< Yoshua 10 >

1 Baada ya haya Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu alisikia kuwa Yoshua alikuwa ameteka mji wa Ai na kuuangamiza kabisa, tena alikuwa ameua mfalme wake, kama alivyofanya huko Yeriko na mfalme wake, tena ya kuwa watu wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli, na walikuwa wakiishi karibu yao.
And whanne Adonysedech, kyng of Jerusalem, hadde herde these thingis, that is, that Josue hadde take Hai, and hadde destried it; for as Josue hadde do to Jerico and to the kyng therof, so he dide to Hay, and to the kyng therof; and that Gabaonytis hadden fled to Israel, and weren boundun in pees with hem,
2 Yeye na watu wake wakataharuki mno kwa kuwa Gibeoni ulikuwa mji mkubwa kama mmojawapo ya miji ya kifalme; ulikuwa mkubwa kuliko Ai, nao watu wake wote walikuwa mashujaa wa vita.
Adonysedech dredde greetli; for Gabaon was a greet citee, and oon of the kyngis citees, and grettere than the citee of Hai, and alle the fiyteris therof weren most stronge.
3 Hivyo Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu akaomba msaada kwa Hohamu mfalme wa Hebroni, Piramu mfalme wa Yarmuthi, Yafia mfalme wa Lakishi, na Debiri mfalme wa Egloni.
Therfor Adonysedech, kyng of Jerusalem, sente to Ocham, kyng of Ebron, and to Pharam, kyng of Herymoth, and to Japhie, kyng of Lachis, and to Dabir, kyng of Eglon, and seide,
4 Akawaambia, “Njooni mnisaidie kuipiga Gibeoni, kwa sababu imefanya mapatano ya amani na Yoshua na Waisraeli.”
Stie ye to me, and helpe ye, that we fiyte ayens Gabaon, for it was yoldun to Josue, and to the sones of Israel.
5 Ndipo hao wafalme watano wa Waamori, ambao ni wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni, wakaunganisha majeshi yao. Wakapanda na vikosi vyao vyote, nao wakajipanga dhidi ya Gibeoni na kuishambulia.
Therfor fyue kyngis of Ammorreis, the kyng of Jerusalem, the kyng of Ebron, the kyng of Herymoth, the kyng of Lachis, the kyng of Eglon, weren gaderid, and stieden togidere with her oostis; and settiden tentis ayens Gabaon, and fouyten ayens it.
6 Nao Wagibeoni wakatuma ujumbe kwa Yoshua kwenye kambi ya Gilgali na kumwambia, “Usiwatelekeze watumishi wako. Panda haraka uje kwetu kutuokoa! Tusaidie, kwa sababu wafalme wote wa Waamori wakaao kwenye nchi ya vilima wameunganisha majeshi yao pamoja dhidi yetu.”
Sotheli the dwelleris of the citee of Gabaon, `that weren bisegid, senten to Josue, that dwellide than in tentis at Galgala, and seide to hym, Withdrawe not thin hondis fro the help of thi seruauntis; `stie thou soone, and delyuere vs, and helpe thou; for alle the kyngis of Amorreis, that dwelliden in the hilli places, camen togidere ayens vs.
7 Basi Yoshua akaondoka Gilgali pamoja na jeshi lake lote, wakiwepo watu wote mashujaa wa vita.
And Josue stiede fro Galgala, and al the oost of fiyters, `the strengeste men, `with hym.
8 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope watu hao, nimewatia mkononi mwako. Hakuna yeyote atakayeweza kushindana nawe.”
And the Lord seide to Josue, Drede thou not hem, for Y yaf hem in to thin hondis; noon of hem schal mow ayenstonde thee.
9 Baada ya Yoshua kutembea usiku kucha kutoka Gilgali, akawashambulia ghafula.
Therfor Josue felde sodenli on hem, and stiede in al the nyyt fro Galgala;
10 Bwana akawafadhaisha mbele ya Waisraeli, nao wakawashinda kwa ushindi mkuu huko Gibeoni. Israeli wakawafukuza kuelekea njia iendayo Beth-Horoni wakiwaua mpaka kufikia njia iendayo Azeka na Makeda.
and the Lord `disturblide hem fro the face of Israel, and al to-brak with greet veniaunce in Gabaon. And Josue pursuede hem bi the weie of the stiyng of Betheron, and smoot `til to Azecha and Maceda.
