< Yoshua 12 >

1 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
Now these are the kings of the land whom the Israelites struck down and whose lands they took beyond the Jordan to the east, from the Arnon Valley to Mount Hermon, including all the Arabah eastward:
2 Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
Sihon king of the Amorites, who lived in Heshbon. He ruled from Aroer on the rim of the Arnon Valley, along the middle of the valley, up to the Jabbok River (the border of the Ammonites), that is, half of Gilead,
3 Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
as well as the Arabah east of the Sea of Chinnereth to the Sea of the Arabah (the Salt Sea ), eastward through Beth-jeshimoth, and southward below the slopes of Pisgah.
4 Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
And Og king of Bashan, one of the remnant of the Rephaim, who lived in Ashtaroth and Edrei.
5 Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
He ruled over Mount Hermon, Salecah, all of Bashan up to the border of the Geshurites and Maacathites, and half of Gilead to the border of Sihon king of Heshbon.
6 Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
Moses, the servant of the LORD, and the Israelites had struck them down and given their land as an inheritance to the Reubenites, the Gadites, and the half-tribe of Manasseh.
7 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
And these are the kings of the land that Joshua and the Israelites conquered beyond the Jordan to the west, from Baal-gad in the Valley of Lebanon to Mount Halak, which rises toward Seir (according to the allotments to the tribes of Israel, Joshua gave them as an inheritance
8 nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
the hill country, the foothills, the Arabah, the slopes, the wilderness, and the Negev—the lands of the Hittites, Amorites, Canaanites, Perizzites, Hivites, and Jebusites):
9 mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
the king of Jericho, one; the king of Ai, which is near Bethel, one;
10 mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
the king of Jerusalem, one; the king of Hebron, one;
11 mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
the king of Jarmuth, one; the king of Lachish, one;
12 mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
the king of Eglon, one; the king of Gezer, one;
13 mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
the king of Debir, one; the king of Geder, one;
14 mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
the king of Hormah, one; the king of Arad, one;
15 mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
the king of Libnah, one; the king of Adullam, one;
16 mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
the king of Makkedah, one; the king of Bethel, one;
17 mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
the king of Tappuah, one; the king of Hepher, one;
18 mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
the king of Aphek, one; the king of Lasharon, one;
19 mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
the king of Madon, one; the king of Hazor, one;
20 mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
the king of Shimron-meron, one; the king of Achshaph, one;
21 mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
the king of Taanach, one; the king of Megiddo, one;
22 mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
the king of Kedesh, one; the king of Jokneam in Carmel, one;
23 mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
the king of Dor in Naphath-dor, one; the king of Goiim in Gilgal, one;
24 mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.
and the king of Tirzah, one. So there were thirty-one kings in all.

< Yoshua 12 >