< Yohana 9 >

1 Yesu alipokuwa akipita, akamwona mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa.
Comme Jésus passait, il vit un homme aveugle de naissance.
2 Wanafunzi wake wakamuuliza, “Rabi, ni nani aliyetenda dhambi, ni huyu mtu au wazazi wake hata azaliwe kipofu?”
Et ses disciples lui demandèrent: Maître, qui a péché, cet homme ou ses parents, pour qu'il soit né aveugle?
3 Yesu akawajibu, “Huyu mtu wala wazazi wake hawakutenda dhambi. Alizaliwa kipofu ili kazi za Mungu zidhihirishwe katika maisha yake.
Jésus répondit: Ce n'est pas que lui ou ses parents aient péché, mais c'est afin que les oeuvres de Dieu soient manifestées en lui.
4 Yanipasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana, kwa kuwa usiku waja ambapo hakuna mtu awezaye kufanya kazi.
Tandis qu'il fait jour, il me faut accomplir les oeuvres de Celui qui m'a envoyé; la nuit vient, dans laquelle personne ne peut travailler.
5 Wakati niko ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
Pendant que je suis dans le monde, je suis la lumière du monde.
6 Baada ya kusema haya, akatema mate ardhini, akatengeneza tope kwa mate na kumpaka yule mtu kipofu machoni.
Ayant dit cela, il cracha à terre et fit de la boue avec sa salive; et il oignit de cette boue les yeux de l'aveugle.
7 Kisha akamwambia, “Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu.” (Siloamu maana yake ni aliyetumwa.) Ndipo yule kipofu akaenda, akanawa, naye akarudi akiwa anaona.
Puis il lui dit: Va; lave-toi au réservoir de Siloé — mot qui signifie Envoyé. — Il y alla donc et se lava, et il revint voyant clair.
8 Majirani zake na wale wote waliokuwa wamemwona hapo awali akiombaomba wakaanza kuuliza, “Je, huyu si yule aliyekuwa akiketi akiombaomba?”
Ses voisins, et ceux qui l'avaient vu auparavant demander l'aumône, disaient: N'est-ce pas celui qui se tenait assis et qui mendiait?
9 Wengine wakasema, “Ndiye.” Wengine wakasema, “Siye, bali wamefanana.” Lakini yeye akawaambia, “Mimi ndiye.”
Les uns disaient: C'est lui. D'autres disaient: Non, mais c'est quelqu'un qui lui ressemble. Lui disait: C'est bien moi.
10 Wakamuuliza, “Basi macho yako yalifumbuliwaje?”
Ils lui demandèrent alors: Comment tes yeux ont-ils été ouverts?
11 Yeye akawajibu, “Yule mtu aitwaye Yesu alitengeneza tope, akanipaka machoni mwangu, naye akaniambia nenda ukanawe katika Bwawa la Siloamu, ndipo nikanawa nami nikapata kuona!”
Il répondit; Cet homme, qu'on appelle Jésus, a fait de la boue; il en a oint mes yeux, et il m'a dit: Va au réservoir de Siloé, et lave-toi. J'y suis donc allé, je m'y suis lavé, et je vois.
12 Wale wakamuuliza, “Yeye huyo mtu yuko wapi?” Akawajibu, “Sijui.”
Ils lui dirent: Où est cet homme? Il répondit: Je ne sais pas.
13 Wakamleta kwa Mafarisayo yule mtu aliyekuwa kipofu hapo awali.
Ils amenèrent aux pharisiens celui qui avait été aveugle.
14 Basi siku hiyo Yesu alipotengeneza tope na kuyafungua macho ya huyo mtu ilikuwa Sabato.
Or, c'était un jour de sabbat que Jésus avait fait de la boue et avait ouvert les yeux de cet homme.
15 Mafarisayo nao wakaanza kumuuliza alivyopata kuponywa. Naye akawaambia, “Alinipaka tope kwenye macho yangu, nikanawa na sasa ninaona.”
