< Yona 2 >

1 Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
約拿在魚腹中禱告耶和華-他的上帝,
2 Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol h7585)
說: 我遭遇患難求告耶和華, 你就應允我; 從陰間的深處呼求, 你就俯聽我的聲音。 (Sheol h7585)
3 Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
你將我投下深淵, 就是海的深處; 大水環繞我, 你的波浪洪濤都漫過我身。
4 Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
我說:我從你眼前雖被驅逐, 我仍要仰望你的聖殿。
5 Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
諸水環繞我,幾乎淹沒我; 深淵圍住我; 海草纏繞我的頭。
6 Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
我下到山根, 地的門將我永遠關住。 耶和華-我的上帝啊, 你卻將我的性命從坑中救出來。
7 “Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
我心在我裏面發昏的時候, 我就想念耶和華。 我的禱告進入你的聖殿, 達到你的面前。
8 “Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
那信奉虛無之神的人, 離棄憐愛他們的主;
9 Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
但我必用感謝的聲音獻祭與你。 我所許的願,我必償還。 救恩出於耶和華。
10 Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.
耶和華吩咐魚,魚就把約拿吐在旱地上。

< Yona 2 >