< Yoshua 10 >
1 Baada ya haya Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu alisikia kuwa Yoshua alikuwa ameteka mji wa Ai na kuuangamiza kabisa, tena alikuwa ameua mfalme wake, kama alivyofanya huko Yeriko na mfalme wake, tena ya kuwa watu wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli, na walikuwa wakiishi karibu yao.
Et lorsque Adoni-Tsédec, Roi de Jérusalem, apprit que Josué avait pris et dévoué Aï et traité Aï et son Roi, comme il avait traité Jéricho et son Roi, et que les habitants de Gabaon avaient fait leur paix avec Israël et restaient dans son sein,
2 Yeye na watu wake wakataharuki mno kwa kuwa Gibeoni ulikuwa mji mkubwa kama mmojawapo ya miji ya kifalme; ulikuwa mkubwa kuliko Ai, nao watu wake wote walikuwa mashujaa wa vita.
alors il eut une crainte extrême. Car Gabaon était une ville grande comme l'une des villes royales et plus considérable qu'Aï, et tous ses hommes étaient des guerriers.
3 Hivyo Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu akaomba msaada kwa Hohamu mfalme wa Hebroni, Piramu mfalme wa Yarmuthi, Yafia mfalme wa Lakishi, na Debiri mfalme wa Egloni.
Alors Adoni-Tsédec, Roi de Jérusalem, députa vers Hoham, Roi de Hébron, et vers Piream, Roi de Jarmuth, et vers Japhia, Roi de Lachis, et vers Débir, Roi de Eglon, pour leur dire:
4 Akawaambia, “Njooni mnisaidie kuipiga Gibeoni, kwa sababu imefanya mapatano ya amani na Yoshua na Waisraeli.”
Venez me joindre pour m'aider à réduire Gabaon, car elle a fait sa paix avec Josué et les enfants d'Israël.
5 Ndipo hao wafalme watano wa Waamori, ambao ni wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni, wakaunganisha majeshi yao. Wakapanda na vikosi vyao vyote, nao wakajipanga dhidi ya Gibeoni na kuishambulia.
Et cinq Rois des Amoréens, le Roi de Jérusalem, le Roi de Hébron, le Roi de Jarmuth, le Roi de Lachis, le Roi de Eglon opérèrent leur jonction et s'avancèrent eux et toutes leurs armées et vinrent camper devant Gabaon, et l'assiégèrent.
6 Nao Wagibeoni wakatuma ujumbe kwa Yoshua kwenye kambi ya Gilgali na kumwambia, “Usiwatelekeze watumishi wako. Panda haraka uje kwetu kutuokoa! Tusaidie, kwa sababu wafalme wote wa Waamori wakaao kwenye nchi ya vilima wameunganisha majeshi yao pamoja dhidi yetu.”
Alors les gens de Gabaon députèrent vers Josué, à son camp près de Guilgal, pour lui dire: Ne retire pas ta main à tes serviteurs, avance-toi vers nous en hâte, apporte-nous aide et secours car tous les Rois des Amoréens habitant la montagne se sont ligués contre nous.
7 Basi Yoshua akaondoka Gilgali pamoja na jeshi lake lote, wakiwepo watu wote mashujaa wa vita.
Là-dessus Josué se mit en marche de Guilgal, lui et avec lui tous les gens de guerre, et tous les braves guerriers.
8 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope watu hao, nimewatia mkononi mwako. Hakuna yeyote atakayeweza kushindana nawe.”
Et l'Éternel dit à Josué: N'aie pas peur d'eux, car je les ai livrés entre tes mains, pas un de leurs hommes ne te tiendra tête.
9 Baada ya Yoshua kutembea usiku kucha kutoka Gilgali, akawashambulia ghafula.
Et Josué fondit sur eux tout à coup. Or il employa toute la nuit à venir de Guilgal.
10 Bwana akawafadhaisha mbele ya Waisraeli, nao wakawashinda kwa ushindi mkuu huko Gibeoni. Israeli wakawafukuza kuelekea njia iendayo Beth-Horoni wakiwaua mpaka kufikia njia iendayo Azeka na Makeda.
Et l'Éternel jeta la confusion parmi eux devant Israël, et il leur fit essuyer une grande défaite près de Gabaon, et il les poursuivit sur la route de la montée de Beth-Horon, et les mena battant jusqu'à Azéca et à Makkéda.