Les pharisiens lui demandèrent à leur tour comment il avait recouvré la vue. Il leur répondit: Il m'a mis de la boue sur les yeux; je me suis lavé, et je vois.
16 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Huyu mtu hatoki kwa Mungu, kwa sababu hashiki Sabato.” Lakini wengine wakasema, “Awezaje mtu mwenye dhambi kufanya miujiza kama hii?” Wakagawanyika.
Alors quelques-uns des pharisiens dirent: Cet homme ne vient point de la part de Dieu, puisqu'il n'observe pas le sabbat. Mais d'autres disaient: Comment un pécheur pourrait-il faire de tels miracles? Et ils étaient divisés entre eux.
17 Hivyo wakamwambia tena yule mtu aliyekuwa kipofu, “Wewe ndiwe uliyefumbuliwa macho, wasemaje kuhusu mtu huyo?” Maana macho yako ndiyo yaliyofumbuliwa. Yeye akawajibu, “Yeye ni nabii.”
Alors ils demandèrent de nouveau à l'aveugle: Et toi, que dis-tu de cet homme, qui t'a ouvert les yeux? Il répondit: C'est un prophète!
18 Wale Wayahudi hawakuamini ya kuwa mtu huyo alikuwa kipofu, akapata kuona, mpaka walipowaita wazazi wake.
Mais les Juifs ne crurent pas que cet homme eût été aveugle et qu'il eût recouvré la vue, jusqu'à ce qu'ils eussent fait venir son père et sa mère.
19 Wakawauliza, “Je, huyu ni mtoto wenu, ambaye mnasema alizaliwa kipofu? Imekuwaje basi sasa anaona?”
Ils les interrogèrent et leur dirent: Est-ce bien là votre fils, que vous dites être né aveugle? Comment donc voit-il maintenant?
20 Wazazi wake wakajibu, “Tunajua ya kuwa huyu ni mtoto wetu na ya kuwa alizaliwa kipofu.
Ses parents répondirent: Nous savons que c'est là notre fils, et qu'il est né aveugle;
21 Lakini sisi hatujui ni kwa jinsi gani kwamba sasa anaona, wala hatujui ni nani aliyemfungua macho yake. Muulizeni, yeye ni mtu mzima na anaweza kujieleza mwenyewe.”
mais comment il se fait qu'il voit maintenant, nous ne le savons pas. Nous ne savons pas non plus qui lui a ouvert les yeux. Interrogez-le; il a de l'âge, il s'expliquera lui-même.
22 Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliwaogopa Wayahudi kwani walikuwa wamekubaliana kuwa mtu yeyote atakayemkiri Yesu kuwa ndiye Kristo atafukuzwa kutoka sinagogi.
Ses parents dirent cela, parce qu'ils craignaient les Juifs; car les Juifs avaient déjà décidé que si quelqu'un reconnaissait Jésus pour le Christ, il serait chassé de la synagogue.
23 Kwa hiyo wazazi wake wakasema, “Yeye ni mtu mzima. Muulizeni.”
C'est pour cela que ses parents dirent: Il a de l'âge, interrogez-le.
24 Hivyo kwa mara ya pili wakamwita yule aliyekuwa kipofu, nao wakamwambia, “Mpe Mungu utukufu! Sisi tunafahamu kuwa mtu huyu aliyekuponya ni mwenye dhambi.”
Les pharisiens appelèrent donc pour la seconde fois l'homme qui avait été aveugle, et ils lui dirent: Donne gloire à Dieu! Nous savons que cet homme est un pécheur.
25 Akawajibu, “Mimi sijui kama yeye ni mwenye dhambi. Lakini jambo moja ninalojua, nilikuwa kipofu na sasa ninaona.”
Il répondit: Je ne sais si c'est un pécheur; je sais une chose, c'est que j'étais aveugle, et que maintenant je vois.
26 Wakamuuliza, “Alikufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
Ils lui dirent encore: Que t'a-t-il fait? Comment t'a-t-il ouvert les yeux?
