< Yona 2 >

1 Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
И помолися Иона ко Господу Богу своему от чрева китова
2 Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol h7585)
и рече: возопих в скорби моей ко Господу Богу моему, и услыша мя из чрева адова вопль мой, услышал еси глас мой: (Sheol h7585)
3 Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
отвергл мя еси во глубины сердца морскаго, и реки обыдоша мя вся высоты Твоя и волны Твоя мне преидоша.
4 Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
И аз рех: отринуся от очию Твоею: еда приложу призрети ми ко храму святому Твоему?
5 Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
Возлияся на мя вода до души моея, бездна обыде мя последняя, понре глава моя в разселины гор,
6 Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
снидох в землю, еяже вереи ея заклепи вечнии: и да взыдет из истления живот мой к Тебе, Господи Боже мой.
7 “Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
Внегда скончаватися от мене души моей, Господа помянух, и да приидет к Тебе молитва моя ко храму святому Твоему.
8 “Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
Хранящии суетная и ложная милость свою оставиша:
9 Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
аз же со гласом хваления и исповедания пожру Тебе, елика обещах, воздам Тебе во спасение мое Господеви.
10 Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.
И повеле Господь китови, и изверже Иону на сушу.

< Yona 2 >