11 Walipokuwa wakikimbia mbele ya Israeli kwenye barabara iteremkayo kutoka Beth-Horoni hadi Azeka, Bwana akawavumishia mawe makubwa ya mvua kutoka mbinguni, na wengi wao wakauawa na hayo mawe kuliko wale waliouawa kwa upanga wa Waisraeli.
Et comme ils fuyaient devant Israël, ils étaient à la descente de Beth-Horon; là l'Éternel fit tomber sur eux du ciel de grosses pierres jusqu'à Azéca; et ils périrent; il y eut un plus grand nombre de ceux que tuèrent les pierres de grêle, que de ceux que les enfants d'Israël égorgèrent avec l'épée.
12 Katika siku ile ambayo Bwana aliwapeana Waamori kwa Israeli, Yoshua akanena na Bwana akiwa mbele ya Waisraeli akasema: “Wewe jua, simama juu ya Gibeoni, wewe mwezi, tulia juu ya Bonde la Aiyaloni.”
C'est alors que Josué parla à l'Éternel, dans la journée où l'Éternel livra les Amoréens aux enfants d'Israël, et il dit en présence d'Israël: Soleil, attends à Gabaon, et toi, Lune, au val d'Ajalon.
13 Hivyo jua likasimama, nao mwezi ukatulia, hadi taifa hilo lilipokwisha kujilipizia kisasi kwa adui wake, kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Yashari. Jua likasimama kimya katikati ya mbingu, likachelewa kuzama muda wa siku moja nzima.
Et le soleil attendit et la lune resta, jusqu'à ce qu'Israël eût puni ses ennemis. N'est-ce pas ce qui est écrit dans le Livre du Droiturier? Et le soleil resta dans le milieu du ciel et ne se hâta pas vers son couchant, presque un jour entier.
14 Haijakuwepo siku nyingine kama hiyo kabla au baada, siku ambayo Bwana alimsikiliza mwanadamu. Hakika Bwana alikuwa akiwapigania Israeli.
Et avant et après il n'y eut pas une journée telle que l'Éternel écoutât la voix d'un homme, car l'Éternel combattait pour Israël.
15 Ndipo Yoshua akarudi kambini huko Gilgali pamoja na Israeli yote.
Et Josué, et tout Israël avec lui, retourna au camp à Guilgal.
16 Basi wale wafalme watano wakawa wamekimbia kujificha kwenye pango huko Makeda.
Ces cinq Rois étaient donc en fuite, et ils se cachèrent dans la caverne à Makkéda.
17 Yoshua alipoambiwa kuwa wafalme hao watano wamekutwa wakiwa wamejificha ndani ya pango huko Makeda,
Alors Josué reçut cette information: Les cinq Rois se trouvent cachés dans la caverne à Makkéda.
18 akasema, “Vingirisheni mawe makubwa kwenye mdomo wa hilo pango, tena wekeni walinzi wa kulilinda.
Et Josué dit: Roulez de grosses pierres à l'ouverture de la caverne, et postez-y des hommes pour les garder.
19 Lakini msiwaache! Wafuatieni adui zenu, washambulieni kutoka nyuma, wala msiwaache wafike kwenye miji yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewatia mkononi mwenu.”
Quant à vous, ne vous arrêtez pas, poursuivez vos ennemis, et attaquez-les en queue, ne les laissez pas regagner leurs villes; car l'Éternel, votre Dieu, les a livrés entre vos mains.
20 Hivyo Yoshua pamoja na Waisraeli wakawaangamiza kabisa karibu wote, lakini wachache waliosalia walifika kwenye miji yao yenye maboma.
Et lorsque Josué et les enfants d'Israël eurent consommé leur défaite qui fut très grande, jusqu'à extermination (des réchappés échappèrent pourtant et gagnèrent les places fortes)
21 Basi jeshi lote likarudi salama kwa Yoshua huko kambini Makeda, na hakuna yeyote aliyetoa neno kinyume cha Waisraeli.
et lorsque tout le peuple fut revenu sain et sauf au camp auprès de Josué à Makkéda sans que personne remuât la langue contre les enfants d'Israël,
22 Ndipo Yoshua akasema, “Haya fungueni mdomo wa pango, mniletee hao wafalme watano.”
alors Josué dit: Ouvrez l'entrée de la caverne et tirez de la caverne pour me les amener ces cinq Rois-là.
