< Yoshua 10 >
1 Baada ya haya Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu alisikia kuwa Yoshua alikuwa ameteka mji wa Ai na kuuangamiza kabisa, tena alikuwa ameua mfalme wake, kama alivyofanya huko Yeriko na mfalme wake, tena ya kuwa watu wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli, na walikuwa wakiishi karibu yao.
Pripetilo se je torej, ko je jeruzalemski kralj Adoní Cedek slišal, kako je Józue zavzel Aj in ga popolnoma uničil; kakor je storil Jerihi in njenemu kralju, tako je storil Aju in njegovemu kralju; in kako so prebivalci Gibeóna sklenili mir z Izraelom in so bili med njimi;
2 Yeye na watu wake wakataharuki mno kwa kuwa Gibeoni ulikuwa mji mkubwa kama mmojawapo ya miji ya kifalme; ulikuwa mkubwa kuliko Ai, nao watu wake wote walikuwa mashujaa wa vita.
da so se silno bali, ker je bil Gibeón veliko mesto, kakor eno izmed kraljevskih mest in ker je bil večji kakor Aj in vsi njihovi možje so bili mogočni.
3 Hivyo Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu akaomba msaada kwa Hohamu mfalme wa Hebroni, Piramu mfalme wa Yarmuthi, Yafia mfalme wa Lakishi, na Debiri mfalme wa Egloni.
Zato je jeruzalemski kralj Adoní Cedek poslal k Hohámu, kralju v Hebrónu in Pirámu, kralju v Jarmútu in Jafíju, kralju v Lahíšu in Debírju, kralju v Eglónu, rekoč:
4 Akawaambia, “Njooni mnisaidie kuipiga Gibeoni, kwa sababu imefanya mapatano ya amani na Yoshua na Waisraeli.”
»Pridite gor k meni in mi pomagajte, da bomo lahko udarili Gibeón, kajti ta je sklenil mir z Józuetom in z Izraelovimi otroki.«
5 Ndipo hao wafalme watano wa Waamori, ambao ni wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni, wakaunganisha majeshi yao. Wakapanda na vikosi vyao vyote, nao wakajipanga dhidi ya Gibeoni na kuishambulia.
Zato se je pet kraljev izmed Amoréjcev, kralj iz Jeruzalema, kralj iz Hebróna, kralj iz Jarmúta, kralj iz Lahíša in kralj iz Eglóna, zbralo skupaj in odšlo gor, oni in vse njihove vojske in se utaborili pred Gibeónom in začeli vojno zoper njega.
6 Nao Wagibeoni wakatuma ujumbe kwa Yoshua kwenye kambi ya Gilgali na kumwambia, “Usiwatelekeze watumishi wako. Panda haraka uje kwetu kutuokoa! Tusaidie, kwa sababu wafalme wote wa Waamori wakaao kwenye nchi ya vilima wameunganisha majeshi yao pamoja dhidi yetu.”
Možje iz Gibeóna so poslali k Józuetu, v tabor pri Gilgálu, rekoč: »Ne odtegni svoje roke od svojih služabnikov. Hitro pridi gor k nam in nas reši in nam pomagaj, kajti vsi kralji Amoréjcev, ki prebivajo po gorah, so skupaj zbrani zoper nas.«
7 Basi Yoshua akaondoka Gilgali pamoja na jeshi lake lote, wakiwepo watu wote mashujaa wa vita.
Tako se je Józue vzpel iz Gilgála, on in vse bojno ljudstvo z njim in vsi močni junaški možje.
8 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope watu hao, nimewatia mkononi mwako. Hakuna yeyote atakayeweza kushindana nawe.”
Gospod je rekel Józuetu: »Ne boj se jih, kajti izročil sem jih v tvojo roko. Niti mož izmed njih ne bo obstal pred teboj.«
9 Baada ya Yoshua kutembea usiku kucha kutoka Gilgali, akawashambulia ghafula.
Józue je torej nenadoma prišel k njim in vso noč so hodili gor od Gilgála.
10 Bwana akawafadhaisha mbele ya Waisraeli, nao wakawashinda kwa ushindi mkuu huko Gibeoni. Israeli wakawafukuza kuelekea njia iendayo Beth-Horoni wakiwaua mpaka kufikia njia iendayo Azeka na Makeda.
