< Yona 2 >

1 Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
And Jonas prayed to the Lord his God out of the belly of the whale,
2 Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol h7585)
and said, I cried in my affliction to the Lord my God, and he hearkened to me, [even] to my cry out of the belly of hell: thou heardest my voice. (Sheol h7585)
3 Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
Thou didst cast me into the depths of the heart of the sea, and the floods compassed me: all thy billows and thy waves have passed upon me.
4 Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
And I said, I am cast out of thy presence: shall I indeed look again toward thy holy temple?
5 Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
Water was poured around me to the soul: the lowest deep compassed me, my head went down
6 Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
to the clefts of the mountains; I went down into the earth, whose bars are the everlasting barriers: yet, O Lord my God, let my ruined life be restored.
7 “Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
When my soul was failing me, I remembered the Lord; and may my prayer come to thee into thy holy temple.
8 “Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
They that observe vanities and lies have forsaken their own mercy.
9 Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
But I will sacrifice to thee with the voice of praise and thanksgiving: all that I have vowed I will pay to thee, the Lord of [my] salvation.
10 Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.
And the whale was commanded by the Lord, and it cast up Jonas on the dry [land].

< Yona 2 >