< Yohana 8 >
1 Lakini Yesu akaenda katika Mlima wa Mizeituni.
Et Jésus s’en alla à la montagne des Oliviers.
2 Alfajiri na mapema Yesu akaja tena Hekaluni, watu wote wakakusanyika, akakaa akaanza kuwafundisha.
Et au point du jour il vint encore au temple, et tout le peuple vint à lui; et s’étant assis, il les enseignait.
3 Walimu wa sheria na Mafarisayo wakamleta mwanamke mmoja aliyefumaniwa akizini. Wakamsimamisha katikati ya umati wa watu wote.
Et les scribes et les pharisiens lui amènent une femme surprise en adultère; et l’ayant placée devant lui,
4 Wakamwambia Yesu, “Mwalimu, huyu mwanamke amekutwa akizini.
ils lui disent: Maître, cette femme a été surprise sur le fait même, commettant adultère.
5 Katika sheria, Mose alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake wa namna hii, mpaka wafe. Sasa wewe wasemaje?”
Or, dans la loi, Moïse nous a commandé de lapider de telles femmes: toi donc, que dis-tu?
6 Walimuuliza swali hili kama mtego ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Yesu akainama akaanza kuandika ardhini kwa kidole chake.
Or ils disaient cela pour l’éprouver, afin qu’ils aient de quoi l’accuser. Mais Jésus, s’étant baissé, écrivait avec le doigt sur la terre.
7 Walipoendelea kumuulizauliza akainuka, akawaambia, “Kama kuna mtu yeyote miongoni mwenu ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe.”
Et comme ils continuaient à l’interroger, s’étant relevé, il leur dit: Que celui de vous qui est sans péché, jette le premier la pierre contre elle.
8 Akainama tena na kuandika ardhini.
Et s’étant encore baissé, il écrivait sur la terre.
9 Waliposikia haya, wakaanza kuondoka mmoja mmoja, wakianzia wazee, hadi Yesu akabaki peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake.
Et eux, l’ayant entendu, sortirent un à un, en commençant depuis les plus anciens jusqu’aux derniers; et Jésus fut laissé seul avec la femme devant lui.
10 Yesu akainuka na kumwambia, “Wako wapi wale waliokuwa wanakuhukumu kuwa mwenye hatia?”
Et Jésus, s’étant relevé et ne voyant personne que la femme, lui dit: Femme, où sont-ils, ceux-là, tes accusateurs? Nul ne t’a-t-il condamnée?
11 Yule mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akamwambia, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda zako, kuanzia sasa usitende dhambi tena.”]
Et elle dit: Nul, Seigneur. Et Jésus lui dit: Moi non plus, je ne te condamne pas; va, – dorénavant ne pèche plus.
12 Kisha Yesu akasema nao tena akawaambia, “Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”
Jésus donc leur parla encore, disant: Moi, je suis la lumière du monde; celui qui me suit ne marchera point dans les ténèbres, mais il aura la lumière de la vie.
13 Mafarisayo wakamwambia, “Ushuhuda wako haukubaliki kwa kuwa unajishuhudia mwenyewe.”
Les pharisiens donc lui dirent: Tu rends témoignage de toi-même; ton témoignage n’est pas vrai.
14 Yesu akawajibu, “Hata kama najishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli kwa sababu najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
Jésus répondit et leur dit: Quoique moi je rende témoignage de moi-même, mon témoignage est vrai, car je sais d’où je suis venu et où je vais; mais vous, vous ne savez pas d’où je viens et où je vais.
15 Ninyi mnahukumu kwa kufuata vipimo vya kibinadamu, mimi simhukumu mtu yeyote.
Vous, vous jugez selon la chair; moi, je ne juge personne.
16 Lakini hata kama nikihukumu, uamuzi wangu ni sahihi kwa sababu sitoi hukumu yangu peke yangu, bali niko pamoja na Baba, aliyenituma.
Et si aussi moi, je juge, mon jugement est vrai, car je ne suis pas seul, mais moi et le Père qui m’a envoyé.