11 Walipokuwa wakikimbia mbele ya Israeli kwenye barabara iteremkayo kutoka Beth-Horoni hadi Azeka, Bwana akawavumishia mawe makubwa ya mvua kutoka mbinguni, na wengi wao wakauawa na hayo mawe kuliko wale waliouawa kwa upanga wa Waisraeli.
And whanne thei fledden the sones of Israel, and weren in the goyng doun of Betheron, the Lord sente grete stoonus on hem fro heuene, til to Azecha; and many mo weren deed bi the `stoonys of hail, than thei whiche the sones of Israel `smytiden bi swerd.
12 Katika siku ile ambayo Bwana aliwapeana Waamori kwa Israeli, Yoshua akanena na Bwana akiwa mbele ya Waisraeli akasema: “Wewe jua, simama juu ya Gibeoni, wewe mwezi, tulia juu ya Bonde la Aiyaloni.”
Thanne Josue spak to the Lord, in the dai in which he bitook Amorrey in the siyt of the sones of Israel; and Josue seide bifore hem, Sunne, be thou not mouyd ayens Gabaon, and the moone ayens the valei of Hailon.
13 Hivyo jua likasimama, nao mwezi ukatulia, hadi taifa hilo lilipokwisha kujilipizia kisasi kwa adui wake, kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Yashari. Jua likasimama kimya katikati ya mbingu, likachelewa kuzama muda wa siku moja nzima.
And the sunne and the moone stoden, til the folc of God vengide it silf of hise enemyes. Whether this is not writun in the book of iust men? And so the sunne stood in the myddis of heuene, and hastide not to go doun in the space of o dai; so long a dai was not bifore and aftirward;
14 Haijakuwepo siku nyingine kama hiyo kabla au baada, siku ambayo Bwana alimsikiliza mwanadamu. Hakika Bwana alikuwa akiwapigania Israeli.
for the Lord obeiede to the vois of man, and fauyt for Israel.
15 Ndipo Yoshua akarudi kambini huko Gilgali pamoja na Israeli yote.
And Josue turnede ayen, with al Israel, in to the tentis of Galgala.
16 Basi wale wafalme watano wakawa wamekimbia kujificha kwenye pango huko Makeda.
Forsothe fyue kyngis fledden, and hidden hem silf in the denne of the citee of Maceda.
17 Yoshua alipoambiwa kuwa wafalme hao watano wamekutwa wakiwa wamejificha ndani ya pango huko Makeda,
And it was teld to Josue, that fyue kyngis weren foundun hid in the denne of the citee of Maceda.
18 akasema, “Vingirisheni mawe makubwa kwenye mdomo wa hilo pango, tena wekeni walinzi wa kulilinda.
Which Josue comaundide to felowis, and seide, Walewe ye grete stoonus to the `mouth of the denne, and putte ye witti men, that schulen kepe the closid kyngis; sotheli nyle ye stonde,
19 Lakini msiwaache! Wafuatieni adui zenu, washambulieni kutoka nyuma, wala msiwaache wafike kwenye miji yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewatia mkononi mwenu.”
but pursue ye the enemyes, and slee ye alle the laste of fleeris; and suffre ye not hem entre in to the strengthis of her citees, whiche enemyes youre Lord God bitook in to youre hondis.
20 Hivyo Yoshua pamoja na Waisraeli wakawaangamiza kabisa karibu wote, lakini wachache waliosalia walifika kwenye miji yao yenye maboma.
Therfor whanne the aduersaries weren betun with greet veniaunce, and weren almost wastid `til to deeth, thei that myyten fle Israel, entriden in to the strengthid citees.
21 Basi jeshi lote likarudi salama kwa Yoshua huko kambini Makeda, na hakuna yeyote aliyetoa neno kinyume cha Waisraeli.
And al the oost turnede ayen hoole, and in hoole noumbre to Josue, in to Maceda, where the tentis weren thanne; and no man was hardi to grutche, `ether to make priuy noise, ayens the sones of Israel.
