< Yona 2 >

1 Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
Et Jonas pria le Seigneur son Dieu, dans le ventre de la baleine.
2 Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol h7585)
Et il dit: J'ai crié dans ma tribulation au Seigneur mon Dieu, et Il m'a exaucé; mon cri est parti des entrailles de l'enfer, et Tu as écouté ma voix; (Sheol h7585)
3 Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
Tu m'as précipité au plus profond du cœur de la mer; et les fleuves m'ont enveloppé, et toutes tes grandes vagues, tous Tes flots ont passé sur moi.
4 Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
Et j'ai dit: C'est moi qui me suis éloigné de Tes yeux; me permettras-Tu de voir encore Ton saint temple?
5 Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
L'eau s'est répandue autour de moi, jusqu'à l'âme; l'abîme le plus profond m'a enclos, et ma tête a plongé
6 Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
jusqu'aux racines des monts; je suis descendu sous la terre, dont les verrous sont des barrières éternelles. Seigneur mon Dieu, que la destruction de ma vie remonte à la surface des flots.
7 “Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
En la défaillance de mon âme, je me suis souvenu de Toi, Seigneur; que ma prière arrive à Toi dans Ton saint temple!
8 “Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
Ceux-là seuls qui s'attachent aux vanités et aux mensonges ont renoncé à Ta miséricorde.
9 Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
Pour moi, je T'offrirai dans mes chants un sacrifice de louanges et d'admiration; je rendrai au Seigneur les vœux que je Lui ai faits pour mon salut.
10 Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.
Et le Seigneur donna ordre à la baleine, et elle rejeta Jonas sur la terre ferme.

< Yona 2 >