< Yoshua 11 >
1 Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya, akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na kwa mfalme wa Akishafu,
Ke pweng ke kutangla lun Israel inge sonol Tokosra Jabin lun acn Hazor, el sapla nu sel Tokosra Jobab lun mwet Madon, ac nu sin tokosra lun acn Shimron ac acn Achshaph,
2 na pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerethi, kwenye shefela, upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi;
ac nu sin tokosra nukewa fin acn tohktok in acn epang, ac Infahlfal Jordan eir in Lulu Galilee, ac pe eol uh, ac sisken meoa apkuran nu Dor.
3 kwa Wakanaani upande wa mashariki na magharibi; kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi katika nchi ya vilima; na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika eneo ya Mispa.
El oayapa supwala kas nu sin mwet Canaan lefahl kutulap ac roto Infacl Jordan, ac nu sin mwet Amor, ac nu sin mwet Hit, ac nu sin mwet Periz, ac nu sin mwet Jebus su muta fineol uh, ac nu sin mwet Hiv su muta pe Fineol Hermon in acn Mizpah.
4 Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya farasi na magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari.
Elos tuku wi mwet mweun puspis lalos, ac pisalos pus oana puk weacn uh. Oayapa pus horse ac chariot natulos.
5 Wafalme hawa wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja kwenye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli.
Tokosra inge nukewa wi mwet mweun lalos elos tukeni tuku ac tulokunak lohm nuknuk selos sisken infacl srisrik Merom, ac akola in mweun lain mwet Israel.
6 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mikononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao ya vita.”
LEUM GOD El fahk nu sel Joshua, “Nik kom sangeng selos, tuh pacl se inge lutu, nga fah onelosla nufon ke sripen Israel. Kom fah pakiya alko ke nien horse natulos, ac esukak chariot natulos.”
7 Hivyo Yoshua pamoja na jeshi lake lote wakaja dhidi yao ghafula kwenye Maji ya Meromu kuwashambulia,
Na Joshua ac mwet lal nukewa sa na sruokolosi meet liki elos akola sisken infacl srisrik Merom.
8 naye Bwana akawatia mikononi mwa Israeli. Wakawashinda na kuwafukuza hadi Sidoni Kuu na kuwafikisha Misrefoth-Maimu, hadi Bonde la Mispa upande wa mashariki, hadi pakawa hakuna yeyote aliyebaki.
LEUM GOD El sang kutangla nu sin Israel fin mwet inge. Mwet Israel lainulos ac ukwalos nwe Misrephoth Maim ac Sidon nu eir, oayapa nwe ke Infahlfal Mizpah nu kutulap. Elos mweunelos nwe ke na wangin sie moul.
9 Yoshua akawatendea kama Bwana alivyoamuru. Akakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuchoma moto magari yao ya vita.
Joshua el oru nu selos oana ma LEUM GOD El sapkin — el pakela alko ke nien horse natulos ac esukak chariot natulos.
10 Wakati huo Yoshua akarudi na kuuteka mji wa Hazori na kumuua mfalme wake kwa upanga. (Hazori ulikuwa mji mkuu wa falme hizo zote.)
Na Joshua el forla sruokya acn Hazor, ac uniya tokosra se lun acn we. (In pacl sac acn Hazor pa ku fin mutunfacl ingo kewa.)
11 Kila aliyekuwa ndani yake wakamuua kwa upanga. Wakawaangamiza kabisa, wala hawakusaza chochote chenye pumzi na akauchoma Hazori kwenyewe kwa moto.
Elos onelosla nufon mwet in acn sac. Wangin sie mwet lula. Na elos esukak siti sac.
12 Yoshua akaiteka hii miji yote ya kifalme pamoja na wafalme wake na kuwapiga kwa upanga. Akawaangamiza kabisa wote, jinsi Mose mtumishi wa Bwana alivyowaagiza.
