< Yohana 1 >
1 Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
Na początku było Słowo. Było ono u Boga i było Bogiem.
2 Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
Od samego początku było razem z Bogiem.
3 Vitu vyote viliumbwa kwa yeye, wala pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa.
Ono powołało wszystko do istnienia. I nic, co zostało stworzone, nie zaistniało bez Niego.
4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
W Nim było życie, a życie jest dla ludzi światłem.
5 Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.
To Światło świeci w ciemnościach, a mrok nie był w stanie Go pochłonąć.
6 Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
Bóg posłał swojego człowieka, imieniem Jan,
7 Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
aby powiedział ludziom o prawdziwym Świetle i aby dzięki niemu wszyscy uwierzyli.
8 Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
Sam Jan nie był Światłem, lecz miał o Nim opowiedzieć.
9 Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
I nadeszło prawdziwe Światło, które oświeca każdego człowieka, przychodzącego na świat.
10 Huyo Neno alikuwako ulimwenguni na ingawa ulimwengu uliumbwa kupitia kwake, haukumtambua.
Pojawiło się na świecie, który dzięki Niemu powstał, ale świat Go nie rozpoznał.
11 Alikuja kwa walio wake, lakini wao hawakumpokea.
Przyszło do swojej własności, ale swoi Go nie przyjęli.
12 Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
Tym jednak, którzy Je przyjęli, i uwierzyli Mu dało prawo stać się dziećmi Bożymi,
13 Hawa ndio wasiozaliwa kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali kwa mapenzi ya Mungu.
które narodziły się nie fizycznie —w wyniku namiętności czy ludzkich planów—ale z Boga.
14 Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.
Słowo stało się ciałem i jako człowiek zamieszkało wśród nas. Ujrzeliśmy więc Jego chwałę—chwałę, jaką Ojciec obdarzył swojego jedynego Syna, pełnego łaski i prawdy.
15 Yohana alishuhudia habari zake, akapaza sauti, akisema, “Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’”
Jan Chrzciciel powiedział o Nim, wołając do zebranych wokół niego ludzi: —To właśnie o Nim mówiłem: „Nadchodzi ktoś większy ode mnie, bo istniał wcześniej niż ja!”.
16 Kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema juu ya neema.
Z Jego bogactwa wszyscy otrzymaliśmy wiele łask.
17 Kwa kuwa sheria ilitolewa kwa mkono wa Mose, lakini neema na kweli imekuja kupitia Yesu Kristo.
Mojżesz dał nam Prawo, natomiast dzięki Jezusowi Chrystusowi nadeszła łaska i prawda.
18 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote, ila ni Mungu Mwana pekee, aliye kifuani mwa Baba ndiye ambaye amemdhihirisha.
Boga nikt nigdy nie widział, a pokazał Go nam Jedyny Syn—Bóg, który stanowi jedno z Ojcem.
19 Huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu kumuuliza, “Wewe ni nani?”
Żydowscy przywódcy z Jerozolimy wysłali do Jana Chrzciciela kapłanów i ich pomocników z pytaniem: —Kim właściwie jesteś?
20 Yohana alikiri waziwazi pasipo kuficha akasema, “Mimi si Kristo.”
Wtedy on jednoznacznie i dobitnie odpowiedział: —Nie jestem Mesjaszem!
21 Wakamuuliza, “Wewe ni nani basi? Je, wewe ni Eliya?” Yeye akajibu, “Hapana, mimi siye.” “Je, wewe ni yule Nabii?” Akajibu, “Hapana.”
—No to kim? Eliaszem?—pytali. —Nie. —To może prorokiem? —Też nie—odpowiedział Jan.
22 Ndipo wakasema, “Basi tuambie wewe ni nani ili tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wewe wasemaje juu yako mwenyewe?”
—Kim więc jesteś? Co mamy powiedzieć tym, którzy nas wysłali? Co możesz o sobie powiedzieć?—dopytywali go.
23 Akawajibu kwa maneno ya nabii Isaya, akisema, “Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Yanyoosheni mapito ya Bwana.’”
—Jak powiedział prorok Izajasz: „Jestem głosem wołającego na pustyni: Przygotujcie Panu drogę!”—odrzekł Jan.
24 Basi walikuwa wametumwa watu kutoka kwa Mafarisayo
Niektórzy wysłannicy, należący do ugrupowania faryzeuszy,
25 wakamuuliza, “Kama wewe si Kristo, wala si Eliya na wala si yule Nabii, kwa nini basi unabatiza?”
zapytali go: —Dlaczego więc chrzcisz, skoro nie jesteś ani Mesjaszem, ani Eliaszem, ani prorokiem?
26 Yohana akawajibu, “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini katikati yenu yupo mtu msiyemjua.
—Ja zanurzam tylko w wodzie—odparł Jan. —Lecz niebawem nadejdzie ktoś, kto już jest wśród was, ale na razie nie dał się wam poznać. Ja nie jestem nawet godzien zdjąć Mu butów!
27 Yeye ajaye baada yangu, sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”
28 Mambo haya yote yalitukia huko Bethania, ngʼambo ya Mto Yordani, mahali Yohana alipokuwa akibatiza.
Miało to miejsce po drugiej stronie Jordanu, w Betanii, gdzie Jan udzielał ludziom chrztu.
29 Siku iliyofuata, Yohana alimwona Yesu akimjia akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
Następnego dnia Jan ujrzał nadchodzącego Jezusa i rzekł: —Oto Baranek, którego Bóg złoży w ofierze, aby usunąć grzech świata!
