< Yona 2 >

1 Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
Then Jonah prayed to the Lord his God from the belly of the fish.
2 Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol h7585)
He began, “In my agony I cried out to the Lord and he answered me; from the depths of Sheol I pleaded for help and you answered me. (Sheol h7585)
3 Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
You threw me into the deep, all the way down to the bottom of the sea. Water flooded all around me; your crashing waves rolled over me.
4 Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
I said to myself, ‘The Lord has banished me from his sight. Will I ever see your holy Temple again?’
5 Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
The water swirled over me so I couldn't breathe; the deep sucked me down; seaweed wrapped itself around my head.
6 Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
I sank down to the base of the mountains; the earth barred me in forever. But you, my Lord, my God, brought me back up from the abyss.
7 “Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
As my life ebbed away, I remembered the Lord; my prayer came to you in your holy Temple.
8 “Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
Those who worship worthless idols give up their trust in God's goodness.
9 Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
But I will offer you sacrifices, shouting out my thanks. I will keep my promises to you, for salvation comes from the Lord.”
10 Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.
Then the Lord told the fish to spit out Jonah onto the shore.

< Yona 2 >