< Yoshua 12 >
1 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
이스라엘 자손이 요단 저편 해 돋는 편 곧 아르논 골짜기에서 헤르몬 산까지의 동방 온 아라바를 점령하고 그 땅에서 쳐 죽인 왕들은 이러하니라
2 Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
헤스본에 거하던 아모리 사람의 왕 시혼이라 그 다스리던 땅은 아르논 골짜기 가에 있는 아로엘에서부터 골짜기 가운데 성읍과 길르앗 절반 곧 암몬 자손의 지경 얍복 강까지며
3 Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
또 동방 아라바 긴네롯 바다까지며 또 동방 아라바의 바다 곧 염해의 벧여시못으로 통한 길까지와 남편으로 비스가 산록까지며
4 Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
또 르바의 남은 족속으로서 아스다롯과 에브레이에 거하던 바산 왕 옥이라
5 Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
그 치리하던 땅은 헤르몬 산과 살르가와 온 바산과 및 그술 사람과 마아가 사람의 지경까지의 길르앗 절반이니 헤스본 왕 시혼의 지경에 접한 것이라
6 Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
여호와의 종 모세와 이스라엘 자손이 그들을 치고 여호와의 종 모세가 그 땅을 르우벤 사람과 갓 사람과 므낫세 반 지파에게 기업으로 주었더라
7 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
여호수아와 이스라엘 자손이 요단 이편 곧 서편 레바논 골짜기의 바알갓에서부터 세일로 올라가는 곳 할락 산까지에서 쳐서 멸한 왕들은 이러하니 (그 땅을 여호수아가 이스라엘의 구별을 따라 그 지파에게 기업으로 주었으니
8 nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
곧 산지와 평지와 아라바와 경사지와 광야와 남방 곧 헷 사람과 아모리 사람과 가나안 사람과 브리스 사람과 히위 사람과 여부스 사람의 땅이라)
9 mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
하나는 여리고 왕이요 하나는 벧엘 곁의 아이 왕이요
10 mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
하나는 예루살렘 왕이요 하나는 헤브론 왕이요 하나는 야르뭇 왕이요
11 mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
하나는 라기스 왕이요
12 mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
하나는 에글론 왕이요 하나는 게셀 왕이요
13 mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
하나는 드빌 왕이요 하나는 게델 왕이요
14 mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
하나는 호르마 왕이요 하나는 아랏 왕이요
15 mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
하나는 립나 왕이요 하나는 아둘람 왕이요
16 mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
하나는 막게다 왕이요 하나는 벧엘 왕이요
17 mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
하나는 답부아 왕이요 하나는 헤벨 왕이요
18 mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
하나는 아벡 왕이요 하나는 랏사론 왕이요
19 mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
하나는 마돈 왕이요 하나는 하솔 왕이요
20 mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
하나는 시므론 므론 왕이요 하나는 악삽 왕이요
21 mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
하나는 다아낙 왕이요 하나는 므깃도 왕이요
22 mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
하나는 게데스 왕이요 하나는 갈멜의 욕느암 왕이요
23 mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
하나는 돌의 높은 곳의 돌 왕이요 하나는 길갈의 고임 왕이요
24 mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.
하나는 디르사 왕이라 도합 삼십일 왕이었더라