< Yohana 1 >

1 Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
In the beginning was the WORD, and the WORD was with God, and the WORD was God.
2 Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
He was in the beginning with God.
3 Vitu vyote viliumbwa kwa yeye, wala pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa.
All things were made by him, and without him not one thing was made that now exists.
4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
In him was life, and the life was the light of men.
5 Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.
And the light shines in the darkness, and the darkness comprehends it not.
6 Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
There was a man sent from God, whose name was John.
7 Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
This man came as a witness, to testify of the Light, that all through him might believe.
8 Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
He was not the Light; but he came to testify of the Light.
9 Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
He was the true Light, which, coming into the world, gives light to every man.
10 Huyo Neno alikuwako ulimwenguni na ingawa ulimwengu uliumbwa kupitia kwake, haukumtambua.
He was in the world, and the world was made by him, and the world knew him not.
11 Alikuja kwa walio wake, lakini wao hawakumpokea.
He came to his own country, and his own people received him not.
12 Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
But as many as received him, to them he gave the privilege of becoming the children of God, even to those who believe on his name;
13 Hawa ndio wasiozaliwa kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali kwa mapenzi ya Mungu.
who were begotten, not of blood, nor of the will of the flesh, nor of the will of man, but of God.
14 Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.
And the WORD became flesh, and tabernacled among us, (and we beheld his glory, the glory as of the only begotten of the Father, ) full of grace and of truth.
15 Yohana alishuhudia habari zake, akapaza sauti, akisema, “Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’”
John testified of him, and cried, saying: This is he of whom I said: He that comes after me, is now before me, for he existed before me.
16 Kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema juu ya neema.
And from his fullness have we all received, even grace for grace;
17 Kwa kuwa sheria ilitolewa kwa mkono wa Mose, lakini neema na kweli imekuja kupitia Yesu Kristo.
for the law was given through Moses, but the grace and the truth came through Jesus Christ.
18 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote, ila ni Mungu Mwana pekee, aliye kifuani mwa Baba ndiye ambaye amemdhihirisha.
No one has seen God at any time; the only begotten Son, who is in the bosom of the Father, he has revealed him.
19 Huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu kumuuliza, “Wewe ni nani?”
And this is the testimony of John, when the Jews sent priests and Levites from Jerusalem to ask him: Who are you?
20 Yohana alikiri waziwazi pasipo kuficha akasema, “Mimi si Kristo.”
And he confessed, and did not deny; and he confessed: I am not the Christ.
21 Wakamuuliza, “Wewe ni nani basi? Je, wewe ni Eliya?” Yeye akajibu, “Hapana, mimi siye.” “Je, wewe ni yule Nabii?” Akajibu, “Hapana.”
And they asked him: What then? Are you Elijah? And he said: I am not. Are you the prophet? And he answered: No.
22 Ndipo wakasema, “Basi tuambie wewe ni nani ili tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wewe wasemaje juu yako mwenyewe?”
They then said to him: Who are you? that we may give an answer to those who sent us; what say you of yourself?
23 Akawajibu kwa maneno ya nabii Isaya, akisema, “Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Yanyoosheni mapito ya Bwana.’”
He said: I am the voice of one crying in the wilderness, Make straight the way of the Lord; as said the prophet Isaiah.
24 Basi walikuwa wametumwa watu kutoka kwa Mafarisayo
And those who were sent were of the Pharisees;
25 wakamuuliza, “Kama wewe si Kristo, wala si Eliya na wala si yule Nabii, kwa nini basi unabatiza?”
and they asked him, and said to him: Why, then, do you immerse, if you are not the Christ, nor Elijah, nor the prophet?
26 Yohana akawajibu, “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini katikati yenu yupo mtu msiyemjua.
John answered them, saying: I immerse in water; but there stands one among you whom you know not.
27 Yeye ajaye baada yangu, sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”
He it is, who, though he comes after me, is now before me; the strap of whose sandal I am not worthy to loose.
28 Mambo haya yote yalitukia huko Bethania, ngʼambo ya Mto Yordani, mahali Yohana alipokuwa akibatiza.
These things were done in Bethany, beyond the Jordan, where John was immersing.
29 Siku iliyofuata, Yohana alimwona Yesu akimjia akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
The next day John saw Jesus coming to him, and said: Behold the Lamb of God, that takes away the sin of the world.
30 Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Mtu anakuja baada yangu ambaye ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’
This is he of whom I said, After me comes a man who is now before me, for he existed before me.
31 Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini sababu ya kuja nikibatiza kwa maji ni ili yeye apate kufunuliwa kwa Israeli.”