Gospod jih je porazil pred Izraelom ter jih pri Gibeónu usmrtil z velikim pobojem in jih zasledoval na poti, ki gre gor do Bet Horóna in jih udarjal do Azéke in proti Makédi.
11 Walipokuwa wakikimbia mbele ya Israeli kwenye barabara iteremkayo kutoka Beth-Horoni hadi Azeka, Bwana akawavumishia mawe makubwa ya mvua kutoka mbinguni, na wengi wao wakauawa na hayo mawe kuliko wale waliouawa kwa upanga wa Waisraeli.
Ko so bežali izpred Izraela in so bili pri spuščanju dol k Bet Horónu, se je pripetilo, da je Gospod z neba nanje metal velike kamne do Azéke in so umrli. Bilo jih je več, ki so umrli od kamnite toče, kakor tistih, ki so jih Izraelovi otroci usmrtili z mečem.
12 Katika siku ile ambayo Bwana aliwapeana Waamori kwa Israeli, Yoshua akanena na Bwana akiwa mbele ya Waisraeli akasema: “Wewe jua, simama juu ya Gibeoni, wewe mwezi, tulia juu ya Bonde la Aiyaloni.”
Potem je Józue spregovoril Gospodu na dan, ko je pred Izraelovimi otroki Gospod izročil Amoréjce in rekel pred očmi Izraela: »Sonce, ti stoj mirno nad Gibeónom in ti luna v dolini Ajalón.«
13 Hivyo jua likasimama, nao mwezi ukatulia, hadi taifa hilo lilipokwisha kujilipizia kisasi kwa adui wake, kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Yashari. Jua likasimama kimya katikati ya mbingu, likachelewa kuzama muda wa siku moja nzima.
Sonce je stalo mirno in luna je obstala, dokler se ljudstvo ni maščevalo nad svojimi sovražniki. Mar ni to zapisano v Jasherjevi knjigi? Tako je sonce mirno stalo na sredi neba in približno cel dan ni pohitelo, da bi zašlo.
14 Haijakuwepo siku nyingine kama hiyo kabla au baada, siku ambayo Bwana alimsikiliza mwanadamu. Hakika Bwana alikuwa akiwapigania Israeli.
Pred tem niti za tem ni bilo takšnega dne, da bi Gospod prisluhnil glasu moža, kajti Gospod se je bojeval za Izrael.
15 Ndipo Yoshua akarudi kambini huko Gilgali pamoja na Israeli yote.
Józue se je vrnil in ves Izrael z njim, k taboru pri Gilgálu.
16 Basi wale wafalme watano wakawa wamekimbia kujificha kwenye pango huko Makeda.
Toda teh pet kraljev je pobegnilo in se skrilo v votlini pri Makédi.
17 Yoshua alipoambiwa kuwa wafalme hao watano wamekutwa wakiwa wamejificha ndani ya pango huko Makeda,
To je bilo povedano Józuetu, rekoč: »Pet kraljev je najdenih skritih v votlini pri Makédi.«
18 akasema, “Vingirisheni mawe makubwa kwenye mdomo wa hilo pango, tena wekeni walinzi wa kulilinda.
Józue je rekel: »Na odprtino votline zavalite velike kamne in poleg postavite može, da jih varujejo.
19 Lakini msiwaache! Wafuatieni adui zenu, washambulieni kutoka nyuma, wala msiwaache wafike kwenye miji yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewatia mkononi mwenu.”
Ne stojte, temveč sledite za svojimi sovražniki in udarite najbolj zadnje izmed njih. Ne trpite, da vstopijo v svoja mesta, kajti Gospod, vaš Bog, jih je izročil v vašo roko.«
20 Hivyo Yoshua pamoja na Waisraeli wakawaangamiza kabisa karibu wote, lakini wachache waliosalia walifika kwenye miji yao yenye maboma.
Pripetilo se je, ko so Józue in Izraelovi otroci z zelo velikim pokolom, dokler niso bili použiti, naredili konec njihovemu pobijanju, da je preostanek, ki je preostal izmed njih, vstopil v utrjena mesta.
21 Basi jeshi lote likarudi salama kwa Yoshua huko kambini Makeda, na hakuna yeyote aliyetoa neno kinyume cha Waisraeli.
In vse ljudstvo se je v miru vrnilo k taboru, k Józuetu, pri Makédi. Nihče ni svojega jezika premaknil zoper kateregakoli izmed Izraelovih otrok.
