< Yoshua 12 >

1 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
Dies sind die Könige des Landes, welche die Kinder Israel schlugen und deren Land sie einnahmen jenseits des Jordan, gegen Aufgang der Sonne, von dem Bache Arnon an bis zum Berg Hermon, und die ganze Ebene gegen Morgen:
2 Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
Sihon, der König der Amoriter, der zu Hesbon wohnte und herrschte von Aroer an, das am Ufer des Baches Arnon liegt, und über die Mitte des Tales und über das halbe Gilead und bis an den Bach Jabbok, der die Grenze der Kinder Ammon ist,
3 Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
und über die Ebene bis an den See Genezaret gegen Morgen und bis an das Meer der Ebene, nämlich das Salzmeer gegen Morgen am Wege gen Beth-Jesimot; und von Teman an unterhalb der Abhänge des Pisga.
4 Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
Dann das Gebiet des Königs Og zu Basan, der noch von den Rephaitern übrig war und zu Astarot und Edrei wohnte,
5 Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
welcher herrschte über den Berg Hermon und über Salcha und über ganz Basan, bis an die Grenze der Gessuriter und Maachiter, und über das halbe Gilead, bis zum Gebiet Sihons, des Königs zu Hesbon.
6 Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
Mose, der Knecht des HERRN, und die Kinder Israel schlugen sie. Und Mose, der Knecht des HERRN, gab sie den Rubenitern, Gaditern und dem halben Stamme Manasse zum Besitz.
7 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
Folgendes aber sind die Könige des Landes, die Josua und die Kinder Israel schlugen diesseits des Jordan, gegen Westen, von Baal-Gad an im Tale des Libanon bis an das kahle Gebirge, welches gegen Seir aufsteigt. Und Josua gab es den Stämmen Israels zum Besitz, einem jeden seinen Teil,
8 nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
auf den Gebirgen, in den Tälern, in der Ebene, an den Abhängen, in den Wüsten und gegen Mittag, die Hetiter, Amoriter, Kanaaniter, Pheresiter, Heviter und Jebusiter:
9 mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
Der König von Jericho, der König von Ai, das zur Seite von Bethel liegt,
10 mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
der König von Jerusalem, der König von Hebron,
11 mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
der König von Jarmut, der König von Lachis,
12 mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
der König von Eglon, der König von Geser,
13 mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
der König von Debir, der König von Geder,
14 mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
der König von Horma, der König von Arad,
15 mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
der König von Libna,
16 mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
der König von Adullam, der König von Makkeda,
17 mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
der König von Bethel, der König von Tappuach, der König von Hepher,
18 mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
der König von Aphek, der König von Lascharon,
19 mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
der König von Madon,
20 mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
der König von Hazor, der König von Simron-Meron, der König von Achsaph,
21 mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
der König von Taanach, der König von Megiddo,
22 mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
der König von Kedesch, der König von Jokneam am Karmel,
23 mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
der König von Dor, auf der Höhe von Dor, der König der Heiden zu Gilgal, der König von Tirza.
24 mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.
Zusammen einunddreißig Könige.

< Yoshua 12 >