27 Akawajibu, “Tayari nimekwisha kuwaambia, nanyi hamtaki kunisikiliza. Mbona mnataka kusikia tena? Je, ninyi nanyi mnataka kuwa wanafunzi wake?”
Il leur répondit: Je vous l'ai déjà dit, et vous ne m'avez pas écouté. Pourquoi voulez-vous l'entendre encore une fois? Voulez-vous, vous aussi, devenir ses disciples?
28 Ndipo wakamtukana na kusema, “Wewe ndiwe mwanafunzi wake, Sisi ni wanafunzi wa Mose.
Alors ils se mirent à l'injurier, et ils lui dirent: C'est toi qui es son disciple; nous, nous sommes les disciples de Moïse.
29 Tunajua kwamba Mungu alisema na Mose, lakini kwa habari ya mtu huyu hatujui atokako.”
Nous savons que Dieu a parlé à Moïse; mais celui-ci, nous ne savons d'où il est.
30 Yule mtu akawajibu, “Hili ni jambo la ajabu! Hamjui anakotoka, naye amenifungua macho yangu!
Cet homme répondit: C'est là ce qui est étonnant, que vous ne sachiez pas d'où il est, alors qu'il m'a ouvert les yeux!
31 Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomcha na kumtii.
Nous savons que Dieu n'exauce pas les pécheurs; mais si quelqu'un craint Dieu et fait sa volonté, il l'exauce.
32 Tangu zamani hatujasikia kwamba mtu amemponya yeyote aliyezaliwa kipofu. (aiōn g165)
Jamais on n'a entendu dire que quelqu'un ait ouvert les yeux d'un aveugle-né. (aiōn g165)
33 Kama huyu mtu hakutoka kwa Mungu, asingeweza kufanya lolote.”
Si cet homme ne venait pas de la part de Dieu, il ne pourrait rien faire.
34 Wao wakamjibu, “Wewe ulizaliwa katika dhambi kabisa, nawe unajaribu kutufundisha?” Wakamfukuza atoke nje.
Ils lui répondirent: Tu es né entièrement dans le péché, et tu veux nous enseigner! Puis ils le jetèrent dehors.
35 Yesu aliposikia kuwa wamemfukuzia nje yule mtu aliyemfumbua macho, alimkuta akamuuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?”
Jésus apprit qu'on l'avait chassé; et, l'ayant rencontré, il lui dit: Crois-tu au Fils de Dieu?
36 Yule mtu akamjibu, “Yeye ni nani, Bwana? Niambie ili nipate kumwamini.”
Il répondit: Qui est-il, Seigneur, pour que je croie en lui?
37 Yesu akamjibu, “Umekwisha kumwona, naye anayezungumza nawe, ndiye.”
Jésus lui dit: Tu l'as vu, et c'est lui-même qui te parle!
38 Yule mtu akasema, “Bwana, naamini.” Naye akamwabudu.
Il reprit: Je crois. Seigneur! Et il se prosterna devant lui.
39 Yesu akasema, “Nimekuja ulimwenguni humu kwa ajili ya kuhukumu, ili wale walio vipofu wapate kuona, nao wale wanaoona, wawe vipofu.”
Alors Jésus dit: Je suis venu dans le monde pour exercer ce jugement: que ceux qui ne voient point, voient, et que ceux qui voient, deviennent aveugles.
40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa karibu naye wakamsikia na kumwambia, “Je, kweli sisi ni vipofu?”
Ceux des pharisiens qui étaient auprès de lui entendirent cela, et ils lui dirent: Et nous, sommes-nous aussi des aveugles?
41 Yesu akawajibu, “Kama mngekuwa vipofu kweli, msingekuwa na hatia ya dhambi, lakini kwa kuwa mnasema, ‘Tunaona,’ basi mna hatia.
Jésus leur répondit: Si vous étiez aveugles, vous seriez sans péché, mais comme vous dites: Nous voyons. — c'est pour cela que votre péché subsiste.

< Yohana 9 >