Joshua el sruokya siti ingo kewa, oayapa tokosra lalos. El onelosla nufon, oana ma Moses, mwet kulansap lun LEUM GOD, el tuh sapkin.
13 Lakini Israeli hawakuichoma moto hata mojawapo ya miji iliyojengwa katika vilima vyao vidogo isipokuwa mji wa Hazori ambao Yoshua aliuchoma moto.
Tusruktu, mwet Israel elos tia esukak kutena siti su musala fin pwelung matu, sayen Hazor mukena, su Joshua el tuh esukak.
14 Waisraeli wakajichukulia nyara zote na mifugo yote ya miji hii, bali waliwaua watu wote kwa upanga hadi walipowaangamiza kabisa, pasipo kumbakiza yeyote mwenye pumzi.
Mwet Israel elos eis mwe kasrup ac kosro nut nukewa liki siti inge tuh in ma lalos. A elos uniya mwet nukewa, ac wangin sie lula.
15 Kama vile Bwana alivyomwagiza Mose mtumishi wake, vivyo hivyo Mose alimwagiza Yoshua, naye Yoshua akafanya kama vivyo, hakukosa kufanya lolote katika yale yote Bwana aliyomwagiza Mose.
LEUM GOD El tuh sang ma sap lal nu sel Moses, mwet kulansap lal, ac Moses el sang nu sel Joshua, ac Joshua el akos. El oru ma nukewa oana ma LEUM GOD El tuh sapkin nu sel Moses.
16 Yoshua akaiteka nchi hii yote: nchi ya vilima, Negebu yote, eneo yote ya Gosheni, shefela ya upande wa magharibi, Araba na milima ya Israeli pamoja na shefela zao,
Joshua el sruokya kewa acn inge, acn fineol uh ac pe eol uh, epang ac eir, oayapa acn Goshen nufon ac acn mwesis nu eir, ac Infahlfal Jordan.
17 kuanzia Mlima Halaki ambao umeinuka kuelekea Seiri hadi Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni chini ya Mlima Hermoni. Akawateka wafalme wake wote, akawapiga na kuwaua.
Lupan mutunfacl se inge mutawauk ke Fineol Halak nu eir apkuran nu Edom, fahla nwe ke acn Baalgad nu epang, ke Infahlfal Lebanon su oan eir in Fineol Hermon.
18 Yoshua akapigana vita dhidi ya wafalme hawa wote kwa muda mrefu.
Joshua el tuh mweuni tokosra lun acn inge ke pulan pacl na loes se. Tusruktu, el sruokolosi kewa ac el onelosla.
19 Hakuna mji wowote katika eneo hili uliofanya mkataba wa amani na Israeli, isipokuwa hao Wahivi wa Gibeoni. Wengine wote walishindwa katika vita.
Siti sefanna ma tuh orala misla yurin mwet Israel pa Gibeon, su pa inge acn se ma kutu sin mwet Hiv muta we. Siti nukewa saya sruhu ke mweun.
20 Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
LEUM GOD El pirik insien mwet inge tuh elos in lungse mweun lain mwet Israel, elos in mau arulana sikiyukla ac anwuki nufon, in kalem lah wangin pakomuta nu selos. Pa inge ma LEUM GOD El tuh sapkin nu sel Moses.
21 Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
In pacl se inge Joshua el som ac onelosla mwet yohk pisa ac ku su pangpang Anakim su muta fineol uh in acn Hebron, Debir, Anab, ac infulan eol in Judah ac Israel. Joshua el kunauselosla nukewa wi siti selos.
22 Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
Wangin mwet Anakim lula in facl sin mwet Israel. Tusruktu mwet ekasrna selos lula in acn Gaza, Gath, ac Ashdod.
23 Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.
Joshua el sruokya facl sac nufon in oana ma LEUM GOD El tuh sapkin nu sel Moses. Ac Joshua el sang facl sac tuh in mwe usru nu sin mwet Israel, ac kitalik fal nu ke kais sie sruf lalos. Na mwet uh mongla liki mweun.