22 Ndipo Yoshua akasema, “Haya fungueni mdomo wa pango, mniletee hao wafalme watano.”
Potem je Józue rekel: »Odprite odprtino votline in teh pet kraljev privedite k meni, ven iz votline.«
23 Kwa hiyo wakawatoa hao wafalme watano nje ya pango: wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni.
Storili so tako in iz votline so k njemu privedli teh pet kraljev, kralja iz Jeruzalema, kralja iz Hebróna, kralja iz Jarmúta, kralja iz Lahíša in kralja iz Eglóna.
24 Walipokuwa wamewaleta hawa wafalme kwa Yoshua, akawaita watu wote wa Israeli, na kuwaambia majemadari wa vita waliokwenda pamoja naye, “Njooni hapa mweke nyayo zenu juu ya shingo za hawa wafalme.” Basi wakaja wakaweka nyayo zao shingoni.
Ko so te kralje privedli k Józuetu, se je pripetilo, da je Józue dal poklicati vse Izraelove može in rekel poveljnikom bojevnikov, ki so odšli z njim: »Pridite bliže, položite svoja stopala na vratove teh kraljev.« Približali so se in svoja stopala položili na njihove vratove.
25 Yoshua akawaambia, “Msiogope, wala msivunjike moyo. Kuweni hodari na wenye ushujaa. Hili ndilo Bwana atakalowatendea adui zenu wote mnaokwenda kupigana nao.”
Józue jim je rekel: »Ne bojte se niti ne bodite zaprepadeni, bodite močni in odločnega poguma, kajti tako bo Gospod storil vsem vašim sovražnikom, zoper katere se borite.«
26 Ndipo Yoshua akawapiga na kuwaua wale wafalme na kuwatundika juu ya miti mitano, nao wakaachwa wakiningʼinia juu ya ile miti hadi jioni.
Potem jih je Józue udaril, jih usmrtil in jih obesil na pet dreves; in do večera so viseli na drevesih.
27 Wakati wa kuzama jua Yoshua akaamuru, nao wakawashusha kutoka kwenye ile miti na kuwatupa kwenye lile pango ambalo walikuwa wamejificha. Kwenye mdomo wa lile pango wakaweka mawe makubwa, ambayo yapo hadi leo.
Ob času zahajanja sonca pa se je pripetilo, da je Józue zapovedal in so jih sneli iz dreves in jih vrgli v votlino, v kateri so bili skriti in na ustje votline so položili velike kamne, ki ostajajo do točno tega dne.
28 Siku ile Yoshua akateka Makeda. Akamuua kila mmoja katika ule mji, pamoja na mfalme wake kwa upanga. Hakubakiza mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Makeda kama vile alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
Ta dan je Józue zavzel Makédo in jo udaril z ostrino meča in njenega kralja je popolnoma uničil, njih in vse duše, ki so bile tam. Nikogar ni pustil ostati. Kralju v Makédi pa je storil, kakor je storil kralju v Jerihi.
29 Ndipo Yoshua akaondoka Makeda akiwa pamoja na Israeli yote mpaka mji wa Libna na kuushambulia.
Potem je Józue in ves Izrael z njim, prešel od Makéde v Libno in se boril zoper Libno.
30 Bwana pia akautia huo mji wa Libna pamoja na mfalme wake mikononi mwa Israeli. Yoshua akaangamiza ule mji na kila mtu aliyekuwa ndani yake kwa upanga. Hakubakiza huko mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Libna kama alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
Tudi njo je Gospod izročil in njenega kralja, v Izraelovo roko. Udaril jo je z ostrino meča in vse duše, ki so bile v njej. Nikogar ni pustil preostati v njej, toda njenemu kralju je storil, kakor je storil kralju Jerihe.
31 Kisha Yoshua akaondoka Libna kwenda Lakishi akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
Józue in ves Izrael z njim, je prešel od Libne do Lahíša in se utaboril zoper njega in se boril zoper njega.
32 Bwana akautia Lakishi mikononi mwa Israeli, Yoshua akauteka siku ya pili. Yoshua akauangamiza mji na kila kilichokuwa ndani yake kwa upanga, kama tu vile alivyokuwa ameufanyia mji wa Libna.
