< Yoshua 12 >

1 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
These ben the kyngis whiche the sones of Israel han smyte, and weldiden `the lond of hem, biyende Jordan, at the `risyng of the sunne, fro the stronde of Arnon `til to the hil of Hermon, and al the eest coost that biholdith the wildirnesse.
2 Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
Seon, the kyng of Amorreis, that dwellide in Esebon, was lord fro Aroer, which is set on the brenke of the stronde of Arnon, and of the myddil part in the valey, and of half Galaad, til to the stronde of Jaboth, which is the terme of the sones of Amon, and fro the wildirnesse `til to the see of Ceneroth,
3 Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
ayens the eest, and `til to the see of deseert, which is the saltist see at the eest coost, bi the weie that ledith to Bethessymoth, and fro the south part that liggith vndur Assedoch, `til to Phasga.
4 Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
The terme of Og, kyng of Basan, of the relikis of Raphaym, `that is, giauntis, that dwelliden in Astoroth and in Edraym, and he was lord in the hil of Hermon, and in Salacha, and in al Basan, `til to the termes of Gessuri and Machati,
5 Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
and of the half part of Galaad, and to the terme of Seon, kyng of Esebon.
6 Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
Moyses, the `seruaunt of the Lord, and the sones of Israel `smytiden hem; and Moises yaf `the lond of hem in to possessioun to Rubenytis and `to Gadditis and to half the lynage of Manaasses.
7 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
These ben the kyngis of the lond, whiche Josue and the sones of Israel smytiden biyende Jordan, at the west coost, fro Algad in the feeld of Liban, `til to the hil whos part stieth in to Seir; and Josue yaf it in to possessioun to the lynagis of Israel, to ech his owne part,
8 nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
as wel in `hilli placis as in pleyn and feeldi placis; in Asseroth, and in wildirnesse, and in the south was Ethei, and Ammorrei, Cananie, and Pheresei, Euey, and Jebusei.
9 mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
The kyng of Jerico oon; the kyng of Hai, which is at the side of Bethel, oon;
10 mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
the kyng of Jerusalem, oon; the kyng of Ebron, oon;
11 mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
the kyng of Herymoth, oon; the kyng of Lachis, oon; the kyng of Eglon, oon;
12 mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
the kyng of Gazer, oon;
13 mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
the kyng of Dabir, oon; the kyng of Gader, oon;
14 mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
the kyng of Herma, oon;
15 mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
the kyng of Hedreth, oon; the kyng of Lempna, oon; the kyng of Odollam, oon;
16 mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
the kyng of Maceda, oon; the kyng of Bethel, oon;
17 mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
the kyng of Thaphua, oon;
18 mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
the kyng of Affer, oon; the kyng of Affeth, oon; the kyng of Saron, oon; the kyng of Madon, oon;
19 mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
the king of Asor, oon;
20 mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
the kyng of Semeron, oon; the kyng of Axaph, oon;
21 mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
the kyng of Thenach, oon; the kyng of Magedo, oon; the kyng of Cetes, oon;
22 mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
the kyng of Jachanaem of Carmele, oon;
23 mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
the kyng of Dor and of the prouince of Dor, oon; the kyng of folkis of Galgal, oon;
24 mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.
the kyng of Thersa, oon; alle the kyngis, oon and thretti.

< Yoshua 12 >