< Yoshua 11 >

1 Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya, akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na kwa mfalme wa Akishafu,
Olup bitenleri duyan Hasor Kralı Yavin, Madon Kralı Yovav'a, Şimron ve Akşaf krallarına,
2 na pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerethi, kwenye shefela, upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi;
dağlık kuzey bölgesinde, Kinneret Gölü'nün güneyindeki Arava'da, Şefela'da ve batıda Dor Kenti sırtlarındaki krallara,
3 kwa Wakanaani upande wa mashariki na magharibi; kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi katika nchi ya vilima; na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika eneo ya Mispa.
doğu ve batı bölgelerindeki Kenan, Amor, Hitit, Periz halklarına ve dağlık bölgedeki Yevuslular'la Hermon Dağı'nın eteğindeki Mispa bölgesinde yaşayan Hivliler'e haber gönderdi.
4 Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya farasi na magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari.
Bu krallar bütün ordularıyla, kıyıların kumu kadar sayısız askerleriyle, çok sayıdaki at ve savaş arabalarıyla yola çıktılar.
5 Wafalme hawa wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja kwenye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli.
Bütün bu krallar İsrailliler'e karşı savaşmak üzere birleşerek Merom suları kıyısına gelip hep birlikte ordugah kurdular.
6 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mikononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao ya vita.”
Bu arada RAB Yeşu'ya, “Onlardan korkma” diye seslendi, “Onların hepsini yarın bu saatlerde İsrail'in önünde yere sereceğim. Atlarını sakatlayıp savaş arabalarını ateşe ver.”
7 Hivyo Yoshua pamoja na jeshi lake lote wakaja dhidi yao ghafula kwenye Maji ya Meromu kuwashambulia,
Böylece Yeşu bütün ordusuyla birlikte Merom suları kıyısındaki kralların üzerine beklenmedik bir anda yürüdü ve onlara saldırdı.
8 naye Bwana akawatia mikononi mwa Israeli. Wakawashinda na kuwafukuza hadi Sidoni Kuu na kuwafikisha Misrefoth-Maimu, hadi Bonde la Mispa upande wa mashariki, hadi pakawa hakuna yeyote aliyebaki.
RAB onları İsrailliler'in eline teslim etti. Onları bozguna uğratan İsrailliler, kaçanları Büyük Sayda'ya, Misrefot-Mayim'e ve doğuda Mispe Vadisi'ne kadar kovalayıp öldürdüler; kimseyi sağ bırakmadılar.
9 Yoshua akawatendea kama Bwana alivyoamuru. Akakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuchoma moto magari yao ya vita.
Yeşu, RAB'bin kendisine buyurduğu gibi yaptı, atlarını sakatladı, savaş arabalarını ateşe verdi.
10 Wakati huo Yoshua akarudi na kuuteka mji wa Hazori na kumuua mfalme wake kwa upanga. (Hazori ulikuwa mji mkuu wa falme hizo zote.)
Yeşu bundan sonra geri dönüp Hasor'u ele geçirdi, Hasor Kralı'nı kılıçla öldürdü. Çünkü Hasor eskiden bütün bu krallıkların başıydı.
11 Kila aliyekuwa ndani yake wakamuua kwa upanga. Wakawaangamiza kabisa, wala hawakusaza chochote chenye pumzi na akauchoma Hazori kwenyewe kwa moto.
İsrailliler kentteki bütün canlıları kılıçtan geçirip yok ettiler. Soluk alan bir tek kişiyi esirgemediler. Ardından Yeşu Hasor'u ateşe verdi.
12 Yoshua akaiteka hii miji yote ya kifalme pamoja na wafalme wake na kuwapiga kwa upanga. Akawaangamiza kabisa wote, jinsi Mose mtumishi wa Bwana alivyowaagiza.
Böylece bütün bu kentlerle krallarını ele geçirdi. RAB'bin kulu Musa'nın buyruğu uyarınca hepsini kılıçtan geçirip yok etti.
13 Lakini Israeli hawakuichoma moto hata mojawapo ya miji iliyojengwa katika vilima vyao vidogo isipokuwa mji wa Hazori ambao Yoshua aliuchoma moto.
Ancak, İsrailliler, Yeşu'nun ateşe verdiği Hasor dışında, tepe üzerinde kurulu kentlerden hiçbirini ateşe vermediler.
14 Waisraeli wakajichukulia nyara zote na mifugo yote ya miji hii, bali waliwaua watu wote kwa upanga hadi walipowaangamiza kabisa, pasipo kumbakiza yeyote mwenye pumzi.
Bu kentlerdeki bütün mal ve hayvanları ganimet olarak aldılar, insanların tümünü ise kılıçtan geçirip öldürdüler; soluk alan bir tek kişiyi esirgemediler.
15 Kama vile Bwana alivyomwagiza Mose mtumishi wake, vivyo hivyo Mose alimwagiza Yoshua, naye Yoshua akafanya kama vivyo, hakukosa kufanya lolote katika yale yote Bwana aliyomwagiza Mose.
RAB'bin kulu Musa RAB'den aldığı buyrukları Yeşu'ya aktarmıştı. Yeşu bunlara uydu ve RAB'bin Musa'ya buyurduklarını eksiksiz yerine getirdi.
16 Yoshua akaiteka nchi hii yote: nchi ya vilima, Negebu yote, eneo yote ya Gosheni, shefela ya upande wa magharibi, Araba na milima ya Israeli pamoja na shefela zao,
Böylece Yeşu, dağlık bölge, bütün Negev ve Goşen bölgesi, Şefela, Arava ve İsrail dağlarıyla bu dağların etekleri, Seir yönünde yükselen Halak Dağı'ndan Hermon Dağı'nın altındaki Lübnan Vadisi'nde bulunan Baal-Gat'a varıncaya dek bütün toprakları ele geçirdi. Buraların krallarını yakalayıp öldürdü.
17 kuanzia Mlima Halaki ambao umeinuka kuelekea Seiri hadi Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni chini ya Mlima Hermoni. Akawateka wafalme wake wote, akawapiga na kuwaua.
18 Yoshua akapigana vita dhidi ya wafalme hawa wote kwa muda mrefu.
Yeşu bu krallarla uzun süre savaştı.
19 Hakuna mji wowote katika eneo hili uliofanya mkataba wa amani na Israeli, isipokuwa hao Wahivi wa Gibeoni. Wengine wote walishindwa katika vita.
Givon'da yaşayan Hivliler dışında, İsrailliler'le barış antlaşması yapan bir kent olmadı. İsrailliler öbür kentlerin hepsini savaşarak aldılar.
20 Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Çünkü onları İsrail'e karşı savaşmaya kararlı yapan RAB'bin kendisiydi. Böylece RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi, İsrailliler onlara acımadı, hepsini öldürüp yok ettiler.
21 Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
Yeşu bundan sonra Anaklılar'ın üzerine yürüdü. Onları dağlık bölgeden, Hevron, Devir ve Anav'dan, Yahuda ve İsrail'in bütün dağlık bölgelerinden söküp attı. Kentleriyle birlikte onları tümüyle yok etti.
22 Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
İsrailliler'in elindeki topraklarda hiç Anaklı kalmadı. Yalnız Gazze, Gat ve Aşdot'ta sağ kalanlar oldu.
23 Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.
RAB'bin Musa'ya söylediği gibi, Yeşu bütün ülkeyi ele geçirdi ve İsrail oymakları arasında mülk olarak bölüştürdü. Böylece savaş sona erdi, ülke barışa kavuştu.

< Yoshua 11 >