< Yoshua 11 >

1 Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya, akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na kwa mfalme wa Akishafu,
And it was when heard Jabin [the] king of Hazor and he sent to Jobab [the] king of Madon and to [the] king of Shimron and to [the] king of Acshaph.
2 na pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerethi, kwenye shefela, upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi;
And to the kings who [were] from [the] north in the hill country and in the Arabah south of Kinnereth and in the Shephelah and on [the] heights of Dor from [the] west.
3 kwa Wakanaani upande wa mashariki na magharibi; kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi katika nchi ya vilima; na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika eneo ya Mispa.
The Canaanite[s] from [the] east and from [the] west and the Amorite[s] and the Hittite[s] and the Perizzite[s] and the Jebusite[s] in the hill country and the Hivite[s] under Hermon in [the] land of Mizpah.
4 Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya farasi na magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari.
And they came out they and all armies their with them a people numerous like the sand which [is] on [the] shore of the sea for multitude and horse[s] and chariot[s] many very.
5 Wafalme hawa wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja kwenye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli.
And they gathered all the kings these and they came and they encamped together to [the] water of Merom to wage war with Israel.
6 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mikononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao ya vita.”
And he said Yahweh to Joshua may not you be afraid because of them for tomorrow about the time this I [am] delivering up all of them slain before Israel horses their you will hamstring and chariots their you will burn with fire.
7 Hivyo Yoshua pamoja na jeshi lake lote wakaja dhidi yao ghafula kwenye Maji ya Meromu kuwashambulia,
And he came Joshua and all [the] people of war with him on them at [the] waters of Merom suddenly and they fell on them.
8 naye Bwana akawatia mikononi mwa Israeli. Wakawashinda na kuwafukuza hadi Sidoni Kuu na kuwafikisha Misrefoth-Maimu, hadi Bonde la Mispa upande wa mashariki, hadi pakawa hakuna yeyote aliyebaki.
And he gave them Yahweh in [the] hand of Israel and they struck down them and they pursued them to Sidon great and to Misrephoth Maim and to [the] valley of Mizpah east-wards and they struck down them until not he had left to them a survivor.
9 Yoshua akawatendea kama Bwana alivyoamuru. Akakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuchoma moto magari yao ya vita.
And he did to them Joshua just as he had said to him Yahweh horses their he hamstrung and chariots their he burned with fire.
10 Wakati huo Yoshua akarudi na kuuteka mji wa Hazori na kumuua mfalme wake kwa upanga. (Hazori ulikuwa mji mkuu wa falme hizo zote.)
And he turned back Joshua at the time that and he captured Hazor and king its he struck with the sword for Hazor before it [was] [the] head of all the kingdoms these.
11 Kila aliyekuwa ndani yake wakamuua kwa upanga. Wakawaangamiza kabisa, wala hawakusaza chochote chenye pumzi na akauchoma Hazori kwenyewe kwa moto.
And they struck every person who [was] in it to [the] mouth of [the] sword they totally destroyed [them] not it was left any breathing thing and Hazor he burned with fire.
12 Yoshua akaiteka hii miji yote ya kifalme pamoja na wafalme wake na kuwapiga kwa upanga. Akawaangamiza kabisa wote, jinsi Mose mtumishi wa Bwana alivyowaagiza.
And all [the] cities of the kings these and all kings their he captured Joshua and he struck them to [the] mouth of [the] sword he totally destroyed them just as he had commanded Moses [the] servant of Yahweh.
13 Lakini Israeli hawakuichoma moto hata mojawapo ya miji iliyojengwa katika vilima vyao vidogo isipokuwa mji wa Hazori ambao Yoshua aliuchoma moto.
Only all the cities which were standing on mounds their not it burned them Israel except Hazor to alone it he burned Joshua.
14 Waisraeli wakajichukulia nyara zote na mifugo yote ya miji hii, bali waliwaua watu wote kwa upanga hadi walipowaangamiza kabisa, pasipo kumbakiza yeyote mwenye pumzi.
And all [the] booty of the cities these and the cattle they plundered for themselves [the] people of Israel only every man they struck to [the] mouth of [the] sword until had destroyed they them not they left any breathing thing.
15 Kama vile Bwana alivyomwagiza Mose mtumishi wake, vivyo hivyo Mose alimwagiza Yoshua, naye Yoshua akafanya kama vivyo, hakukosa kufanya lolote katika yale yote Bwana aliyomwagiza Mose.
Just as he had commanded Yahweh Moses servant his so he commanded Moses Joshua and so he did Joshua not he left undone anything from all that he had commanded Yahweh Moses.
16 Yoshua akaiteka nchi hii yote: nchi ya vilima, Negebu yote, eneo yote ya Gosheni, shefela ya upande wa magharibi, Araba na milima ya Israeli pamoja na shefela zao,
And he took Joshua all the land this the hill country and all the Negev and all [the] land of Goshen and the Shephelah and the Arabah and [the] hill country of Israel and Shephelah its.
17 kuanzia Mlima Halaki ambao umeinuka kuelekea Seiri hadi Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni chini ya Mlima Hermoni. Akawateka wafalme wake wote, akawapiga na kuwaua.
From the mountain Halak which goes up Seir and to Baal Gad in [the] valley of Lebanon under [the] mountain of Hermon and all kings their he captured and he struck them and he killed them.
18 Yoshua akapigana vita dhidi ya wafalme hawa wote kwa muda mrefu.
Days many he did Joshua with all the kings these battle.
19 Hakuna mji wowote katika eneo hili uliofanya mkataba wa amani na Israeli, isipokuwa hao Wahivi wa Gibeoni. Wengine wote walishindwa katika vita.
Not it was a city which it made peace to [the] people of Israel except the Hivite[s] [the] inhabitants of Gibeon everything they took in battle.
20 Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
For from with Yahweh - it was to strengthen heart their to meet the battle with Israel so as to totally destroy them to not to belong to them favor for so as to destroy them just as he had commanded Yahweh Moses.
21 Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
And he came Joshua at the time that and he cut off the Anakites from the hill country from Hebron from Debir from Anab and from all [the] hill country of Judah and from all [the] hill country of Israel with cities their he totally destroyed them Joshua.
22 Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
Not it was left Anakites in [the] land of [the] people of Israel only in Gaza in Gath and in Ashdod they remained.
23 Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.
And he took Joshua all the land according to all that he had spoken Yahweh to Moses and he gave it Joshua to an inheritance to Israel according to divisions their to tribes their and the land it was at peace from war.

< Yoshua 11 >