< Yoshua 10 >
1 Baada ya haya Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu alisikia kuwa Yoshua alikuwa ameteka mji wa Ai na kuuangamiza kabisa, tena alikuwa ameua mfalme wake, kama alivyofanya huko Yeriko na mfalme wake, tena ya kuwa watu wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli, na walikuwa wakiishi karibu yao.
And it was when heard Adoni-Zedek [the] king of Jerusalem that he had captured Joshua Ai and he had totally destroyed it just as he had done to Jericho and to king its so he had done to Ai and to king its and that they had made peace [the] inhabitants of Gibeon with Israel and they were in midst their.
2 Yeye na watu wake wakataharuki mno kwa kuwa Gibeoni ulikuwa mji mkubwa kama mmojawapo ya miji ya kifalme; ulikuwa mkubwa kuliko Ai, nao watu wake wote walikuwa mashujaa wa vita.
And they were afraid very for [was] a city great Gibeon like one of [the] cities of royalty and for it [was] great more than Ai and all men its [were] warriors.
3 Hivyo Adoni-Sedeki mfalme wa Yerusalemu akaomba msaada kwa Hohamu mfalme wa Hebroni, Piramu mfalme wa Yarmuthi, Yafia mfalme wa Lakishi, na Debiri mfalme wa Egloni.
And he sent Adoni-Zedek [the] king of Jerusalem to Hoham [the] king of Hebron and to Piram [the] king of Jarmuth and to Japhia [the] king of Lachish and to Debir [the] king of Eglon saying.
4 Akawaambia, “Njooni mnisaidie kuipiga Gibeoni, kwa sababu imefanya mapatano ya amani na Yoshua na Waisraeli.”
Come up to me and help me so we may attack Gibeon for it has made peace with Joshua and with [the] people of Israel.
5 Ndipo hao wafalme watano wa Waamori, ambao ni wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni, wakaunganisha majeshi yao. Wakapanda na vikosi vyao vyote, nao wakajipanga dhidi ya Gibeoni na kuishambulia.
And they gathered and they went up [the] five - [the] kings of the Amorite[s] [the] king of Jerusalem [the] king of Hebron [the] king of Jarmuth [the] king of Lachish [the] king of Eglon they and all armies their and they encamped on Gibeon and they waged war on it.
6 Nao Wagibeoni wakatuma ujumbe kwa Yoshua kwenye kambi ya Gilgali na kumwambia, “Usiwatelekeze watumishi wako. Panda haraka uje kwetu kutuokoa! Tusaidie, kwa sababu wafalme wote wa Waamori wakaao kwenye nchi ya vilima wameunganisha majeshi yao pamoja dhidi yetu.”
And they sent [the] men of Gibeon to Joshua to the camp Gilgal towards saying may not you let drop hands your from servants your come up to us quickly and save! us and help us for they have gathered together against us all [the] kings of the Amorite[s] [the] inhabitants of the hill country.
7 Basi Yoshua akaondoka Gilgali pamoja na jeshi lake lote, wakiwepo watu wote mashujaa wa vita.
And he went up Joshua from Gilgal he and all [the] people of war with him and all [the] mighty [men] of strength.
8 Bwana akamwambia Yoshua, “Usiwaogope watu hao, nimewatia mkononi mwako. Hakuna yeyote atakayeweza kushindana nawe.”
And he said Yahweh to Joshua may not you be afraid from them for in hand your I have given them not he will make a stand anyone from them in face your.
9 Baada ya Yoshua kutembea usiku kucha kutoka Gilgali, akawashambulia ghafula.
And he came to them Joshua suddenly all the night he had gone up from Gilgal.
10 Bwana akawafadhaisha mbele ya Waisraeli, nao wakawashinda kwa ushindi mkuu huko Gibeoni. Israeli wakawafukuza kuelekea njia iendayo Beth-Horoni wakiwaua mpaka kufikia njia iendayo Azeka na Makeda.
