< Yona 4 >
1 Lakini Yona alichukizwa sana akakasirika.
And it was displeasing to Jonah displeasure great and it burned to him.
2 Akamwomba Bwana, “Ee Bwana, hili si lile nililolisema nilipokuwa ningali nyumbani? Hii ndiyo sababu niliharikisha kukimbilia Tarshishi. Nikifahamu kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na huruma, si mwepesi wa hasira na umejaa upendo, ni Mungu ambaye hughairi katika kupeleka maafa.
And he prayed to Yahweh and he said I beg you O Yahweh ¿ not [was] this word my until was I on own land my there-fore I did [the] first time to flee Tarshish towards that I knew that you [are] a God gracious and compassionate long of anger and great of covenant loyalty and [who] relents on evil.
3 Sasa, Ee Bwana, niondolee uhai wangu, kwa kuwa ni afadhali mimi nife kuliko kuishi.”
And therefore O Yahweh take please life my from me for [is] good death my more than life my.
4 Lakini Bwana akamjibu, “Je unayo haki yoyote kukasirika?”
And he said Yahweh ¿ rightly does it burn to you.
5 Yona akatoka nje akaketi mahali upande wa mashariki wa mji. Hapo akajitengenezea kibanda, akaketi kwenye kivuli chake na kungojea ni nini kitakachotokea katika mji.
And he went out Jonah from the city and he sat from east of the city and he made for himself there a shelter and he sat under it in the shade until that he will see what? will it be in the city.
6 Ndipo Bwana, Mungu akaweka tayari mzabibu na kuufanya uote, kumpa Yona kivuli kilichomfunika kichwa ili kuondoa taabu yake, naye Yona akafurahi sana kwa ajili ya ule mzabibu.
And he appointed Yahweh God a plant and it went up - over Jonah to be shade over head his to deliver him from distress his and he rejoiced Jonah on the plant a joy great.
7 Lakini kesho yake asubuhi na mapema Mungu akaamuru buu, autafune mzabibu huo nao ukanyauka.
And he appointed God a worm when came up the dawn to the next day and it attacked the plant and it withered.
8 Wakati jua lilipochomoza, Mungu akautuma upepo wa hari wa mashariki, nalo jua likawaka juu ya kichwa cha Yona mpaka akazimia. Akatamani kufa, naye akasema, “Ni afadhali mimi nife kuliko kuishi.”
And it was - when arose the sun and he appointed God a wind an east wind hot and it struck the sun on [the] head of Jonah and he became faint and he asked life his to die and he said [is] good death my more than life my.
9 Lakini Mungu alimwambia Yona, “Je, unayo haki kukasirika kuhusu mzabibu huo?” Akasema, “Ndiyo, ninayo haki. Nimekasirika kiasi cha kufa.”
And he said God to Jonah ¿ rightly does it burn to you on the plant and he said rightly it burns to me to death.
10 Lakini Bwana akamwambia, “Wewe unakasirika kwa ajili ya mzabibu huu, nawe hukuusababisha kuota wala kuutunza. Uliota usiku mmoja, nao ukafa usiku mmoja.
And he said Yahweh you you had compassion on the plant which not you had toiled in it and not you had made grow it that a son of a night it was and a son of a night it perished.
11 Lakini Ninawi ina zaidi ya watu 120,000 ambao hawawezi kupambanua kulia au kushoto, pamoja na ngʼombe wengi. Je, hainipasi kufikiri juu ya mji ule mkubwa?”
And I not will I have compassion? on Nineveh the city great which there in it [are] many more than two [plus] ten ten thousand person[s] who not he distinguishes between right [hand] his and left his and livestock much.