< Yoshua 11 >

1 Ikawa Yabini mfalme wa Hazori aliposikia habari za mambo haya, akatuma ujumbe kwa Yobabu mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na kwa mfalme wa Akishafu,
Hote kamthang teh Hazar siangpahrang Jabin ni a thai torei teh, Madon siangpahrang Jobab, Shimron siangpahrang Akshaph siangpahrangnaw koehai thoseh,
2 na pia kwa wafalme wa upande wa kaskazini wale waliokuwa milimani, katika Araba upande wa kusini mwa Kinerethi, kwenye shefela, upande wa magharibi na katika miinuko ya Nafoth-Dori upande wa magharibi;
Mon dawk atunglah Khinneroth kho koe lah, tanghling dawk kaawm e, kanîloumlah kaawm e Dor ram dawk kaawm e, siangpahrangnaw koehai thoseh,
3 kwa Wakanaani upande wa mashariki na magharibi; kwa Waamori, Wahiti, Waperizi na Wayebusi katika nchi ya vilima; na kwa Wahivi chini ya Hermoni katika eneo ya Mispa.
Kanîtho, kanîloumlah kaawm e Kanaannaw, mon dawk kaawm e Amornaw, Hitnaw, Periznaw, Jebusitnaw, Mizpah ram, hermon mon rahim kaawm e Hivnaw, aonae koe lah, a patoun teh,
4 Wakaja na vikosi vyao vyote na hesabu kubwa ya farasi na magari ya kuvutwa na farasi, jeshi kubwa, kama wingi wa mchanga ulio pwani ya bahari.
Hote siangpahrangnaw teh, palang e sadi touk thai hoeh e yit touh, marangnaw, ranglengnaw, ransanaw, hoi a tâco awh.
5 Wafalme hawa wote wakaunganisha majeshi yao na kupiga kambi pamoja kwenye Maji ya Meromu, ili kupigana dhidi ya Israeli.
Hote siangpahrang abuemlah ni a kamkhueng awh teh, Isarelnaw tuk hanelah, a tho awh teh, Merom tui e teng vah cungtalah a roe awh.
6 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope, kwa sababu kesho saa kama hii nitawatia wote mikononi mwa Israeli, wakiwa wameuawa. Utakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuyachoma moto magari yao ya vita.”
BAWIPA ni ahnimanaw taket hanh awh. Kai ni tangtho e hnin dawk Isarelnaw hmalah ahnimouh abuemlah kadout tangcoung e lah na poe awh han. Marang e khok tharuinaw na bouk awh han. Ranglengnaw hah hmai na sawi awh han telah Joshua koe kâ a poe.
7 Hivyo Yoshua pamoja na jeshi lake lote wakaja dhidi yao ghafula kwenye Maji ya Meromu kuwashambulia,
Joshua ni amae ransanaw abuemlah hoi Merom tie hmuen koe pouk laipalah a cei teh a tuk awh.
8 naye Bwana akawatia mikononi mwa Israeli. Wakawashinda na kuwafukuza hadi Sidoni Kuu na kuwafikisha Misrefoth-Maimu, hadi Bonde la Mispa upande wa mashariki, hadi pakawa hakuna yeyote aliyebaki.
BAWIPA ni ahnimouh teh, Isarelnaw e a kut dawk a poe teh a thei awh. Sidon kho, Misrephothmaim kho, kanîtholah Mizpah tanghling totouh, a pâlei awh teh, buet touh hai pâhlung laipalah a thei awh.
9 Yoshua akawatendea kama Bwana alivyoamuru. Akakata mishipa ya nyuma ya miguu ya farasi wao na kuchoma moto magari yao ya vita.
BAWIPA ni kâ poe e patetlah Joshua ni marang e khok tharuinaw a bouk pouh teh ranglengnaw hmai a sawi pouh awh.
10 Wakati huo Yoshua akarudi na kuuteka mji wa Hazori na kumuua mfalme wake kwa upanga. (Hazori ulikuwa mji mkuu wa falme hizo zote.)
Hahoi Joshua ni Hazar kho bout a tuk teh, siangpahrang hah tahloi hoi a thei. Hatnae tueng dawkvah, Hazor kho ni hote ramnaw hah a uk.
11 Kila aliyekuwa ndani yake wakamuua kwa upanga. Wakawaangamiza kabisa, wala hawakusaza chochote chenye pumzi na akauchoma Hazori kwenyewe kwa moto.
Kho thung e tami pueng hah tahloi hoi a thei awh teh, buet touh hai hring sak awh hoeh. Koung a raphoe awh teh, kho hai hmai a sawi awh.