And he routed them Yahweh before Israel and he struck down them a defeat great at Gibeon and he pursued them [the] direction of [the] ascent of Beth Horon and he struck down them to Azekah and to Makkedah.
11 Walipokuwa wakikimbia mbele ya Israeli kwenye barabara iteremkayo kutoka Beth-Horoni hadi Azeka, Bwana akawavumishia mawe makubwa ya mvua kutoka mbinguni, na wengi wao wakauawa na hayo mawe kuliko wale waliouawa kwa upanga wa Waisraeli.
And it was when fled they - from before Israel they [were] at [the] descent of Beth Horon and Yahweh he threw on them stones large from the heavens to Azekah and they died [were] many [those] who they died by [the] stones of the hail more than [those] whom they killed [the] people of Israel with the sword.
12 Katika siku ile ambayo Bwana aliwapeana Waamori kwa Israeli, Yoshua akanena na Bwana akiwa mbele ya Waisraeli akasema: “Wewe jua, simama juu ya Gibeoni, wewe mwezi, tulia juu ya Bonde la Aiyaloni.”
Then he spoke Joshua to Yahweh on [the] day delivered up Yahweh the Amorite[s] before [the] people of Israel and he said - to [the] eyes of Israel O sun at Gibeon be still and O moon in [the] valley Aijalon.
13 Hivyo jua likasimama, nao mwezi ukatulia, hadi taifa hilo lilipokwisha kujilipizia kisasi kwa adui wake, kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Yashari. Jua likasimama kimya katikati ya mbingu, likachelewa kuzama muda wa siku moja nzima.
And it was still the sun and [the] moon it stood still until it avenged itself on [the] nation enemies its ¿ not [is] it written on [the] scroll of Jashar and it stood still the sun in [the] middle of the heavens and not it hastened to go about a day complete.
14 Haijakuwepo siku nyingine kama hiyo kabla au baada, siku ambayo Bwana alimsikiliza mwanadamu. Hakika Bwana alikuwa akiwapigania Israeli.
And not it has been like the day that before it and after it to listen Yahweh to [the] voice of a man for Yahweh [was] fighting for Israel.
15 Ndipo Yoshua akarudi kambini huko Gilgali pamoja na Israeli yote.
And he returned Joshua and all Israel with him to the camp Gilgal towards.
16 Basi wale wafalme watano wakawa wamekimbia kujificha kwenye pango huko Makeda.
And they fled [the] five the kings these and they hid themselves in the cave at Makkedah.
17 Yoshua alipoambiwa kuwa wafalme hao watano wamekutwa wakiwa wamejificha ndani ya pango huko Makeda,
And it was told to Joshua saying they have been found [the] five the kings hidden in the cave at Makkedah.
18 akasema, “Vingirisheni mawe makubwa kwenye mdomo wa hilo pango, tena wekeni walinzi wa kulilinda.
And he said Joshua roll stones large into [the] mouth of the cave and appoint over it men to guard them.
19 Lakini msiwaache! Wafuatieni adui zenu, washambulieni kutoka nyuma, wala msiwaache wafike kwenye miji yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewatia mkononi mwenu.”
And you may not you delay pursue after enemies your and you will attack in [the] rear them may not you permit them to go into cities their for he has given them Yahweh God your in hand your.
20 Hivyo Yoshua pamoja na Waisraeli wakawaangamiza kabisa karibu wote, lakini wachache waliosalia walifika kwenye miji yao yenye maboma.
And it was when finished Joshua and [the] people of Israel to strike down them a defeat great very until were finished they and the survivors they survived of them and they went into [the] cities of fortification.
21 Basi jeshi lote likarudi salama kwa Yoshua huko kambini Makeda, na hakuna yeyote aliyetoa neno kinyume cha Waisraeli.
And they returned all the people to the camp to Joshua Makkedah in peace not he sharpened to [the] people of Israel to anyone tongue his.
22 Ndipo Yoshua akasema, “Haya fungueni mdomo wa pango, mniletee hao wafalme watano.”
And he said Joshua open [the] mouth of the cave and bring out to me [the] five the kings these from the cave.
