< Yohana 8 >

1 Lakini Yesu akaenda katika Mlima wa Mizeituni.
Ісус же пійшов на гору Оливну.
2 Alfajiri na mapema Yesu akaja tena Hekaluni, watu wote wakakusanyika, akakaa akaanza kuwafundisha.
Вранці ж ізнов прийшов у церкву, і всї люде приходили до Него; й сівши навчав їх.
3 Walimu wa sheria na Mafarisayo wakamleta mwanamke mmoja aliyefumaniwa akizini. Wakamsimamisha katikati ya umati wa watu wote.
Приводять же письменники та Фарисеї до Него жінку, схоплену в перелюбі, і, поставивши її посередині,
4 Wakamwambia Yesu, “Mwalimu, huyu mwanamke amekutwa akizini.
кажуть Йому: Учителю, сю жінку схоплено в перелюбі, на самому вчинку.
5 Katika sheria, Mose alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake wa namna hii, mpaka wafe. Sasa wewe wasemaje?”
В законі ж Мойсей нам звелів таких каменувати; Ти ж що кажеш?
6 Walimuuliza swali hili kama mtego ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Yesu akainama akaanza kuandika ardhini kwa kidole chake.
Се ж казали, спокушуючи Його, щоб мали чим винувата Його. Ісус же, схилившись до долу, писав пальцем по землі'.
7 Walipoendelea kumuulizauliza akainuka, akawaambia, “Kama kuna mtu yeyote miongoni mwenu ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe.”
Як же не переставали питати Його, піднявшись рече до них: Хто з вас без гріха, нехай первий кине камінь на неї.
8 Akainama tena na kuandika ardhini.
І, знов, схилившись до долу, писав по землї.
9 Waliposikia haya, wakaanza kuondoka mmoja mmoja, wakianzia wazee, hadi Yesu akabaki peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake.
Вони ж, почувши й докорені совістю, вийшли один за одним, почавши від старших та аж до останніх; і воетавсь один Ісус та жінка, стоячи посередині.
10 Yesu akainuka na kumwambia, “Wako wapi wale waliokuwa wanakuhukumu kuwa mwenye hatia?”
Піднявши ся ж Ісус і нікого не бачивши, тільки жінку, рече їй: Жінко, де ж ті винувателї твої? ніхто тебе не осудив?
11 Yule mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akamwambia, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda zako, kuanzia sasa usitende dhambi tena.”]
Вона ж каже: Нїхто, Господи. Рече ж їй Ісус: І я тебе не суджу: йди, і більш не гріши.
12 Kisha Yesu akasema nao tena akawaambia, “Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”
Знов же промовляв їм Ісус, глаголючи: Я сьвітло сьвіту. Хто йде слїдом за мною, не ходити ме в темряві, а мати ме сьвітло життя.
13 Mafarisayo wakamwambia, “Ushuhuda wako haukubaliki kwa kuwa unajishuhudia mwenyewe.”
Казали тодї Йому Фарисеї: Ти про себе сьвідкуєш; сьвідченнє Твоє неправдиве.
14 Yesu akawajibu, “Hata kama najishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli kwa sababu najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
Озвавсь Ісус і рече їм: Хоч я сьвідкую про себе, правдиве сьвідченнє моє; бо я знаю, звідкіля я прийшов, і куди йду.
15 Ninyi mnahukumu kwa kufuata vipimo vya kibinadamu, mimi simhukumu mtu yeyote.
Ви по тілу судите; я не суджу нікого.
16 Lakini hata kama nikihukumu, uamuzi wangu ni sahihi kwa sababu sitoi hukumu yangu peke yangu, bali niko pamoja na Baba, aliyenituma.
Коли я суджу, суд мій правдивий; бо я не один, а я й пославший мене Отець.
17 Imeandikwa katika Sheria yenu kwamba, ushahidi wa watu wawili ni thabiti.
І в законі ж вашому написано, що двох людей сьвідченнє правдиве.
18 Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma hunishuhudia.”
Я сьвідкую про себе, й сьвідкує про мене пославший мене Отець.
19 Ndipo wakamuuliza, “Huyo Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu, “Ninyi hamnifahamu mimi ni nani, wala hammfahamu Baba yangu. Kama mngenifahamu mimi, mngemfahamu na Baba yangu.”
Казали тодї Йому: Де Отець Твій? Відказав Ісус: Нї мене не знаєте, ні Отця мого. Коли б мене знали, й Отця мого знали б.
20 Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika chumba cha hazina Hekaluni. Lakini hakuna mtu aliyemkamata kwa kuwa saa yake ilikuwa haijawadia.
Такі слова промовив Ісус у скарбницї, навчаючи в церкві; і ніхто не хапав Його; бо ще не прийшла година Його.
21 Yesu akawaambia tena, “Ninaenda zangu, nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi ninyi hamwezi kuja.”
Рече їм тодї знов Ісус: Я йду, й шукати мете мене, і в гріхах ваших повмираєте. Куди ж я йду, ви не можете йти.
