< Yoshua 12 >

1 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
Now these are the kings of the land, whom the children of Israel smote, and possessed their land on the other side of Jordan toward the rising of the sun, from the river Arnon to mount Hermon, and all the plain on the east:
2 Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
Sihon king of the Amorites, who dwelt in Heshbon, and ruled from Aroer, which is upon the bank of the river Arnon, and from the middle of the river, and half Gilead, even to the river Jabbok, which is the border of the children of Ammon;
3 Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
And from the plain to the sea of Chinneroth on the east, and to the sea of the plain, even the salt sea on the east, the way to Bethjeshimoth; and from the south, under Ashdothpisgah:
4 Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
And the land of Og king of Bashan, who was of the remnant of the giants, that dwelt at Ashtaroth and at Edrei,
5 Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
And reigned in mount Hermon, and in Salcah, and in all Bashan, to the border of the Geshurites and the Maachathites, and half Gilead, the border of Sihon king of Heshbon.
6 Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
Them did Moses the servant of the LORD and the children of Israel smite: and Moses the servant of the LORD gave it for a possession to the Reubenites, and the Gadites, and the half tribe of Manasseh.
7 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
And these are the kings of the country whom Joshua and the children of Israel smote on this side of Jordan on the west, from Baalgad in the valley of Lebanon even to the mount Halak, that goeth up to Seir; which Joshua gave to the tribes of Israel for a possession according to their divisions;
8 nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
In the mountains, and in the valleys, and in the plains, and in the springs, and in the wilderness, and in the south country; the Hittites, the Amorites, and the Canaanites, the Perizzites, the Hivites, and the Jebusites:
9 mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
The king of Jericho, one; the king of Ai, which is beside Bethel, one;
10 mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
The king of Jerusalem, one; the king of Hebron, one;
11 mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
The king of Jarmuth, one; the king of Lachish, one;
12 mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
The king of Eglon, one; the king of Gezer, one;
13 mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
The king of Debir, one; the king of Geder, one;
14 mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
The king of Hormah, one; the king of Arad, one;
15 mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
The king of Libnah, one; the king of Adullam, one;
16 mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
The king of Makkedah, one; the king of Bethel, one;
17 mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
The king of Tappuah, one; the king of Hepher, one;
18 mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
The king of Aphek, one; the king of Lasharon, one;
19 mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
The king of Madon, one; the king of Hazor, one;
20 mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
The king of Shimronmeron, one; the king of Achshaph, one;
21 mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
The king of Taanach, one; the king of Megiddo, one;
22 mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
The king of Kedesh, one; the king of Jokneam of Carmel, one;
23 mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
The king of Dor in the heights of Dor, one; the king of the nations of Gilgal, one;
24 mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.
The king of Tirzah, one: all the kings thirty and one.

< Yoshua 12 >