22 Ndipo Yoshua akasema, “Haya fungueni mdomo wa pango, mniletee hao wafalme watano.”
And Josue comaundide, and seide, Opene ye the `mouth of the denne, and brynge forth to me the fyue kyngis that ben hid therynne.
23 Kwa hiyo wakawatoa hao wafalme watano nje ya pango: wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni.
And the mynystris diden, as it was comaundid to hem; and thei brouyten forth to Josue fyue kyngis fro the denne; the kyng of Jerusalem, the kyng of Ebron, the kyng of Herymoth, the kyng of Lachis, the kyng of Eglon.
24 Walipokuwa wamewaleta hawa wafalme kwa Yoshua, akawaita watu wote wa Israeli, na kuwaambia majemadari wa vita waliokwenda pamoja naye, “Njooni hapa mweke nyayo zenu juu ya shingo za hawa wafalme.” Basi wakaja wakaweka nyayo zao shingoni.
And whanne thei weren led out to Josue, he clepide alle the men of Israel, and seide to the princes of the oost, that weren with hym, Go ye, and sette youre feet on the neckis of these kyngis. And whanne thei hadden go, and trediden the neckis of `the kyngis suget `to her feet,
25 Yoshua akawaambia, “Msiogope, wala msivunjike moyo. Kuweni hodari na wenye ushujaa. Hili ndilo Bwana atakalowatendea adui zenu wote mnaokwenda kupigana nao.”
eft Josue seide to hem, Nyle ye drede, nethir `drede ye with ynne, be ye coumfortid, and be ye stronge; for the Lord schal do so to alle youre enemyes, ayens whiche ye schulen fiyte.
26 Ndipo Yoshua akawapiga na kuwaua wale wafalme na kuwatundika juu ya miti mitano, nao wakaachwa wakiningʼinia juu ya ile miti hadi jioni.
And Josue smoot, and killide hem, and hangide on fyue trees; and thei weren hangid `til to euentid.
27 Wakati wa kuzama jua Yoshua akaamuru, nao wakawashusha kutoka kwenye ile miti na kuwatupa kwenye lile pango ambalo walikuwa wamejificha. Kwenye mdomo wa lile pango wakaweka mawe makubwa, ambayo yapo hadi leo.
And whanne the sunne yede doun, he comaundide to felowis, that thei schulden put hem doun fro the iebatis; and whanne thei weren put doun, thei `castiden forth hem in to the denne, in which thei weren hid; and thei puttiden grete stoonus on the mouth therof, whiche stoonus dwellen `til to present tyme.
28 Siku ile Yoshua akateka Makeda. Akamuua kila mmoja katika ule mji, pamoja na mfalme wake kwa upanga. Hakubakiza mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Makeda kama vile alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
In the same dai Josue took also Maceda, and smoot bi the scharpnesse of swerd, and killide the kyng therof, and alle the dwelleris therof; he lefte not therynne, nameli, litle relikis; and he dide to the kyng of Maceda as he hadde do to the kyng of Jerico.
29 Ndipo Yoshua akaondoka Makeda akiwa pamoja na Israeli yote mpaka mji wa Libna na kuushambulia.
Forsothe Josue passide with al Israel fro Maceda in to Lempna, and fauyt ayens it,
30 Bwana pia akautia huo mji wa Libna pamoja na mfalme wake mikononi mwa Israeli. Yoshua akaangamiza ule mji na kila mtu aliyekuwa ndani yake kwa upanga. Hakubakiza huko mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Libna kama alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
which the Lord bitook, with the kyng therof, in the hond of Israel; and thei smytiden the citee bi the scharpnesse of swerd, and alle the dwelleris therof, and leften not ony relikis therynne; and thei diden to the kyng of Lempna as thei hadden do to the kyng of Jerico.
31 Kisha Yoshua akaondoka Libna kwenda Lakishi akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
Fro Lempna he passide with al Israel in to Lachis; and whanne the oost was disposid bi cumpas, he fauyt ayens it.
32 Bwana akautia Lakishi mikononi mwa Israeli, Yoshua akauteka siku ya pili. Yoshua akauangamiza mji na kila kilichokuwa ndani yake kwa upanga, kama tu vile alivyokuwa ameufanyia mji wa Libna.