22 Ndipo wale Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Je, hii ndiyo sababu amesema, ‘Niendako mimi ninyi hamwezi kuja’?”
Сказали тодї Жиди: Чи не вбє Він себе, що каже: Куди я йду, ви не можете йти?
23 Akawaambia, “Ninyi mmetoka chini, mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
І рече їм: Ви од нижнього, я од вишнього; ви од сьвіту сього, я не од сьвіту сього.
24 Niliwaambia kuwa mtakufa katika dhambi zenu, kwa maana msipoamini ya kwamba ‘Mimi Ndiye,’ mtakufa katika dhambi zenu.”
Тим я сказав вам, що повмираєте в гріхах ваших: коли бо не увіруєте, що се я, повмираєте в гріхах ваших.
25 Wakamuuliza, “Wewe ni nani?” Naye Yesu akawajibu, “Mimi ndiye yule ambaye nimekuwa nikiwaambia tangu mwanzo.
Казали тодї Йому: Хто Ти єси? І рече їм Ісус: Той, що з почину, як і глалолю вам.
26 Nina mambo mengi ya kusema juu yenu na mengi ya kuwahukumu. Lakini yeye aliyenituma ni wa kweli, nami nanena na ulimwengu niliyoyasikia kutoka kwake.”
Багато маю про вас глаголати й судити; тільки ж Пославший мене правдивий; і я, що чув від Него, се глаголю в сьвітї.
27 Hawakuelewa kuwa alikuwa akiwaambia juu ya Baba yake wa Mbinguni.
Не розуміли, що про Отця їм глаголе.
28 Kisha Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha kumwinua juu Mwana wa Adamu, ndipo mtakapojua kuwa, ‘Mimi ndiye yule niliyesema na kwamba mimi sitendi jambo lolote peke yangu bali ninasema yale tu ambayo Baba yangu amenifundisha.
Рече ж їм Ісус: Як знесете вгору Сина чоловічого, тодї зрозумієте, що се я, і що від себе не роблю нїчого; тільки, як навчив мене Отець мій, таке глаголю.
29 Yeye aliyenituma yu pamoja nami, hajaniacha, kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.’”
І Пославший мене - зо мною; не зоставив мене одного Отець; бо я роблю всякого часу, що подобаєть ся Йому.
30 Wengi waliomsikia Yesu akisema maneno haya wakamwamini.
Як се Він промовляв, многі увірували в Него.
31 Kisha Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkidumu katika maneno yangu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli.
Рече тодї Ісус до Жидів, що увірували Йому: Коли пробувати мете у слові моєму, справді ви ученики мої будете,
32 Ndipo mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.”
і зрозумієте правду, й правда визволить вас.
33 Wao wakamjibu, “Sisi tu wazao wa Abrahamu, nasi hatujawa watumwa wa mtu yeyote. Wawezaje kusema kwamba tutawekwa huru?”
Відказали Йому: Ми насїннє Авраамове, й нї в кого не були в неволї ніколи. Як же Ти говориш, що вільнї будете?
34 Yesu akajibu, “Amin, amin nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
Відказав їм Ісус: Істино, істино глаголю вам: Що всякий, хто робить гріх, невільник гріха.
35 Mtumwa hakai nyumbani anakotumika siku zote, lakini mwana hukaa nyumbani daima. (aiōn g165)
Невільник же не пробував в дому до віку, Син пробував до віку. (aiōn g165)
36 Hivyo Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
Коли ж Син визволить вас, справді вільними будете.
37 Ninajua ya kuwa ninyi ni wazao wa Abrahamu, lakini mnatafuta wasaa wa kuniua kwa sababu ndani yenu hamna nafasi ya neno langu.
Знаю, що ви насїннє Авраамове; та шукаєте вбити мене, бо слово моє не містить ся в вас.
38 Ninasema yale niliyoyaona mbele za Baba yangu, nanyi inawapa kufanya yale mliyosikia kutoka kwa baba yenu.”
Я, що видїв ув Отця мого, глаголю; а ви, що видїли в отця вашого, робите.
39 Wakajibu, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, “Kama mngekuwa wazao wa Abrahamu mngefanya mambo yale aliyofanya Abrahamu.
Озвались вони й казали Йому: Отець наш Авраам. Рече їм Ісус: Коли б ви дїти Авраамові були, дїла Авраамові робили б.
40 Lakini sasa ninyi mnatafuta kuniua, mtu ambaye nimewaambia kweli ile niliyosikia kutoka kwa Mungu, Abrahamu hakufanya jambo la namna hii.
Тепер же шукаєте вбити мене, чоловіка, що вам правду глаголав, котру чув я від Бога. Сього Авраам не робив.
