< Yona 2 >
1 Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
And Jonah prayed to the Lord, his God, from the belly of the fish.
2 Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol )
And he said: “I cried out to the Lord from my tribulation, and he heeded me. From the belly of hell, I cried out, and you heeded my voice. (Sheol )
3 Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
And you have thrown me into the deep, in the heart of the sea, and a flood has encircled me. All your whirlpools and your waves have passed over me.
4 Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
And I said: I am expelled from the sight of your eyes. Yet, truly, I will see your holy temple again.
5 Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
The waters surrounded me, even to the soul. The abyss has walled me in. The ocean has covered my head.
6 Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
I descended to the base of the mountains. The bars of the earth have enclosed me forever. And you will raise up my life from corruption, Lord, my God.
7 “Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
When my soul was in anguish within me, I called to mind the Lord, so that my prayer might come to you, to your holy temple.
8 “Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
Those who in vain observe vanities, abandon their own mercy.
9 Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
But I, with a voice of praise, will sacrifice to you. I will repay whatever I have vowed to the Lord, because of my salvation.”
10 Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.
And the Lord spoke to the fish, and it vomited Jonah onto dry land.