And the Lord bitook Lachis in the hond of the sones of Israel; and he took it in the tothir dai, and smoot bi the scharpnesse of swerd, and ech man, that was therynne, as he hadde do to Lempna.
33 Wakati huo huo, Horamu mfalme wa Gezeri alikuwa amepanda ili kusaidia Lakishi, lakini Yoshua akamshinda pamoja na jeshi lake, hadi hapakubakia mtu yeyote.
In that time Yram, kyng of Gazar, stiede to helpe Lachis; whom Josue smoot, with al his puple, til to deeth.
34 Ndipo Yoshua akaondoka Lakishi kwenda Egloni akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
And he passide fro Lachis in to Eglon,
35 Wakauteka mji huo siku ile ile, wakaupiga kwa upanga na kumwangamiza kila mmoja aliyekuwa ndani yake, kama vile walivyokuwa wameufanyia Lakishi.
and cumpasside, and ouercam it in the same dai; and he smoot bi the scharpnesse of swerd alle men that weren therynne, bi alle thingis whiche he hadde do to Lachis.
36 Kisha Yoshua akapanda kutoka Egloni kwenda Hebroni akiwa pamoja na Israeli yote na kuushambulia.
Also he stiede with al Israel fro Eglon in to Ebron, and fauyt ayens it,
37 Wakauteka mji na kuupiga kwa upanga, pamoja na mfalme wake, vijiji vyake na kila mmoja aliyekuwa ndani yake. Hawakubakiza mtu yeyote. Kama vile huko Egloni, waliuangamiza kabisa pamoja na kila mmoja aliyekuwa ndani yake.
and took, and smoot bi the scharpnesse of swerd; and the kyng therof, and alle citees of that cuntrey, and alle men that dwelliden therynne; he lefte not ony relikis therynne; as he hadde do to Eglon so he dide also to Ebron, and wastide bi swerd alle thingis that weren therynne.
38 Ndipo Yoshua na Israeli wote wakageuka na kuushambulia Debiri.
Fro thennus he turnyde in to Dabir, and took it, and wastide;
39 Wakauteka mji, mfalme wake na vijiji vyake, na kuupiga kwa upanga. Kila mmoja aliyekuwa ndani yake wakamwangamiza kabisa. Hawakubakiza mtu yeyote. Wakaufanyia Debiri na mfalme wake kama vile walivyokuwa wameifanyia miji ya Libna na Hebroni na wafalme wao.
and he smoot bi the scharpnesse of swerd the kyng therof, and alle tounnes `bi cumpas; he lefte not ony relikis therynne; as he hadde do to Ebron, and to Lempna, and to `the kyngis of tho, so he dide to Dabir, and to the kyng therof.
40 Hivyo Yoshua akalishinda eneo hilo lote, ikiwa ni pamoja na nchi ya vilima, na Negebu, na sehemu ya magharibi chini ya vilima, materemko ya milima, pamoja na wafalme wake wote. Hakubakiza mtu yeyote. Akaangamiza kabisa kila kitu chenye pumzi, kama vile Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa ameamuru.
And so Josue smoot al the `lond of the hillis, and of the south, and `of the feeld, and Asedoch with her kyngis; he lefte not therynne ony relikis, but he killide al thing that myyte brethe, as the Lord God of Israel comaundide to hym;
41 Yoshua akawashinda kuanzia Kadesh-Barnea hadi Gaza na kutoka eneo lote la Gosheni hadi Gibeoni.
fro Cades Barne `til to Gazan, and al the lond of Jesson, `til to Gabaon Josue took,
42 Wafalme hawa wote pamoja na nchi zao Yoshua aliwashinda kwa wakati mmoja, kwa sababu Bwana, Mungu wa Israeli, aliwapigania Israeli.
and wastide with o fersnesse alle the kyngis, and `cuntreis of hem; for the Lord God of Israel fauyt for hym.
43 Ndipo Yoshua akarudi pamoja na Israeli yote kwenye kambi huko Gilgali.
And he turnede ayen with al Israel to the place of tentis in Galgala.

< Yoshua 10 >