23 Kwa hiyo wakawatoa hao wafalme watano nje ya pango: wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni.
Et on le fit, et on lui amena ces cinq Rois-là qui furent tirés de la caverne, le Roi de Jérusalem, le Roi de Hébron, le Roi de Jarmuth, le Roi de Lachis, le Roi de Eglon.
24 Walipokuwa wamewaleta hawa wafalme kwa Yoshua, akawaita watu wote wa Israeli, na kuwaambia majemadari wa vita waliokwenda pamoja naye, “Njooni hapa mweke nyayo zenu juu ya shingo za hawa wafalme.” Basi wakaja wakaweka nyayo zao shingoni.
Et ces Rois amenés devant Josué, Josué convoqua tous les hommes d'Israël, et dit aux chefs des gens de guerre qui avaient marché avec lui: Approchez! posez vos pieds sur les cous de ces Rois. Et ils s'approchèrent et posèrent leurs pieds sur leurs cous.
25 Yoshua akawaambia, “Msiogope, wala msivunjike moyo. Kuweni hodari na wenye ushujaa. Hili ndilo Bwana atakalowatendea adui zenu wote mnaokwenda kupigana nao.”
Alors Josué leur dit: Soyez sans crainte et sans peur, ayez courage et résolution, car ainsi l'Éternel traitera tous vos ennemis que vous avez à combattre.
26 Ndipo Yoshua akawapiga na kuwaua wale wafalme na kuwatundika juu ya miti mitano, nao wakaachwa wakiningʼinia juu ya ile miti hadi jioni.
Après quoi Josué les fit égorger et tuer, puis pendre à cinq arbres; et ils restèrent pendus aux arbres jusqu'au soir.
27 Wakati wa kuzama jua Yoshua akaamuru, nao wakawashusha kutoka kwenye ile miti na kuwatupa kwenye lile pango ambalo walikuwa wamejificha. Kwenye mdomo wa lile pango wakaweka mawe makubwa, ambayo yapo hadi leo.
Et au moment du coucher du soleil, sur l'ordre de Josué, on les détacha des arbres, et on les jeta dans la caverne où ils s'étaient cachés, et l'on plaça de grosses pierres à l'ouverture de la caverne, et elles y sont aujourd'hui même.
28 Siku ile Yoshua akateka Makeda. Akamuua kila mmoja katika ule mji, pamoja na mfalme wake kwa upanga. Hakubakiza mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Makeda kama vile alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
Et dans ce même jour Josué ayant pris Makkéda la mit à sac avec le tranchant de l'épée, et il dévoua son Roi, ainsi que toutes les personnes qui s'y trouvaient, et ne laissa survivre aucun réchappé; et il traita le Roi de Makkéda comme il avait traité le Roi de Jéricho.
29 Ndipo Yoshua akaondoka Makeda akiwa pamoja na Israeli yote mpaka mji wa Libna na kuushambulia.
Alors Josué et tout Israël avec lui, de Makkéda se porta sur Libna, et il attaqua Libna.
30 Bwana pia akautia huo mji wa Libna pamoja na mfalme wake mikononi mwa Israeli. Yoshua akaangamiza ule mji na kila mtu aliyekuwa ndani yake kwa upanga. Hakubakiza huko mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Libna kama alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
Et l'Éternel la livra aussi entre les mains d'Israël, ainsi que son Roi, et la frappa avec le tranchant de l'épée, ainsi que toutes les personnes qui s'y trouvaient, et il n'y laissa survivre aucun réchappé, et il traita son Roi comme il avait traité le Roi de Jéricho.
31 Kisha Yoshua akaondoka Libna kwenda Lakishi akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
Puis Josué, et tout Israël avec lui, de Libna marcha sur Lachis devant laquelle il campa; et il l'attaqua.
32 Bwana akautia Lakishi mikononi mwa Israeli, Yoshua akauteka siku ya pili. Yoshua akauangamiza mji na kila kilichokuwa ndani yake kwa upanga, kama tu vile alivyokuwa ameufanyia mji wa Libna.
Et l'Éternel livra Lachis entre les mains d'Israël qui la prit dès le second jour et la mit à sac avec le tranchant de l'épée ainsi que toutes les personnes qui y étaient, tout comme il avait traité Libna.
