< Yona 1 >
1 Neno la Bwana lilimjia Yona mwana wa Amitai:
Agora a palavra de Javé veio a Jonas, filho de Amitai, dizendo:
2 “Nenda katika mji mkubwa wa Ninawi ukahubiri juu yake, kwa sababu uovu wake umekuja juu mbele zangu.”
“Levanta-te, vai a Nínive, aquela grande cidade, e prega contra ela, pois a maldade deles surgiu diante de mim”.
3 Lakini Yona alimkimbia Bwana na kuelekea Tarshishi. Alishuka mpaka Yafa, ambapo alikuta meli iliyokuwa imepangwa kuelekea bandari ile. Baada ya kulipa nauli, akapanda melini na kuelekea Tarshishi ili kumkimbia Bwana.
Mas Jonas se levantou para fugir para Tarshish da presença de Yahweh. Ele foi até Joppa, e encontrou um navio indo para Tarshish; então ele pagou sua passagem, e desceu para lá, para ir com eles para Tarshish da presença de Yahweh.
4 Ndipo Bwana akatuma upepo mkali baharini, nayo dhoruba kali sana ikavuma hata meli ikawa hatarini kuvunjika.
Mas Yahweh enviou um grande vento no mar, e houve uma forte tempestade no mar, de modo que era provável que o navio se separasse.
5 Mabaharia wote waliogopa na kila mmoja akamlilia mungu wake mwenyewe. Nao wakatupa mizigo baharini ili meli ipungue uzito. Lakini Yona alikuwa ameteremkia chumba cha ndani ya meli, mahali ambapo alilala na kupatwa na usingizi mzito.
Então os marinheiros ficaram com medo, e cada homem chorou a seu deus. Eles jogaram a carga que estava no navio no mar para aliviar o navio. Mas Jonas tinha descido para as partes mais íntimas do navio e estava deitado, e dormia profundamente.
6 Nahodha akamwendea na kusema, “Wewe unawezaje kulala? Amka ukamwite mungu wako! Huenda akatuangalia, tusiangamie.”
Então o comandante do navio veio até ele e lhe disse: “O que você quer dizer com “dorminhoco”? Levante-se, chame seu Deus! Talvez seu Deus nos perceba, para que não pereçamos”.
7 Kisha mabaharia wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tupige kura tumtafute anayehusika na maafa haya.” Wakapiga kura, kura ikamwangukia Yona.
Todos disseram um para o outro: “Venha! Vamos lançar sortes, para que possamos saber quem é o responsável por este mal que está sobre nós”. Então eles lançaram a sorte, e a sorte caiu sobre Jonas.
8 Kwa hiyo walimuuliza, “Tuambie, ni nani anayehusika kwa kutuletea tatizo hili lote? Unafanya kazi gani? Umetoka wapi? Nchi yako ni ipi? Wewe ni kutoka taifa lipi?”
Então eles lhe perguntaram: “Diga-nos, por favor, por cuja causa este mal está sobre nós”. Qual é a sua ocupação? De onde você vem? Qual é o seu país? De que povo você é?”
9 Akajibu, “Mimi ni Mwebrania, nami namwabudu Bwana, Mungu wa Mbinguni, aliyeumba bahari na nchi kavu.”
Ele lhes disse: “Eu sou hebreu e temo Yahweh, o Deus do céu, que fez o mar e a terra seca”.
10 Hili liliwaogopesha nao wakamuuliza, “Umefanya nini?” (Walijua alikuwa anamkimbia Bwana, kwa sababu alishawaambia hivyo.)
Então os homens tiveram muito medo, e lhe disseram: “O que você fez? Pois os homens sabiam que ele estava fugindo da presença de Yahweh, porque ele lhes havia dito.
11 Bahari ilikuwa inazidi kuchafuka. Kwa hiyo walimuuliza, “Tukutendee nini ili kufanya bahari itulie kwa ajili yetu?”
Então eles lhe disseram: “O que devemos fazer com você, para que o mar seja calmo para nós?”. Pois o mar se tornava cada vez mais tempestuoso.
12 Akawajibu, “Niinueni mnitupe baharini, nayo itakuwa shwari. Ninajua mawimbi haya makubwa yamewatokea kwa ajili ya kosa langu.”
Ele lhes disse: “Levem-me para cima e me joguem no mar”. Então o mar será calmo para vocês; pois sei que por minha causa esta grande tempestade está sobre vocês”.
13 Badala yake, wale watu walijitahidi kupiga makasia wawezavyo ili wapate kurudi pwani. Lakini hawakuweza, kwa kuwa bahari ilizidi kuchafuka kuliko mwanzo.
Mesmo assim, os homens remaram com dificuldade para levá-los de volta à terra; mas não puderam, pois o mar cresceu cada vez mais tempestuoso contra eles.
14 Ndipo wakamlilia Bwana, “Ee Bwana, tafadhali usituue kwa kuondoa uhai wa mtu huyu. Usituhesabie hatia kwa kuutoa uhai wa mtu asiyekuwa na hatia, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umefanya kama ilivyokupendeza.”
Por isso gritaram a Javé, e disseram: “Nós te imploramos, Javé, nós te imploramos, não nos deixes morrer pela vida deste homem, e não nos deites sangue inocente; pois tu, Javé, fizeste o que te agradou”.
15 Kisha walimchukua Yona, wakamtupa baharini nayo bahari iliyokuwa imechafuka ikatulia.
Então eles pegaram Jonas e o jogaram no mar; e o mar cessou sua fúria.
16 Katika jambo hili watu wakamwogopa Bwana sana, wakamtolea Bwana dhabihu na kumwekea nadhiri.
Então os homens temeram muito a Javé; e ofereceram um sacrifício a Javé e fizeram votos.
17 Lakini Bwana akamwandaa nyangumi kummeza Yona, naye Yona alikuwa ndani ya tumbo la nyangumi kwa siku tatu, usiku na mchana.
Yahweh preparou um peixe enorme para engolir Jonas, e Jonas estava na barriga do peixe por três dias e três noites.