< Yona 3 >
1 Ndipo neno la Bwana likamjia Yona mara ya pili:
Et la parole du Seigneur fut adressée une seconde fois à Jonas, disant:
2 “Ondoka uende katika mji mkubwa wa Ninawi, ukautangazie ujumbe ninaokupa.”
Lève-toi, et va dans Ninive la grande cité, et prêches-y ce que moi je te dis de prêcher.
3 Yona akalitii neno la Bwana naye akaenda Ninawi. Basi Ninawi ulikuwa mji maarufu sana, ilichukua siku tatu kuuzunguka.
Et Jonas se leva, et alla à Ninive selon la parole du Seigneur; or Ninive était une grande cité de trois jours de chemin.
4 Siku ya kwanza, Yona aliingia mjini. Akatangaza: “Baada ya siku arobaini Ninawi utaangamizwa.”
Jonas commença à entrer dans la cité, à faire le chemin d’un jour; et il cria, et il dit: Encore quarante jours et Ninive sera renversée.
5 Watu wa Ninawi wakamwamini Mungu, wakatangaza kufunga, watu wote kuanzia mkubwa sana hadi yule mdogo kabisa, wakavaa nguo za gunia.
Les hommes de Ninive crurent en Dieu, et ils publièrent un jeûne, et se revêtirent de cilices, depuis le plus grand jusqu’au plus petit.
6 Habari zilipomfikia mfalme wa Ninawi, aliondoka kwenye kiti chake cha enzi, akavua majoho yake ya kifalme, akajifunika nguo ya gunia kisha akaketi chini mavumbini.
Et le bruit en parvint au roi de Ninive; et il se leva de son trône, et quitta son vêtement, et se revêtit d’un sac, et s’assit sur la cendre.
7 Ndipo akatoa tangazo katika Ninawi yote: “Kwa amri ya mfalme na wakuu wake: “Msiruhusu mtu yeyote au mnyama, makundi ya ngʼombe au wanyama wengine wafugwao, kuonja kitu chochote, msiwaruhusu kula wala kunywa.
Et il cria et dit dans Ninive par la bouche du roi et de ses princes, disant: Que les hommes et les animaux, et les bœufs et les troupeaux de menu bétail ne goûtent rien; et qu’ils ne paissent point, et ne boivent point d’eau.
8 Bali wanadamu na wanyama wafunikwe kwa nguo za gunia. Kila mmoja afanye hima kumwomba Mungu. Waziache njia zao mbaya na udhalimu ulio mikononi mwao.
Et que les hommes se couvrent de sacs ainsi que les animaux, et qu’ils crient au Seigneur avec force, et que chacun se convertisse de sa voie mauvaise, et de l’iniquité qui est en leurs mains.
9 Ni nani ajuaye? Huenda Mungu akaghairi kwa huruma yake akaacha hasira yake kali ili tusiangamie.”
Qui sait si Dieu ne reviendra pas et ne pardonnera pas; et s’il ne se détournera pas de la fureur de sa colère, et nous ne périrons pas?
10 Mungu alipoona walivyofanya na jinsi walivyogeuka kutoka njia zao mbaya, akawa na huruma wala hakuleta maangamizi juu yao kama alivyokuwa ameonya.
Et Dieu vit leurs œuvres, il vit qu’ils étaient convertis de leur voie mauvaise; et Dieu eut pitié d’eux, touchant le mal qu’il avait dit qu’il leur ferait, et il ne le fit pas.