33 Wakati huo huo, Horamu mfalme wa Gezeri alikuwa amepanda ili kusaidia Lakishi, lakini Yoshua akamshinda pamoja na jeshi lake, hadi hapakubakia mtu yeyote.
Alors Horam, Roi de Gézer, s'avança pour secourir Lachis, et Josué le défit lui et son peuple, à ne pas lui laisser un réchappé.
34 Ndipo Yoshua akaondoka Lakishi kwenda Egloni akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
Ensuite Josué, et tout Israël avec lui, de Lachis se porta sur Eglon devant laquelle ils campèrent et qu'ils attaquèrent.
35 Wakauteka mji huo siku ile ile, wakaupiga kwa upanga na kumwangamiza kila mmoja aliyekuwa ndani yake, kama vile walivyokuwa wameufanyia Lakishi.
Et ils la prirent le jour même, et ils sévirent sur elle avec le tranchant de l'épée, ainsi que sur toutes les personnes qui s'y trouvaient, et le jour même il la dévoua tout comme il avait traité Lachis.
36 Kisha Yoshua akapanda kutoka Egloni kwenda Hebroni akiwa pamoja na Israeli yote na kuushambulia.
Ensuite Josué, et tout Israël avec lui, de Eglon se porta sur Hébron qu'ils attaquèrent.
37 Wakauteka mji na kuupiga kwa upanga, pamoja na mfalme wake, vijiji vyake na kila mmoja aliyekuwa ndani yake. Hawakubakiza mtu yeyote. Kama vile huko Egloni, waliuangamiza kabisa pamoja na kila mmoja aliyekuwa ndani yake.
Et l'ayant prise ils sévirent avec le tranchant de l'épée sur elle, et sur son Roi, et sur toutes ses villes et sur toutes les personnes qui y étaient; il ne laissa survivre aucun réchappé ainsi qu'il avait fait à Eglon, et il la dévoua avec toutes les personnes qui y étaient.
38 Ndipo Yoshua na Israeli wote wakageuka na kuushambulia Debiri.
Alors Josué, et tout Israël avec lui, se tourna contre Debir, et il l'attaqua.
39 Wakauteka mji, mfalme wake na vijiji vyake, na kuupiga kwa upanga. Kila mmoja aliyekuwa ndani yake wakamwangamiza kabisa. Hawakubakiza mtu yeyote. Wakaufanyia Debiri na mfalme wake kama vile walivyokuwa wameifanyia miji ya Libna na Hebroni na wafalme wao.
Et il la prit ainsi que son Roi et toutes ses villes, et ils sévirent sur elles avec le tranchant de l'épée, et ils dévouèrent toutes les personnes qui y étaient sans laisser survivre un réchappé; comme il avait traité Hébron, ainsi traita-t-il Debir, et son Roi, de la même manière qu'il avait traité Libna et son Roi.
40 Hivyo Yoshua akalishinda eneo hilo lote, ikiwa ni pamoja na nchi ya vilima, na Negebu, na sehemu ya magharibi chini ya vilima, materemko ya milima, pamoja na wafalme wake wote. Hakubakiza mtu yeyote. Akaangamiza kabisa kila kitu chenye pumzi, kama vile Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa ameamuru.
Ainsi Josué réduisit tout le pays, la Montagne, le Midi, le Pays-bas et les versants, et tous leurs Rois; il ne laissa survivre aucun réchappé, et il dévoua tout ce qui respirait, selon l'ordre de l'Éternel, Dieu d'Israël.
41 Yoshua akawashinda kuanzia Kadesh-Barnea hadi Gaza na kutoka eneo lote la Gosheni hadi Gibeoni.
Et Josué les réduisit de Cadès-Barnéa à Gaza, et tout le district de Gosen jusques à Gabaon.
42 Wafalme hawa wote pamoja na nchi zao Yoshua aliwashinda kwa wakati mmoja, kwa sababu Bwana, Mungu wa Israeli, aliwapigania Israeli.
Et dans une seule campagne Josué prit tous ces rois et leur pays, car l'Éternel, Dieu d'Israël, combattait pour Israël.
43 Ndipo Yoshua akarudi pamoja na Israeli yote kwenye kambi huko Gilgali.
Alors Josué et tout Israël avec lui, revint au camp à Guilgal.