Gospod je Lahíš izročil v Izraelovo roko, ki so ga zavzeli na drugi dan in ga udaril z ostrino meča in vse duše, ki so bile tam, glede na vse, kar je storil Libni.
33 Wakati huo huo, Horamu mfalme wa Gezeri alikuwa amepanda ili kusaidia Lakishi, lakini Yoshua akamshinda pamoja na jeshi lake, hadi hapakubakia mtu yeyote.
Potem je prišel gor Horám, kralj v Gezerju, da pomaga Lahíšu, in Józue je udaril njega in njegovo ljudstvo, dokler nikogar ni pustil preostati.
34 Ndipo Yoshua akaondoka Lakishi kwenda Egloni akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
Iz Lahíša je Józue prešel do Eglóna in ves Izrael z njim in utaborili so se zoper njega in se borili zoper njega.
35 Wakauteka mji huo siku ile ile, wakaupiga kwa upanga na kumwangamiza kila mmoja aliyekuwa ndani yake, kama vile walivyokuwa wameufanyia Lakishi.
Zavzeli so ga na ta dan in ga udarili z ostrino meča in vse duše, ki so bile tam, je ta dan popolnoma uničil, glede na vse, kar je storil Lahíšu.
36 Kisha Yoshua akapanda kutoka Egloni kwenda Hebroni akiwa pamoja na Israeli yote na kuushambulia.
Józue in ves Izrael z njim, je odšel gor od Eglóna, do Hebróna in so se borili zoper njega,
37 Wakauteka mji na kuupiga kwa upanga, pamoja na mfalme wake, vijiji vyake na kila mmoja aliyekuwa ndani yake. Hawakubakiza mtu yeyote. Kama vile huko Egloni, waliuangamiza kabisa pamoja na kila mmoja aliyekuwa ndani yake.
ga zavzeli in udarili z ostrino meča in njihovega kralja in vsa njihova mesta in vse duše, ki so bile v njem. Nikogar ni pustil preostati, glede na vse, kar je storil Eglónu, temveč ga je popolnoma uničil in vse duše, ki so bile v njem.
38 Ndipo Yoshua na Israeli wote wakageuka na kuushambulia Debiri.
Józue se je vrnil in ves Izrael z njim, do Debírja in se boril zoper njega
39 Wakauteka mji, mfalme wake na vijiji vyake, na kuupiga kwa upanga. Kila mmoja aliyekuwa ndani yake wakamwangamiza kabisa. Hawakubakiza mtu yeyote. Wakaufanyia Debiri na mfalme wake kama vile walivyokuwa wameifanyia miji ya Libna na Hebroni na wafalme wao.
in ga zavzel in njegovega kralja in vsa njegova mesta. Udarili so jih z ostrino meča in popolnoma uničili vse duše, ki so bile v njem. Nikogar ni pustil preostati. Kakor je storil Hebrónu, tako je storil Debírju in njegovemu kralju, kakor je storil tudi Libni in njenemu kralju.
40 Hivyo Yoshua akalishinda eneo hilo lote, ikiwa ni pamoja na nchi ya vilima, na Negebu, na sehemu ya magharibi chini ya vilima, materemko ya milima, pamoja na wafalme wake wote. Hakubakiza mtu yeyote. Akaangamiza kabisa kila kitu chenye pumzi, kama vile Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa ameamuru.
Tako je Józue udaril vso hribovito deželo, južno [deželo], [deželo] dolin, izvirov in vse njihove kralje. Ničesar ni pustil preostati, temveč je popolnoma uničil vse, kar je dihalo, kakor je zapovedal Gospod, Izraelov Bog.
41 Yoshua akawashinda kuanzia Kadesh-Barnea hadi Gaza na kutoka eneo lote la Gosheni hadi Gibeoni.
Józue jih je udarjal od Kadeš Barnée, celo do Gaze in vso Gošensko pokrajino, celo do Gibeóna.
42 Wafalme hawa wote pamoja na nchi zao Yoshua aliwashinda kwa wakati mmoja, kwa sababu Bwana, Mungu wa Israeli, aliwapigania Israeli.
Vse te kralje in njihove dežele je Józue zavzel naenkrat, ker se je Gospod, Izraelov Bog, boril za Izrael.
43 Ndipo Yoshua akarudi pamoja na Israeli yote kwenye kambi huko Gilgali.
In Józue se je vrnil in ves Izrael z njim, v tabor h Gilgálu.