17 Imeandikwa katika Sheria yenu kwamba, ushahidi wa watu wawili ni thabiti.
Et il est écrit aussi dans votre loi, que le témoignage de deux hommes est vrai.
18 Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma hunishuhudia.”
Moi, je rends témoignage de moi-même; et le Père qui m’a envoyé rend aussi témoignage de moi.
19 Ndipo wakamuuliza, “Huyo Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu, “Ninyi hamnifahamu mimi ni nani, wala hammfahamu Baba yangu. Kama mngenifahamu mimi, mngemfahamu na Baba yangu.”
Ils lui dirent donc: Où est ton père? Jésus répondit: Vous ne connaissez ni moi, ni mon Père; si vous m’aviez connu, vous auriez connu aussi mon Père.
20 Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika chumba cha hazina Hekaluni. Lakini hakuna mtu aliyemkamata kwa kuwa saa yake ilikuwa haijawadia.
Il dit ces paroles dans le trésor, enseignant dans le temple; et personne ne le prit, parce que son heure n’était pas encore venue.
21 Yesu akawaambia tena, “Ninaenda zangu, nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi ninyi hamwezi kuja.”
[Jésus] leur dit donc encore: Moi, je m’en vais, et vous me chercherez; et vous mourrez dans votre péché: là où moi je vais, vous, vous ne pouvez venir.
22 Ndipo wale Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Je, hii ndiyo sababu amesema, ‘Niendako mimi ninyi hamwezi kuja’?”
Les Juifs donc disaient: Se tuera-t-il, qu’il dise: Là où moi je vais, vous, vous ne pouvez venir?
23 Akawaambia, “Ninyi mmetoka chini, mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
Et il leur dit: Vous êtes d’en bas; moi, je suis d’en haut: vous êtes de ce monde; moi, je ne suis pas de ce monde.
24 Niliwaambia kuwa mtakufa katika dhambi zenu, kwa maana msipoamini ya kwamba ‘Mimi Ndiye,’ mtakufa katika dhambi zenu.”
Je vous ai donc dit que vous mourrez dans vos péchés; car si vous ne croyez pas que c’est moi, vous mourrez dans vos péchés.
25 Wakamuuliza, “Wewe ni nani?” Naye Yesu akawajibu, “Mimi ndiye yule ambaye nimekuwa nikiwaambia tangu mwanzo.
Ils lui disaient donc: Toi, qui es-tu? Et Jésus leur dit: Absolument ce qu’aussi je vous dis.
26 Nina mambo mengi ya kusema juu yenu na mengi ya kuwahukumu. Lakini yeye aliyenituma ni wa kweli, nami nanena na ulimwengu niliyoyasikia kutoka kwake.”
J’ai beaucoup de choses à dire de vous et à juger; mais celui qui m’a envoyé est vrai, et les choses que j’ai entendues de lui, moi, je les dis au monde.
27 Hawakuelewa kuwa alikuwa akiwaambia juu ya Baba yake wa Mbinguni.
Ils ne connurent pas qu’il leur parlait du Père.
28 Kisha Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha kumwinua juu Mwana wa Adamu, ndipo mtakapojua kuwa, ‘Mimi ndiye yule niliyesema na kwamba mimi sitendi jambo lolote peke yangu bali ninasema yale tu ambayo Baba yangu amenifundisha.
Jésus donc leur dit: Quand vous aurez élevé le fils de l’homme, alors vous connaîtrez que c’est moi, et que je ne fais rien de moi-même, mais que, selon que le Père m’a enseigné, je dis ces choses.
29 Yeye aliyenituma yu pamoja nami, hajaniacha, kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.’”
Et celui qui m’a envoyé est avec moi; il ne m’a pas laissé seul, parce que moi, je fais toujours les choses qui lui plaisent.
30 Wengi waliomsikia Yesu akisema maneno haya wakamwamini.
Comme il disait ces choses, plusieurs crurent en lui.
