< Yona 4 >

1 Lakini Yona alichukizwa sana akakasirika.
But it displeased Jonah exceedingly, and he was very angry.
2 Akamwomba Bwana, “Ee Bwana, hili si lile nililolisema nilipokuwa ningali nyumbani? Hii ndiyo sababu niliharikisha kukimbilia Tarshishi. Nikifahamu kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na huruma, si mwepesi wa hasira na umejaa upendo, ni Mungu ambaye hughairi katika kupeleka maafa.
And he prayed to the LORD, and said, I pray thee, O LORD [was] not this my saying, when I was yet in my country? Therefore I fled before to Tarshish: for I knew that thou [art] a gracious God, and merciful, slow to anger, and of great kindness, and repentest of the evil.
3 Sasa, Ee Bwana, niondolee uhai wangu, kwa kuwa ni afadhali mimi nife kuliko kuishi.”
Therefore now, O LORD, take, I beseech thee, my life from me; for [it is] better for me to die than to live.
4 Lakini Bwana akamjibu, “Je unayo haki yoyote kukasirika?”
Then said the LORD, Doest thou well to be angry?
5 Yona akatoka nje akaketi mahali upande wa mashariki wa mji. Hapo akajitengenezea kibanda, akaketi kwenye kivuli chake na kungojea ni nini kitakachotokea katika mji.
So Jonah went out of the city, and sat on the east side of the city, and there made him a booth, and sat under it in the shade, till he might see what would become of the city.
6 Ndipo Bwana, Mungu akaweka tayari mzabibu na kuufanya uote, kumpa Yona kivuli kilichomfunika kichwa ili kuondoa taabu yake, naye Yona akafurahi sana kwa ajili ya ule mzabibu.
And the LORD God prepared a gourd, and made [it] to come up over Jonah, that it might be a shade over his head, to deliver him from his grief. So Jonah was exceeding glad of the gourd.
7 Lakini kesho yake asubuhi na mapema Mungu akaamuru buu, autafune mzabibu huo nao ukanyauka.
But God prepared a worm when the morning rose the next day, and it smote the gourd that it withered.
8 Wakati jua lilipochomoza, Mungu akautuma upepo wa hari wa mashariki, nalo jua likawaka juu ya kichwa cha Yona mpaka akazimia. Akatamani kufa, naye akasema, “Ni afadhali mimi nife kuliko kuishi.”
And it came to pass, when the sun rose that God prepared a vehement east wind; and the sun beat upon the head of Jonah, that he fainted, and wished in himself to die, and said, [It is] better for me to die than to live.
9 Lakini Mungu alimwambia Yona, “Je, unayo haki kukasirika kuhusu mzabibu huo?” Akasema, “Ndiyo, ninayo haki. Nimekasirika kiasi cha kufa.”
And God said to Jonah, Doest thou well to be angry for the gourd? And he said, I do well to be angry, [even] to death.
10 Lakini Bwana akamwambia, “Wewe unakasirika kwa ajili ya mzabibu huu, nawe hukuusababisha kuota wala kuutunza. Uliota usiku mmoja, nao ukafa usiku mmoja.
Then said the LORD, Thou hast had pity on the gourd, for which thou hast not labored, neither made it grow; which came up in a night, and perished in a night:
11 Lakini Ninawi ina zaidi ya watu 120,000 ambao hawawezi kupambanua kulia au kushoto, pamoja na ngʼombe wengi. Je, hainipasi kufikiri juu ya mji ule mkubwa?”
And should not I spare Nineveh, that great city, in which are more than a hundred and twenty thousand persons that cannot discern between their right hand and their left hand, and [also] many cattle?

< Yona 4 >