23 Kwa hiyo wakawatoa hao wafalme watano nje ya pango: wafalme wa Yerusalemu, Hebroni, Yarmuthi, Lakishi na Egloni.
And they did thus and they brought out to him [the] five the kings these from the cave - [the] king of Jerusalem [the] king of Hebron [the] king of Jarmuth [the] king of Lachish [the] king of Eglon.
24 Walipokuwa wamewaleta hawa wafalme kwa Yoshua, akawaita watu wote wa Israeli, na kuwaambia majemadari wa vita waliokwenda pamoja naye, “Njooni hapa mweke nyayo zenu juu ya shingo za hawa wafalme.” Basi wakaja wakaweka nyayo zao shingoni.
And it was when brought out they the kings these to Joshua and he summoned Joshua every man of Israel and he said to [the] commanders of [the] men of war who had gone with him draw near put feet your on [the] necks of the kings these and they drew near and they put feet their on necks their.
25 Yoshua akawaambia, “Msiogope, wala msivunjike moyo. Kuweni hodari na wenye ushujaa. Hili ndilo Bwana atakalowatendea adui zenu wote mnaokwenda kupigana nao.”
And he said to them Joshua may not you be afraid and may not you be dismayed be strong and be bold for thus he will do Yahweh to all enemies your whom you [are] fighting them.
26 Ndipo Yoshua akawapiga na kuwaua wale wafalme na kuwatundika juu ya miti mitano, nao wakaachwa wakiningʼinia juu ya ile miti hadi jioni.
And he struck them Joshua after thus and he killed them and he hanged them on five trees and they were hanged on the trees until the evening.
27 Wakati wa kuzama jua Yoshua akaamuru, nao wakawashusha kutoka kwenye ile miti na kuwatupa kwenye lile pango ambalo walikuwa wamejificha. Kwenye mdomo wa lile pango wakaweka mawe makubwa, ambayo yapo hadi leo.
And it was to [the] time of - [the] going of the sun he commanded Joshua and people took down them from on the trees and they threw them into the cave where they had hidden themselves there and they put stones large over [the] mouth of the cave until [the] substance of the day this.
28 Siku ile Yoshua akateka Makeda. Akamuua kila mmoja katika ule mji, pamoja na mfalme wake kwa upanga. Hakubakiza mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Makeda kama vile alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
And Makkedah he captured Joshua on the day that and he struck it to [the] mouth of [the] sword and king its he totally destroyed them and every person who [was] in it not he left a survivor and he did to [the] king of Makkedah just as he had done to [the] king of Jericho.
29 Ndipo Yoshua akaondoka Makeda akiwa pamoja na Israeli yote mpaka mji wa Libna na kuushambulia.
And he passed on Joshua and all Israel with him from Makkedah Libnah and he engaged in battle with Libnah.
30 Bwana pia akautia huo mji wa Libna pamoja na mfalme wake mikononi mwa Israeli. Yoshua akaangamiza ule mji na kila mtu aliyekuwa ndani yake kwa upanga. Hakubakiza huko mtu yeyote. Akamfanyia mfalme wa Libna kama alivyokuwa amemfanyia mfalme wa Yeriko.
And he gave Yahweh also it in [the] hand of Israel and king its and he struck it to [the] mouth of [the] sword and every person who [was] in it not he left in it a survivor and he did to king its just as he had done to [the] king of Jericho.
31 Kisha Yoshua akaondoka Libna kwenda Lakishi akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
And he passed on Joshua and all Israel with him from Libnah Lachish towards and he encamped on it and he engaged in battle against it.
32 Bwana akautia Lakishi mikononi mwa Israeli, Yoshua akauteka siku ya pili. Yoshua akauangamiza mji na kila kilichokuwa ndani yake kwa upanga, kama tu vile alivyokuwa ameufanyia mji wa Libna.
