< Yoshua 13 >

1 Yoshua alipokuwa mzee na umri wake ukiwa umesogea sana, Bwana akamwambia, “Wewe ni mzee sana, na bado kumesalia sehemu kubwa sana za nchi ambazo ni za kutwaliwa.
and Joshua be old to come (in): advanced in/on/with day: year and to say LORD to(wards) him you(m. s.) be old to come (in): advanced in/on/with day: year and [the] land: country/planet to remain to multiply much to/for to possess: take her
2 “Nchi iliyosalia ni hii: maeneo yote ya Wafilisti na Wageshuri:
this [the] land: country/planet [the] to remain all border [the] Philistine and all [the] Geshurite
3 kutoka Mto Shihori ulioko mashariki mwa Misri, kuelekea kaskazini kwenye eneo la Ekroni, ambayo yote ilihesabika kama ya Wakanaani (maeneo yale matano ya watawala wa Kifilisti, ambayo ni Gaza, Ashdodi, Ashkeloni, Gathi na Ekroni: ndiyo nchi ya Waavi);
from [the] Shihor which upon face: surface Egypt and till border: boundary Ekron north [to] to/for Canaanite to devise: count five lord Philistine [the] Gaza and [the] Ashdod [the] Ashkelonite [the] Gittite and [the] Ekron and [the] Avvim
4 kuanzia kusini, nchi yote ya Wakanaani, kuanzia Ara ambayo ni ya Wasidoni, ikienea hadi Afeki, na eneo la Waamori,
from south all land: country/planet [the] Canaanite and Mearah which to/for Sidonian till Aphek [to] till border: boundary [the] Amorite
5 eneo la Wagebali; Lebanoni yote kuelekea mashariki, kuanzia Baal-Gadi chini ya Mlima Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
and [the] land: country/planet [the] Gebalite and all [the] Lebanon east [the] sun from Baal-gad Baal-gad underneath: under mountain: mount (Mount) Hermon till Lebo-(Hamath) Hamath
6 “Na kuhusu wakaaji wote katika maeneo ya milima, kuanzia Lebanoni hadi Misrefoth-Maimu, pamoja na eneo lote la Wasidoni, mimi mwenyewe nitawafukuza watoke mbele ya Waisraeli. Hakikisha umegawa nchi hii kwa Israeli kuwa urithi, kama nilivyokuagiza,
all to dwell [the] mountain: hill country from [the] Lebanon till Misrephoth-maim Misrephoth-maim all Sidonian I to possess: take them from face: before son: descendant/people Israel except to fall: allot her to/for Israel in/on/with inheritance like/as as which to command you
7 sasa basi, ligawanye eneo hili kwa yale makabila tisa na ile nusu ya kabila la Manase kuwa urithi.”
and now to divide [obj] [the] land: country/planet [the] this in/on/with inheritance to/for nine [the] tribe and half [the] tribe [the] Manasseh
8 Ile nusu nyingine ya Manase, Wareubeni na Wagadi, walishapokea urithi Mose aliokuwa amewapa mashariki mwa Yordani, sawasawa na mtumishi wa Bwana alivyowagawia.
with him [the] Reubenite and [the] Gad to take: recieve inheritance their which to give: give to/for them Moses in/on/with side: beyond [the] Jordan east [to] like/as as which to give: give to/for them Moses servant/slave LORD
9 Eneo lao lilienea toka Aroeri, iliyoko ukingoni mwa Bonde la Arnoni kuanzia mji ulio katikati ya bonde, likijumlisha nchi ya uwanda wa juu wote wa Medeba mpaka Diboni,
from Aroer which upon lip: edge torrent: valley Arnon and [the] city which in/on/with midst [the] torrent: valley and all [the] plain Medeba till Dibon
10 nayo miji yote ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi mpakani mwa Waamoni.
and all city Sihon king [the] Amorite which to reign in/on/with Heshbon till border: boundary son: descendant/people Ammon
11 Vilevile ilijumlisha Gileadi, eneo la Wageshuri na Wamaaka, mlima wote wa Hermoni na Bashani yote ikienea hadi Saleka:
and [the] Gilead and border: area [the] Geshurite and [the] Maacathite and all mountain: mount (Mount) Hermon and all [the] Bashan till Salecah
12 yaani ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyekuwa ametawala katika Ashtarothi na Edrei, na ndiye pekee alisalia kwa Warefai. Mose alikuwa amewashinda na kuteka nchi yao.
all kingdom Og in/on/with Bashan which to reign in/on/with Ashtaroth and in/on/with Edrei he/she/it to remain from remainder [the] Rephaim and to smite them Moses and to possess: take them
13 Lakini Waisraeli hawakuwafukuza watu wa Geshuri na wa Maaka, kwa hiyo wanaendelea kuishi miongoni mwa Waisraeli mpaka leo hii.
and not to possess: take son: descendant/people Israel [obj] [the] Geshurite and [obj] [the] Maacathite and to dwell Geshur and Maacah in/on/with entrails: among Israel till [the] day: today [the] this
14 Lakini kwa kabila la Lawi, Mose hakupeana urithi, kwa kuwa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizotolewa kwa Bwana, Mungu wa Israeli, ndizo zilizokuwa urithi wao, kama alivyowaahidi.
