wa Mto Yordani. Miji hii na vijiji vyake ndiyo iliyokuwa urithi wa Wareubeni ukoo kwa ukoo.
And the terme of the sones of Ruben was maad the flood of Jordan; this is the possessioun of Rubenytis bi her kynredis of citees and of townes.
24 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
And Moises yaf to the lynage of Gad, and to the sones therof, bi her kynredis, possessioun, of which this is departyng;
25 Nchi ya Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Amoni iliyoenea hadi Aroeri, karibu na Raba;
he yaf the termes of Jazer, and alle the citees of Galaad, and the half part of the lond of the sones of Amon, `til to Aroer which is ayens Tabba;
26 na kuanzia Heshboni mpaka Ramath-Mispa na Betonimu, na kutoka Mahanaimu hadi eneo la Debiri;
and fro Esebon `til to Ramoth of Masphe, and Bethamyn, and Manayn, `til to the termes of Dabir;
27 na katika bonde, Beth-Haramu, Beth-Nimra, Sukothi na Safoni na sehemu iliyobaki ya eneo la utawala wa Sihoni mfalme wa Heshboni (upande wa mashariki mwa Mto Yordani, eneo inayoishia kwenye Bahari ya Kinerethi).
and in the valei he yaf Betharan, and Bethneuar, and Socoth, and Saphan, the tother part of the rewme of Seon, kyng of Esebon; and the ende of this is Jordan, `til to the laste part of the see of Cenereth ouer Jordan, at the eest coost.
28 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Gadi ukoo kwa ukoo.
This is the possessioun of the sones of Gad, bi her meynees, the citees and townes of tho.
29 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa hiyo nusu ya kabila la Manase, yaani kwa nusu ya jamaa ya uzao wa Manase, ukoo kwa ukoo:
He yaf also possessioun to the half lynage of Manasses, and to hise sones, bi her kynredis,
30 Eneo lililoenea kuanzia Mahanaimu, na kujumlisha Bashani yote, ufalme wote wa Ogu mfalme wa Bashani, makazi yote ya Yairi huko Bashani, miji sitini,
of which possessioun this is the bigynnyng; he yaf Ammaym, and al Basan, and alle the rewmes of Og, kyng of Basan, and alle the townes of Jair, that ben in Basan, sixti citees;
31 nusu ya Gileadi, na Ashtarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Hii ilikuwa kwa ajili ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, kwa ajili ya nusu ya wana wa Makiri, ukoo kwa ukoo.
and half the part of Galaad, and Astoroth, and Edray, the citees of the rewme of Og, kyng of Basan; to the sones of Machir, sones of Manasses, and to half the part of the sones of Machir, bi her kynredis.
32 Huu ndio urithi alioupeana Mose wakati alipokuwa katika tambarare za Moabu, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
Moises departide this possessioun in the feeldi placis of Moab ouer Jordan, ayens Jericho, at the eest coost.
33 Lakini kwa kabila la Walawi, Mose hakuwapa urithi; Bwana Mungu, Mungu wa Israeli ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
Forsothe he yaf not possessioun to the lynage of Leuy; for the Lord God himself of Israel is the possessioun of Leuy, as the Lord spak to hym.

< Yoshua 13 >