< Yoshua 11 >

1 Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya, akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na kwa mfalme wa Akishafu,
Jabin, roi d'Asor, ayant appris ces choses, envoya un message à Jobab, roi de Madon, au roi de Séméron, au roi d'Achsaph,
2 na pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerethi, kwenye shefela, upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi;
aux rois qui étaient au nord dans la montagne et dans l'Arabah, au sud du Cénéreth, dans le bas pays et sur les hauteurs de Dor à l'occident,
3 kwa Wakanaani upande wa mashariki na magharibi; kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi katika nchi ya vilima; na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika eneo ya Mispa.
aux Chananéens de l'orient et de l'occident, aux Amorrhéens, aux Héthéens, aux Phérézéens, aux Jébuséens dans la montagne, et aux Hévéens du pied de l'Hermon dans le pays de Maspha.
4 Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya farasi na magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari.
Ils sortirent, eux et toutes leurs armées avec eux, peuple innombrable comme le sable qui est sur le bord de la mer, avec une grande multitude de chevaux et de chars.
5 Wafalme hawa wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja kwenye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli.
Tous ces rois se rassemblèrent et vinrent camper ensemble près des eaux de Mérom, pour combattre Israël.
6 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mikononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao ya vita.”
Yahweh dit à Josué: « Ne les crains point, car demain, à cette heure-ci, je les livrerai tous transpercés devant Israël. Tu couperas les jarrets à leurs chevaux et tu livreras au feu leurs chars. »
7 Hivyo Yoshua pamoja na jeshi lake lote wakaja dhidi yao ghafula kwenye Maji ya Meromu kuwashambulia,
Josué, et tous les hommes de guerre avec lui, arrivèrent à eux à l'improviste, près des eaux de Mérom, et ils se précipitèrent sur eux.
8 naye Bwana akawatia mikononi mwa Israeli. Wakawashinda na kuwafukuza hadi Sidoni Kuu na kuwafikisha Misrefoth-Maimu, hadi Bonde la Mispa upande wa mashariki, hadi pakawa hakuna yeyote aliyebaki.
Yahweh les livra entre les mains d'Israël, qui les battit et les poursuivit jusqu'à Sidon la grande, jusqu'aux eaux de Maséréphoth et jusqu'à la vallée de Maspha vers l'orient; il les battit, sans en laisser échapper un seul.
9 Yoshua akawatendea kama Bwana alivyoamuru. Akakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuchoma moto magari yao ya vita.
Josué les traita comme Yahweh le lui avait dit: il coupa les jarrets à leurs chevaux et il livra au feu leurs chars.
10 Wakati huo Yoshua akarudi na kuuteka mji wa Hazori na kumuua mfalme wake kwa upanga. (Hazori ulikuwa mji mkuu wa falme hizo zote.)
En ce même temps, Josué revint et prit Asor, et il frappa son roi de l'épée; car Asor était autrefois la capitale de tous ces royaumes.
11 Kila aliyekuwa ndani yake wakamuua kwa upanga. Wakawaangamiza kabisa, wala hawakusaza chochote chenye pumzi na akauchoma Hazori kwenyewe kwa moto.
Les enfants d'Israël frappèrent du tranchant de l'épée tous les êtres vivants qui s'y trouvaient, en les dévouant par anathème; il ne resta rien de ce qui avait vie, et l'on brûla Asor.
12 Yoshua akaiteka hii miji yote ya kifalme pamoja na wafalme wake na kuwapiga kwa upanga. Akawaangamiza kabisa wote, jinsi Mose mtumishi wa Bwana alivyowaagiza.
Josué prit toutes les villes de ces rois et tous leurs rois, et il les frappa du tranchant de l'épée, les dévouant par anathème, comme l'avait ordonné Moïse, serviteur de Yahweh.
13 Lakini Israeli hawakuichoma moto hata mojawapo ya miji iliyojengwa katika vilima vyao vidogo isipokuwa mji wa Hazori ambao Yoshua aliuchoma moto.
Mais Israël ne brûla aucune des villes situées sur les collines, à l'exception seulement d'Asor, que brûla Josué.
14 Waisraeli wakajichukulia nyara zote na mifugo yote ya miji hii, bali waliwaua watu wote kwa upanga hadi walipowaangamiza kabisa, pasipo kumbakiza yeyote mwenye pumzi.
Et tout le butin de ces villes, et leur bétail, les enfants d'Israël le pillèrent pour eux; mais ils frappèrent tous les hommes du tranchant de l'épée, jusqu'à ce qu'ils les eussent détruits, sans rien laisser de ce qui avait vie.
15 Kama vile Bwana alivyomwagiza Mose mtumishi wake, vivyo hivyo Mose alimwagiza Yoshua, naye Yoshua akafanya kama vivyo, hakukosa kufanya lolote katika yale yote Bwana aliyomwagiza Mose.
Ce que Yahweh avait ordonné à Moïse, son serviteur, Moïse l'avait ordonné à Josué, et Josué l'exécuta; il ne négligea rien de ce que Yahweh avait ordonné à Moïse.
16 Yoshua akaiteka nchi hii yote: nchi ya vilima, Negebu yote, eneo yote ya Gosheni, shefela ya upande wa magharibi, Araba na milima ya Israeli pamoja na shefela zao,
C'est ainsi que Josué s'empara de tout ce pays, de la Montagne, de tout le Négéb, de tout le district de Gosen, du bas pays, de l'Arabah, de la montagne d'Israël et de ses plaines,
17 kuanzia Mlima Halaki ambao umeinuka kuelekea Seiri hadi Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni chini ya Mlima Hermoni. Akawateka wafalme wake wote, akawapiga na kuwaua.
depuis la montagne nue qui s'élève vers Séïr jusqu'à Baal-Gad, dans la vallée du Liban, au pied du mont Hermon; il prit tous leurs rois, les frappa et les mit à mort.
18 Yoshua akapigana vita dhidi ya wafalme hawa wote kwa muda mrefu.
Pendant de longs jours Josué fit la guerre contre tous ces rois.
19 Hakuna mji wowote katika eneo hili uliofanya mkataba wa amani na Israeli, isipokuwa hao Wahivi wa Gibeoni. Wengine wote walishindwa katika vita.
Il n'y eut aucune ville qui fit la paix avec les enfants d'Israël, excepté les Hévéens qui habitaient à Gabaon; ils les prirent toutes par la force des armes.
20 Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Car c'était le dessein de Yahweh que ces peuples endurcissent leur cœur pour faire la guerre à Israël, afin qu'Israël les dévouât par anathème, sans qu'il y eût pour eux de miséricorde, et qu'il les détruisit, comme Yahweh l'avait ordonné à Moïse.
21 Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
Dans le même temps, Josué se mit en marche et il extermina les Enacim de la Montagne, d'Hébron, de Dabir et d'Anab, de toute la montagne de Juda et de toute la montagne d'Israël; Josué les dévoua par anathème avec leurs villes.
22 Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
Il ne resta plus d'Enacim dans le pays des enfants d'Israël; il n'en resta qu'à Gaza, à Geth et à Azoth.
23 Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.
Josué s'empara de tout le pays, selon tout ce que Yahweh avait dit à Moïse; et Josué le donna en héritage à Israël, par portions, selon leurs tribus. Et le pays se reposa de la guerre.

< Yoshua 11 >