31 Kisha Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkidumu katika maneno yangu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli.
Jésus donc dit aux Juifs qui avaient cru en lui: Si vous persévérez dans ma parole, vous êtes vraiment mes disciples;
32 Ndipo mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.”
et vous connaîtrez la vérité, et la vérité vous affranchira.
33 Wao wakamjibu, “Sisi tu wazao wa Abrahamu, nasi hatujawa watumwa wa mtu yeyote. Wawezaje kusema kwamba tutawekwa huru?”
Ils lui répondirent: Nous sommes la postérité d’Abraham, et jamais nous n’avons été dans la servitude de personne; comment dis-tu, toi: Vous serez rendus libres?
34 Yesu akajibu, “Amin, amin nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
Jésus leur répondit: En vérité, en vérité, je vous dis: Quiconque pratique le péché est esclave du péché.
35 Mtumwa hakai nyumbani anakotumika siku zote, lakini mwana hukaa nyumbani daima. (aiōn )
Or l’esclave ne demeure pas dans la maison pour toujours; le fils y demeure pour toujours. (aiōn )
36 Hivyo Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
Si donc le Fils vous affranchit, vous serez réellement libres.
37 Ninajua ya kuwa ninyi ni wazao wa Abrahamu, lakini mnatafuta wasaa wa kuniua kwa sababu ndani yenu hamna nafasi ya neno langu.
Je sais que vous êtes la postérité d’Abraham; mais vous cherchez à me faire mourir, parce que ma parole n’a pas d’entrée auprès de vous.
38 Ninasema yale niliyoyaona mbele za Baba yangu, nanyi inawapa kufanya yale mliyosikia kutoka kwa baba yenu.”
Moi, je dis ce que j’ai vu chez mon Père; vous aussi donc, vous faites les choses que vous avez entendues de la part de votre père.
39 Wakajibu, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, “Kama mngekuwa wazao wa Abrahamu mngefanya mambo yale aliyofanya Abrahamu.
Ils répondirent et lui dirent: Abraham est notre père. Jésus leur dit: Si vous étiez enfants d’Abraham, vous feriez les œuvres d’Abraham;
40 Lakini sasa ninyi mnatafuta kuniua, mtu ambaye nimewaambia kweli ile niliyosikia kutoka kwa Mungu, Abrahamu hakufanya jambo la namna hii.
mais maintenant vous cherchez à me faire mourir, moi, un homme qui vous ai dit la vérité que j’ai entendue de Dieu: Abraham n’a pas fait cela.
41 Ninyi mnafanya mambo afanyayo baba yenu.” Wakamjibu, “Sisi hatukuzaliwa kwa uzinzi. Tunaye Baba mmoja, Mungu pekee.”
Vous, vous faites les œuvres de votre père. Ils lui dirent donc: Nous ne sommes pas nés de la fornication; nous avons un père, Dieu.
42 Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
Jésus leur dit: Si Dieu était votre père, vous m’aimeriez, car moi je procède de Dieu et je viens de lui; car je ne suis pas venu de moi-même, mais c’est lui qui m’a envoyé.
43 Kwa nini hamwelewi ninayowaambia? Ni kwa sababu hamwezi kusikia nisemacho.
Pourquoi n’entendez-vous pas mon langage? Parce que vous ne pouvez pas entendre ma parole.
44 Ninyi ni watoto wa baba yenu ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli maana hamna kweli ndani yake. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo.
Vous, vous avez pour père le diable, et vous voulez faire les convoitises de votre père. Lui a été meurtrier dès le commencement, et il n’a pas persévéré dans la vérité, car il n’y a pas de vérité en lui. Quand il profère le mensonge, il parle de son propre fonds, car il est menteur, et le père du mensonge.
45 Lakini kwa sababu nimewaambia kweli hamkuniamini!
Mais moi, parce que je dis la vérité, vous ne me croyez pas.