41 Ninyi mnafanya mambo afanyayo baba yenu.” Wakamjibu, “Sisi hatukuzaliwa kwa uzinzi. Tunaye Baba mmoja, Mungu pekee.”
Ви робите дїла отця вашого. Казали тодї Йому: Ми не з перелюбу родились: одного Отця маємо, Бога.
42 Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
Рече ж їм Ісус: Коли б Бог отець ваш був, любили б ви мене; бо я від Бога вийшов і приходжу, бо не від себе прийшов я, а Він мене післав.
43 Kwa nini hamwelewi ninayowaambia? Ni kwa sababu hamwezi kusikia nisemacho.
Чом бесїди моєї не розумієте? Бо не можете слухати слова мого.
44 Ninyi ni watoto wa baba yenu ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli maana hamna kweli ndani yake. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo.
Ви від отця диявола, й хотїння отця вашого диявола хочете робити. Той був душогубцем з почину; й в правдї не встояв; бо нема правди в йому. Коли говорить брехню, із свого говорить; бо він брехун і отець її.
45 Lakini kwa sababu nimewaambia kweli hamkuniamini!
А що я правду глаголю, не віруєте менї.
46 Je, kuna yeyote miongoni mwenu awezaye kunithibitisha kuwa mwenye dhambi? Kama nawaambia yaliyo kweli, mbona hamniamini?
Хто з вас докорить менї за гріх? Коли ж правду глаголю, чому ви не віруєте менї?
47 Yeye atokaye kwa Mungu husikia kile Mungu asemacho. Sababu ya ninyi kutosikia ni kwa kuwa hamtokani na Mungu.”
Хто від Бога, слова Божі слухає. Тому ви не слухаєте, що ви не від Бога.
48 Wayahudi wakamjibu Yesu, “Je, hatuko sahihi tunaposema ya kwamba wewe ni Msamaria na ya kwamba una pepo mchafu?”
Озвались тодї Жиди, й казали Йому: Чи недобре ми кажемо, що Самарянин єси Ти, і біса маєш?
49 Yesu akawajibu, “Mimi sina pepo mchafu, bali ninamheshimu Baba yangu, nanyi mnanidharau.
Відказав Ісус: Я біса не маю, а шаную Отця мого; ви ж не шануєте мене.
50 Lakini mimi sitafuti utukufu wangu mwenyewe, bali yuko anayetaka kunitukuza, naye ndiye mwamuzi.
Я ж не шукаю моєї слави; єсть, хто шукає й судить.
51 Amin, amin nawaambia, mtu yeyote akilitii neno langu hataona mauti milele.” (aiōn g165)
Істино, істино глаголю вам: Коли хто слово моє хоронити ме, смерти не побачить по вік. (aiōn g165)
52 Ndipo Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kwamba una pepo mchafu. Ikiwa Abrahamu alikufa na vivyo hivyo manabii, nawe unasema ‘Mtu akitii neno langu hatakufa milele.’ (aiōn g165)
Сказали тодї Йому Жиди: Тепер ми знаємо, що Ти біса маєш. Авраам умер і пророки, а Ти кажеш: Коли хто слово моє хоронити ме, не вкусить смерти по вік. (aiōn g165)
53 Je, wewe ni mkuu kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa na manabii ambao nao pia walikufa? Hivi wewe unajifanya kuwa nani?”
Хиба Ти більший єси, нїж отець наш Авраам, що вмер? І пророки повмирали. Ким Ти себе робиш?
54 Yesu akawajibu, “Kama nikijitukuza utukufu wangu hauna maana. Baba yangu, huyo ambaye ninyi mnadai kuwa ni Mungu wenu, ndiye anitukuzaye mimi.
Відказав Ісус: Коди я прославляю себе, слава моя нїщо. Єсть Отець мій, що прославляє мене, про котрого ви кажете, що Він Бог ваш.
55 Ingawa hamkumjua, mimi ninamjua. Kama ningesema simjui, ningekuwa mwongo kama ninyi, lakini mimi ninamjua na ninalitii neno lake.
не пізнали Його; я ж знаю Його. А коли я скажу, що не знаю Його, буду подобний вам ложник. Нї, знаю Його, й слово Його хороню.
56 Baba yenu Abrahamu alishangilia kwamba angaliiona siku yangu, naye akaiona na akafurahi.”
Авраам, отець ваш, рад був видїти день мій; та він увидїв, і зрадїв.
57 Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza hata miaka hamsini, wewe wasema umemwona Abrahamu?”
Казали тодї Жиди до Него: Не маєш пятидесяти років ще, і Авраама видїв єси?
58 Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, kabla Abrahamu hajakuwako, ‘Mimi niko.’”
Рече їм Ісус: Істино, істино глаголю вам: Перш нїж Авраамові бути, я був.
59 Ndipo wakaokota mawe ili kumpiga, lakini Yesu akajificha, naye akatoka Hekaluni.
Брали тодї каміннє, щоб кидати на Него; Ісус же сховав ся, і вийшов з церкви, пройшовши посеред них, і дійшов так мимо.

< Yohana 8 >