And I knew him not; but that he might be made manifest to Israel, for this reason I have come immersing in water.
32 Kisha Yohana akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho akishuka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake.
And John testified, saying: I saw the Spirit descending from heaven like a dove, and it remained on him.
33 Mimi nisingemtambua, lakini yeye aliyenituma nibatize kwa maji alikuwa ameniambia, ‘Yule mtu utakayemwona Roho akimshukia na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho Mtakatifu.’
And I knew him not; but he that sent me to immerse in water, said to me, On whom you shall see the Spirit descending and remaining, this is he that immerses in the Holy Spirit.
34 Mimi mwenyewe nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”
And I saw, and do testify that this is the Son of God.
35 Siku iliyofuata, Yohana alikuwa huko tena pamoja na wanafunzi wake wawili.
Again the next day, John was standing with two of his disciples.
36 Alipomwona Yesu akipita, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu!”
And looking on Jesus as he walked, he said: Behold the Lamb of God.
37 Wale wanafunzi wawili walipomsikia Yohana akisema haya, wakamfuata Yesu.
And the two disciples heard him speak, and they followed Jesus.
38 Yesu akageuka, akawaona wakimfuata akawauliza, “Mnataka nini?” Wakamwambia, “Rabi,” (maana yake Mwalimu), “Unaishi wapi?”
And Jesus turned, and saw them following, and said to them:
39 Yesu akawajibu, “Njooni, nanyi mtapaona!” Hivyo wakaenda na kupaona mahali alipokuwa anaishi, wakakaa naye siku ile, kwa kuwa ilikuwa yapata saa kumi.
What do you seek? They said to him: Rabbi, (which, when translated, is called Teacher, ) where abidest thou?
40 Andrea nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia yale Yohana aliyokuwa amesema, naye ndiye alimfuata Yesu.
He said to them: Come and see. They went and saw where he abode; and they remained with him that day; for it was about the tenth hour.
41 Kitu cha kwanza Andrea alichofanya ni kumtafuta Simoni nduguye na kumwambia, “Tumemwona Masiya” (yaani, Kristo).
One of the two that heard John speak, and followed him, was Andrew, the brother of Simon Peter.
42 Naye akamleta kwa Yesu. Yesu akamwangalia na kusema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana. Utaitwa Kefa” (ambalo limetafsiriwa Petro).
He first found his own brother Simon, and said to him: We have found the Messiah; (which, when translated, is the Christ; )
43 Siku iliyofuata Yesu aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”
and he brought him to Jesus. Jesus looking on him, said: You are Simon, the son of Jonah; you shall be called Cephas (which, when translated, is Rock).
44 Basi Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji alikotoka Andrea na Petro.
The day following, Jesus wished to go into Galilee; and he found Philip, and said to him: Follow me.
45 Filipo naye akamkuta Nathanaeli na kumwambia, “Tumemwona yeye ambaye Mose aliandika habari zake katika Sheria na ambaye pia manabii waliandika kumhusu, yaani, Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”
Now, Philip was of Bethsaida, the city of Andrew and Peter.
46 Nathanaeli akauliza, “Nazareti! Je, kitu chochote chema chaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”
Philip found Nathaniel, and said to him: We have found him of whom Moses in the law and the prophets did write, Jesus of Nazareth, the son of Joseph.
47 Yesu alipomwona Nathanaeli anakaribia, akanena habari zake akasema, “Tazama huyu ni Mwisraeli kweli kweli; hana hila ndani yake.”
And Nathaniel said to him: Can any thing good come out of Nazareth? Philip said to him: Come and see.
48 Nathanaeli akamuuliza, “Umenifahamuje?” Yesu akamjibu, “Nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini, kabla hata Filipo hajakuita.”
Jesus saw Nathaniel coming to him, and said of him: Be hold, an Israelite in truth, in whom there is no guile.
49 Nathanaeli akamwambia, “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli!”
Nathaniel said to him: How knowest thou me? Jesus answered and said to him: Before Philip called you, while you were under the fig-tree, I saw you.
50 Yesu akamwambia, “Unaamini kwa kuwa nilikuambia nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini? Basi utaona mambo makuu zaidi kuliko hilo.”
Nathaniel answered and said to him: Rabbi, thou art the Son of God; thou art the King of Israel.
51 Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
Jesus answered and said to him: Do you believe, because I said to you, I saw you under the fig-tree? You shall see greater things than these. And he said to him: Verily, verily I say to you, From this time you shall see heaven opened, and the angels of God ascending and descending upon the Son of man.

< Yohana 1 >