except to/for tribe [the] Levi not to give: give inheritance food offering LORD God Israel he/she/it inheritance his like/as as which to speak: speak to/for him
15 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Reubeni ukoo kwa ukoo:
and to give: give Moses to/for tribe son: descendant/people Reuben to/for family their
16 Eneo la Aroeri lililo ukingoni mwa Bonde la Arnoni, na kuanzia mji ulio katikati ya bonde, pia uwanda wote wa juu kupita Medeba
and to be to/for them [the] border: area from Aroer which upon lip: edge torrent: valley Arnon and [the] city which in/on/with midst [the] torrent: valley and all [the] plain upon Medeba
17 hadi Heshboni na miji yake yote kwenye uwanda wa juu, ikijumlishwa miji ya Diboni, Bamoth-Baali, Beth-Baal-Meoni,
Heshbon and all city her which in/on/with plain Dibon and Bamoth (Bamoth)-baal and Beth-(baal-meon) Baal-meon Baal-meon
18 Yahasa, Kedemothi, Mefaathi,
and Jahaz [to] and Kedemoth and Mephaath
19 Kiriathaimu, Sibma, Sereth-Shahari juu ya kilima kilicho katika bonde,
and Kiriathaim and Sibmah and Zereth-shahar [the] Zereth-shahar in/on/with mountain: mount [the] valley
20 Beth-Peori, materemko ya Pisga na Beth-Yeshimothi:
and Beth-peor Beth-peor and Slopes (of Pisgah) [the] Pisgah and Beth-jeshimoth [the] Beth-jeshimoth
21 miji yote ya uwanda wa juu na eneo lote la utawala wa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala katika Heshboni. Mose alikuwa amemshinda Sihoni, pia watawala wakuu wa Wamidiani, ambao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba, waliokuwa wameungana na Sihoni, ambao waliishi katika nchi ile.
and all city [the] plain and all kingdom Sihon king [the] Amorite which to reign in/on/with Heshbon which to smite Moses [obj] him and [obj] leader Midian [obj] Evi and [obj] Rekem and [obj] Zur and [obj] Hur and [obj] Reba prince Sihon to dwell [the] land: country/planet
22 Pamoja na wale waliouawa katika vita, Waisraeli walikuwa wamemuua kwa upanga Balaamu mwana wa Beori aliyekuwa mchawi.
and [obj] Balaam son: child Beor [the] to divine to kill son: descendant/people Israel in/on/with sword to(wards) slain: killed their
23 Mpaka wa Wareubeni ulikuwa ni ukingo wa Mto Yordani. Miji hii na vijiji vyake ndiyo iliyokuwa urithi wa Wareubeni ukoo kwa ukoo.
and to be border: boundary son: descendant/people Reuben [the] Jordan and border: boundary this inheritance son: descendant/people Reuben to/for family their [the] city and village their
24 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
and to give: give Moses to/for tribe Gad to/for son: descendant/people Gad to/for family their
25 Nchi ya Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Amoni iliyoenea hadi Aroeri, karibu na Raba;
and to be to/for them [the] border: area Jazer and all city [the] Gilead and half land: country/planet son: descendant/people Ammon till Aroer which upon face: surface Rabbah
26 na kuanzia Heshboni mpaka Ramath-Mispa na Betonimu, na kutoka Mahanaimu hadi eneo la Debiri;
and from Heshbon till Ramath-mizpeh [the] Ramath-mizpeh and Betonim and from Mahanaim till border: area Debir
27 na katika bonde, Beth-Haramu, Beth-Nimra, Sukothi na Safoni na sehemu iliyobaki ya eneo la utawala wa Sihoni mfalme wa Heshboni (upande wa mashariki mwa Mto Yordani, eneo inayoishia kwenye Bahari ya Kinerethi).
and in/on/with valley Beth-haram Beth-haram and Beth-nimrah Beth-nimrah and Succoth and Zaphon remainder kingdom Sihon king Heshbon [the] Jordan and border: boundary till end sea (Sea of) Chinnereth side: beyond [the] Jordan east [to]
28 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Gadi ukoo kwa ukoo.
this inheritance son: descendant/people Gad to/for family their [the] city and village their
29 Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa hiyo nusu ya kabila la Manase, yaani kwa nusu ya jamaa ya uzao wa Manase, ukoo kwa ukoo:
and to give: give Moses to/for half tribe Manasseh and to be to/for half tribe son: descendant/people Manasseh to/for family their
30 Eneo lililoenea kuanzia Mahanaimu, na kujumlisha Bashani yote, ufalme wote wa Ogu mfalme wa Bashani, makazi yote ya Yairi huko Bashani, miji sitini,
and to be border: area their from Mahanaim all [the] Bashan all kingdom Og king [the] Bashan and all village Jair which in/on/with Bashan sixty city
31 nusu ya Gileadi, na Ashtarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Hii ilikuwa kwa ajili ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, kwa ajili ya nusu ya wana wa Makiri, ukoo kwa ukoo.
and half [the] Gilead and Ashtaroth and Edrei city kingdom Og in/on/with Bashan to/for son: descendant/people Machir son: child Manasseh to/for half son: descendant/people Machir to/for family their
32 Huu ndio urithi alioupeana Mose wakati alipokuwa katika tambarare za Moabu, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
these which to inherit Moses in/on/with Plains (of Moab) (Plains of) Moab from side: beyond to/for Jordan Jericho east [to]
33 Lakini kwa kabila la Walawi, Mose hakuwapa urithi; Bwana Mungu, Mungu wa Israeli ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
and to/for tribe [the] Levi not to give: give Moses inheritance LORD God Israel he/she/it inheritance their like/as as which to speak: speak to/for them

< Yoshua 13 >