12 Yoshua akaiteka hii miji yote ya kifalme pamoja na wafalme wake na kuwapiga kwa upanga. Akawaangamiza kabisa wote, jinsi Mose mtumishi wa Bwana alivyowaagiza.
BAWIPA Cathut e san Mosi koe kâ a poe e patetlah hote siangpahrangnaw ni a uk e khonaw pueng hoi siangpahrangnaw abuemlah, Joshua ni a tuk teh, tahloi hoi koung a thei.
13 Lakini Israeli hawakuichoma moto hata mojawapo ya miji iliyojengwa katika vilima vyao vidogo isipokuwa mji wa Hazori ambao Yoshua aliuchoma moto.
Hatei, Hazor kho dei laipalah, alouklah mon dawk kaawm e kho pueng teh, Isarelnaw ni hmaisawi awh hoeh. Hazor kho buet touh dueng hah Joshua ni hmai a sawi.
14 Waisraeli wakajichukulia nyara zote na mifugo yote ya miji hii, bali waliwaua watu wote kwa upanga hadi walipowaangamiza kabisa, pasipo kumbakiza yeyote mwenye pumzi.
Hote khonaw dawk e hnopainaw hoi saring kaawm e pueng Isarelnaw ni amamouh hane a la awh. Taminaw koung a thei hoehroukrak tahloi hoi a thei awh. Buet touh hai kahring e awm sak awh hoeh.
15 Kama vile Bwana alivyomwagiza Mose mtumishi wake, vivyo hivyo Mose alimwagiza Yoshua, naye Yoshua akafanya kama vivyo, hakukosa kufanya lolote katika yale yote Bwana aliyomwagiza Mose.
BAWIPA Cathut ni amae san Mosi koe kâ a poe e patetlah Mosi ni Joshua koe patuen a dei pouh. Joshua ni hai telah a sak. BAWIPA ni Mosi koe kâ a poe e pueng a sak hoeh e buet touh hai awm hoeh.
16 Yoshua akaiteka nchi hii yote: nchi ya vilima, Negebu yote, eneo yote ya Gosheni, shefela ya upande wa magharibi, Araba na milima ya Israeli pamoja na shefela zao,
Hote Seir lam dawk kaawm e Halak mon koehoi Harmon mon a rahim,
17 kuanzia Mlima Halaki ambao umeinuka kuelekea Seiri hadi Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni chini ya Mlima Hermoni. Akawateka wafalme wake wote, akawapiga na kuwaua.
Lebanon tanghling dawk kaawm e Baalgad kho totouh, mon dawk e, mon hoi akalae hmuen Goshen ram tanghlingnaw, Isarel mon, Isarel tanghling hoi hote ram abuemlah Joshua ni a la teh, siangpahrangnaw abuemlah a tâ teh, koung a thei.
18 Yoshua akapigana vita dhidi ya wafalme hawa wote kwa muda mrefu.
Hote siangpahrangnaw pueng hah atueng moikasawlah a tuk.
19 Hakuna mji wowote katika eneo hili uliofanya mkataba wa amani na Israeli, isipokuwa hao Wahivi wa Gibeoni. Wengine wote walishindwa katika vita.
Hivnaw, Gibeon khonaw dei laipalah Isarelnaw hoi huikonae ka tawn e kho buet touh hai awm hoeh. Alouke khonaw pueng a tuk awh teh, a tâ e pueng a la awh.
20 Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Bangkongtetpawiteh, BAWIPA Cathut ni Mosi koe kâ a poe e patetlah hote taminaw koe pahrennae awm laipalah, abuemlah koung pâmit sak hanelah a ngam totouh a lungthin ka patak sak e lah, BAWIPA Cathut a ma ngainae doeh.
21 Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
Hatnae tueng nah, Joshua ni a cei teh, Anakim taminaw mon dawk kaawm e Hebron kho, Debir kho, Anab kho, Judah mon, Isarel mon kaawm e pueng, khonaw koung a raphoe teh, hote khonaw khuehoi koung a raphoe.
22 Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
Gaza kho, Gath kho, Asdod kho, hoeh laipalah, Isarel ram thung dawk kaawm e Anakim taminaw buet touh hai awm hoeh.
23 Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.
BAWIPA ni Mosi koe kâ a poe e patetlah Joshua ni hote ram pueng a la teh, Isarelnaw râw lah lengkaleng a poe teh, ram pueng dawk taran teh a roum.

< Yoshua 11 >