30 Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Mtu anakuja baada yangu ambaye ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’
To Jego miałem na myśli mówiąc, że „nadchodzi ktoś większy ode mnie, bo istniał wcześniej niż ja!”.
31 Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini sababu ya kuja nikibatiza kwa maji ni ili yeye apate kufunuliwa kwa Israeli.”
Nie wiedziałem, że to On, ale po to właśnie przyszedłem i zacząłem chrzcić ludzi, aby ogłosić Izraelowi Jego nadejście.
32 Kisha Yohana akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho akishuka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake.
Jan kontynuował: —Widziałem Ducha, który zstąpił na Niego z nieba jak gołąb.
33 Mimi nisingemtambua, lakini yeye aliyenituma nibatize kwa maji alikuwa ameniambia, ‘Yule mtu utakayemwona Roho akimshukia na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho Mtakatifu.’
Nie wiedziałem, że to On, ale Bóg, który mnie posłał, abym zanurzał ludzi w wodzie, powiedział: „Ten, na którego zstąpi Duch i spocznie na Nim, będzie zanurzał ludzi w Duchu Świętym”.
34 Mimi mwenyewe nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”
Widziałem to i dlatego oświadczam, że On jest Synem Boga!
35 Siku iliyofuata, Yohana alikuwa huko tena pamoja na wanafunzi wake wawili.
Następnego dnia Jan stał z dwoma uczniami.
36 Alipomwona Yesu akipita, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu!”
Gdy zobaczył idącego Jezusa, powiedział: —Oto Baranek, którego Bóg złoży w ofierze!
37 Wale wanafunzi wawili walipomsikia Yohana akisema haya, wakamfuata Yesu.
Obaj uczniowie usłyszeli to i poszli za Jezusem.
38 Yesu akageuka, akawaona wakimfuata akawauliza, “Mnataka nini?” Wakamwambia, “Rabi,” (maana yake Mwalimu), “Unaishi wapi?”
On obejrzał się i widząc, że za Nim idą, zapytał: —Czego szukacie? —Rabbi! (to znaczy: „Nauczycielu!”). Gdzie się zatrzymałeś na nocleg?—zapytali.
39 Yesu akawajibu, “Njooni, nanyi mtapaona!” Hivyo wakaenda na kupaona mahali alipokuwa anaishi, wakakaa naye siku ile, kwa kuwa ilikuwa yapata saa kumi.
—Chodźcie i zobaczcie—odpowiedział Jezus. Poszli więc z Nim, a ponieważ było już około czwartej po południu, zostali u Niego do końca dnia.
40 Andrea nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia yale Yohana aliyokuwa amesema, naye ndiye alimfuata Yesu.
Jednym z nich był Andrzej, brat Szymona Piotra.
41 Kitu cha kwanza Andrea alichofanya ni kumtafuta Simoni nduguye na kumwambia, “Tumemwona Masiya” (yaani, Kristo).
Odszukał on później Szymona i powiedział: —Znaleźliśmy Mesjasza! (to znaczy: „Chrystusa”).
42 Naye akamleta kwa Yesu. Yesu akamwangalia na kusema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana. Utaitwa Kefa” (ambalo limetafsiriwa Petro).
I zaprowadził go do Jezusa, a On spojrzał na niego i rzekł: —Ty jesteś Szymon, syn Jana. Ale od teraz będziesz się nazywał Kefas (to znaczy: „Piotr”—„skała”).
43 Siku iliyofuata Yesu aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”
Następnego dnia Jezus postanowił pójść do Galilei. Po drodze spotkał Filipa i rzekł do niego: —Chodź ze Mną.
44 Basi Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji alikotoka Andrea na Petro.
Filip pochodził z Betsaidy, rodzinnego miasteczka Andrzeja i Piotra.
45 Filipo naye akamkuta Nathanaeli na kumwambia, “Tumemwona yeye ambaye Mose aliandika habari zake katika Sheria na ambaye pia manabii waliandika kumhusu, yaani, Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”
Spotkał on później Natanaela i powiedział mu: —Znaleźliśmy Tego, o którym pisał Mojżesz i prorocy! To Jezus, syn Józefa z Nazaretu!
46 Nathanaeli akauliza, “Nazareti! Je, kitu chochote chema chaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”
—Z Nazaretu?!—zdziwił się Natanael. —Czy stamtąd może pochodzić coś dobrego? —Sam się przekonaj!—odrzekł Filip.
47 Yesu alipomwona Nathanaeli anakaribia, akanena habari zake akasema, “Tazama huyu ni Mwisraeli kweli kweli; hana hila ndani yake.”
Gdy zbliżali się do Jezusa, On zobaczył Natanaela i powiedział: —Oto prawdziwy Izraelita, w którym nie ma fałszu.
48 Nathanaeli akamuuliza, “Umenifahamuje?” Yesu akamjibu, “Nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini, kabla hata Filipo hajakuita.”
—Skąd mnie znasz?—zdumiał się Natanael. —Widziałem cię pod drzewem figowym, zanim spotkał cię Filip—odrzekł Jezus.
49 Nathanaeli akamwambia, “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli!”
—Nauczycielu! Jesteś Synem Boga! Jesteś Królem Izraela!
50 Yesu akamwambia, “Unaamini kwa kuwa nilikuambia nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini? Basi utaona mambo makuu zaidi kuliko hilo.”
—Wierzysz w to, ponieważ powiedziałem, że widziałem cię, gdy byłeś pod drzewem figowym?—odparł Jezus. —Ujrzysz jeszcze więcej!
51 Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
Zapewniam was: Zobaczycie otwarte niebo i aniołów Boga wstępujących i zstępujących na Mnie, Syna Człowieczego.