And he gave Yahweh Lachish in [the] hand of Israel and he captured it on the day second and he struck it to [the] mouth of [the] sword and every person who [was] in it according to all that he had done to Libnah.
33 Wakati huo huo, Horamu mfalme wa Gezeri alikuwa amepanda ili kusaidia Lakishi, lakini Yoshua akamshinda pamoja na jeshi lake, hadi hapakubakia mtu yeyote.
Then he came up Horam [the] king of Gezer to help Lachish and he attacked him Joshua and people his until not he had left to him a survivor.
34 Ndipo Yoshua akaondoka Lakishi kwenda Egloni akiwa pamoja na Israeli yote; wakajipanga dhidi yake na kuushambulia.
And he passed on Joshua and all Israel with him from Lachish Eglon towards and they encamped on it and they engaged in battle on it.
35 Wakauteka mji huo siku ile ile, wakaupiga kwa upanga na kumwangamiza kila mmoja aliyekuwa ndani yake, kama vile walivyokuwa wameufanyia Lakishi.
And they captured it on the day that and they struck it to [the] mouth of [the] sword and every person who [was] in it on the day that he totally destroyed according to all that he had done to Lachish.
36 Kisha Yoshua akapanda kutoka Egloni kwenda Hebroni akiwa pamoja na Israeli yote na kuushambulia.
And he went up Joshua and all Israel with him from Eglon Hebron towards and they engaged in battle on it.
37 Wakauteka mji na kuupiga kwa upanga, pamoja na mfalme wake, vijiji vyake na kila mmoja aliyekuwa ndani yake. Hawakubakiza mtu yeyote. Kama vile huko Egloni, waliuangamiza kabisa pamoja na kila mmoja aliyekuwa ndani yake.
And they captured it and they struck it to [the] mouth of [the] sword and king its and all cities its and every person who [was] in it not he left a survivor according to all that he had done to Eglon and he totally destroyed it and every person who [was] in it.
38 Ndipo Yoshua na Israeli wote wakageuka na kuushambulia Debiri.
And he turned back Joshua and all Israel with him Debir towards and he engaged in battle on it.
39 Wakauteka mji, mfalme wake na vijiji vyake, na kuupiga kwa upanga. Kila mmoja aliyekuwa ndani yake wakamwangamiza kabisa. Hawakubakiza mtu yeyote. Wakaufanyia Debiri na mfalme wake kama vile walivyokuwa wameifanyia miji ya Libna na Hebroni na wafalme wao.
And he captured it and king its and all cities its and they struck them to [the] mouth of [the] sword and they totally destroyed every person who [was] in it not he left a survivor just as he had done to Hebron so he did to Debir and to king its and just as he had done to Libnah and to king its.
40 Hivyo Yoshua akalishinda eneo hilo lote, ikiwa ni pamoja na nchi ya vilima, na Negebu, na sehemu ya magharibi chini ya vilima, materemko ya milima, pamoja na wafalme wake wote. Hakubakiza mtu yeyote. Akaangamiza kabisa kila kitu chenye pumzi, kama vile Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa ameamuru.
And he defeated Joshua all the land the hill country and the Negev and the Shephelah and the slopes and all kings their not he left a survivor and every breathing thing he totally destroyed just as he had commanded Yahweh [the] God of Israel.
41 Yoshua akawashinda kuanzia Kadesh-Barnea hadi Gaza na kutoka eneo lote la Gosheni hadi Gibeoni.
And he struck down them Joshua from Kadesh Barnea and to Gaza and all [the] land of Goshen and to Gibeon.
42 Wafalme hawa wote pamoja na nchi zao Yoshua aliwashinda kwa wakati mmoja, kwa sababu Bwana, Mungu wa Israeli, aliwapigania Israeli.
And all the kings these and land their he captured Joshua time one for Yahweh [the] God of Israel [was] fighting for Israel.
43 Ndipo Yoshua akarudi pamoja na Israeli yote kwenye kambi huko Gilgali.
And he returned Joshua and all Israel with him to the camp Gilgal towards.