46 Je, kuna yeyote miongoni mwenu awezaye kunithibitisha kuwa mwenye dhambi? Kama nawaambia yaliyo kweli, mbona hamniamini?
Qui d’entre vous me convainc de péché? Si je dis la vérité, vous, pourquoi ne me croyez-vous pas?
47 Yeye atokaye kwa Mungu husikia kile Mungu asemacho. Sababu ya ninyi kutosikia ni kwa kuwa hamtokani na Mungu.”
Celui qui est de Dieu entend les paroles de Dieu; c’est pourquoi vous, vous n’entendez pas, parce que vous n’êtes pas de Dieu.
48 Wayahudi wakamjibu Yesu, “Je, hatuko sahihi tunaposema ya kwamba wewe ni Msamaria na ya kwamba una pepo mchafu?”
Les Juifs répondirent et lui dirent: Ne disons-nous pas bien que tu es un Samaritain, et que tu as un démon?
49 Yesu akawajibu, “Mimi sina pepo mchafu, bali ninamheshimu Baba yangu, nanyi mnanidharau.
Jésus répondit: Moi, je n’ai point un démon, mais j’honore mon Père, et vous, vous jetez du déshonneur sur moi.
50 Lakini mimi sitafuti utukufu wangu mwenyewe, bali yuko anayetaka kunitukuza, naye ndiye mwamuzi.
Mais pour moi, je ne cherche pas ma gloire; il y en a un qui cherche, et qui juge.
51 Amin, amin nawaambia, mtu yeyote akilitii neno langu hataona mauti milele.” (aiōn )
En vérité, en vérité, je vous dis: Si quelqu’un garde ma parole, il ne verra point la mort, à jamais. (aiōn )
52 Ndipo Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kwamba una pepo mchafu. Ikiwa Abrahamu alikufa na vivyo hivyo manabii, nawe unasema ‘Mtu akitii neno langu hatakufa milele.’ (aiōn )
Les Juifs donc lui dirent: Maintenant nous connaissons que tu as un démon: Abraham est mort, et les prophètes, et toi, tu dis: Si quelqu’un garde ma parole, il ne goûtera point la mort, à jamais. (aiōn )
53 Je, wewe ni mkuu kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa na manabii ambao nao pia walikufa? Hivi wewe unajifanya kuwa nani?”
Es-tu plus grand que notre père Abraham, qui est mort? et les prophètes sont morts. Qui te fais-tu toi-même?
54 Yesu akawajibu, “Kama nikijitukuza utukufu wangu hauna maana. Baba yangu, huyo ambaye ninyi mnadai kuwa ni Mungu wenu, ndiye anitukuzaye mimi.
Jésus répondit: Si moi je me glorifie moi-même, ma gloire n’est rien; c’est mon Père qui me glorifie, lui de qui vous dites: Il est notre Dieu.
55 Ingawa hamkumjua, mimi ninamjua. Kama ningesema simjui, ningekuwa mwongo kama ninyi, lakini mimi ninamjua na ninalitii neno lake.
Et vous ne le connaissez pas; mais moi, je le connais: et si je disais que je ne le connais pas, je serais menteur, semblable à vous; mais je le connais, et je garde sa parole.
56 Baba yenu Abrahamu alishangilia kwamba angaliiona siku yangu, naye akaiona na akafurahi.”
Abraham, votre père, a tressailli de joie de ce qu’il verrait mon jour; et il l’a vu, et s’est réjoui.
57 Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza hata miaka hamsini, wewe wasema umemwona Abrahamu?”
Les Juifs donc lui dirent: Tu n’as pas encore 50 ans, et tu as vu Abraham!
58 Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, kabla Abrahamu hajakuwako, ‘Mimi niko.’”
Jésus leur dit: En vérité, en vérité, je vous dis: Avant qu’Abraham fût, je suis.
59 Ndipo wakaokota mawe ili kumpiga, lakini Yesu akajificha, naye akatoka Hekaluni.
Ils prirent donc des pierres pour les jeter contre lui; mais Jésus se cacha et sortit du temple.