< Yohana 8 >
1 Lakini Yesu akaenda katika Mlima wa Mizeituni.
But Jesus went to the Mount of Olives.
2 Alfajiri na mapema Yesu akaja tena Hekaluni, watu wote wakakusanyika, akakaa akaanza kuwafundisha.
Early in the morning he again went to the temple courts. All the people came, and he sat down and taught them.
3 Walimu wa sheria na Mafarisayo wakamleta mwanamke mmoja aliyefumaniwa akizini. Wakamsimamisha katikati ya umati wa watu wote.
Then the scribes and the Pharisees brought him a woman who had been caught in adultery. Making her stand before them all,
4 Wakamwambia Yesu, “Mwalimu, huyu mwanamke amekutwa akizini.
they said to Jesus, testing him, “Teacher, this woman was caught in the very act of committing adultery.
5 Katika sheria, Mose alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake wa namna hii, mpaka wafe. Sasa wewe wasemaje?”
In the law, Moses commanded us that such women should be stoned; what then do yoʋ say?”
6 Walimuuliza swali hili kama mtego ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Yesu akainama akaanza kuandika ardhini kwa kidole chake.
(They said this to test him, so that they might have something to accuse him of.) But Jesus stooped down and wrote with his finger on the ground, taking no notice.
7 Walipoendelea kumuulizauliza akainuka, akawaambia, “Kama kuna mtu yeyote miongoni mwenu ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe.”
When they continued asking him, he stood up and said to them, “Let him among you who is without sin throw the first stone at her.”
8 Akainama tena na kuandika ardhini.
And again he stooped down and wrote on the ground.
9 Waliposikia haya, wakaanza kuondoka mmoja mmoja, wakianzia wazee, hadi Yesu akabaki peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake.
When they heard this, they were convicted by their own consciences and began to go away one by one, starting with the older men. So Jesus was left alone, with the woman there before him.
10 Yesu akainuka na kumwambia, “Wako wapi wale waliokuwa wanakuhukumu kuwa mwenye hatia?”
Then Jesus stood up and saw no one but the woman. So he said to her, “Where are yoʋr accusers? Has no one condemned yoʋ?”
11 Yule mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akamwambia, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda zako, kuanzia sasa usitende dhambi tena.”]
She said, “No one, Lord.” Jesus said, “Neither do I pass judgment on yoʋ; go and sin no more.”
12 Kisha Yesu akasema nao tena akawaambia, “Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”
Then Jesus spoke to them again, saying, “I am the light of the world. Whoever follows me will certainly not walk in darkness, but will have the light of life.”
13 Mafarisayo wakamwambia, “Ushuhuda wako haukubaliki kwa kuwa unajishuhudia mwenyewe.”
So the Pharisees said to him, “Yoʋ are testifying about yoʋrself, so yoʋr testimony is not valid.”
14 Yesu akawajibu, “Hata kama najishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli kwa sababu najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
Jesus answered them, “Even if I testify about myself, my testimony is valid, for I know where I came from and where I am going, but you do not know where I come from or where I am going.
15 Ninyi mnahukumu kwa kufuata vipimo vya kibinadamu, mimi simhukumu mtu yeyote.
You judge according to the flesh, but I judge no one.
16 Lakini hata kama nikihukumu, uamuzi wangu ni sahihi kwa sababu sitoi hukumu yangu peke yangu, bali niko pamoja na Baba, aliyenituma.
Yet even if I do judge, my judgment is valid; for I am not alone, but I am with the Father who sent me.
17 Imeandikwa katika Sheria yenu kwamba, ushahidi wa watu wawili ni thabiti.
In your own law it is written that the testimony of two men is valid.
18 Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma hunishuhudia.”
I testify about myself, and the Father who sent me also testifies about me.”
19 Ndipo wakamuuliza, “Huyo Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu, “Ninyi hamnifahamu mimi ni nani, wala hammfahamu Baba yangu. Kama mngenifahamu mimi, mngemfahamu na Baba yangu.”
Then they said to him, “Where is yoʋr father?” Jesus answered, “You neither know me nor my Father. If you knew me, you would know my Father as well.”
20 Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika chumba cha hazina Hekaluni. Lakini hakuna mtu aliyemkamata kwa kuwa saa yake ilikuwa haijawadia.
(Jesus spoke these words in the treasury as he taught in the temple courts. But no one arrested him, because his hour had not yet come.)
21 Yesu akawaambia tena, “Ninaenda zangu, nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi ninyi hamwezi kuja.”
Then Jesus said to them again, “I am going away, and you will seek me, but you will die in your sin. Where I am going, you cannot come.”
22 Ndipo wale Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Je, hii ndiyo sababu amesema, ‘Niendako mimi ninyi hamwezi kuja’?”
So the Jews said, “Is he going to kill himself? Is that what he means by saying, ‘Where I am going, you cannot come’?”
23 Akawaambia, “Ninyi mmetoka chini, mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
He said to them, “You are from below; I am from above. You are of this world; I am not of this world.
24 Niliwaambia kuwa mtakufa katika dhambi zenu, kwa maana msipoamini ya kwamba ‘Mimi Ndiye,’ mtakufa katika dhambi zenu.”
Therefore I said to you that you will die in your sins, for if you do not believe that I am he, you will die in your sins.”
25 Wakamuuliza, “Wewe ni nani?” Naye Yesu akawajibu, “Mimi ndiye yule ambaye nimekuwa nikiwaambia tangu mwanzo.
They said to him, “Who are yoʋ?” Jesus said to them, “Exactly what I have been saying to you from the beginning.
26 Nina mambo mengi ya kusema juu yenu na mengi ya kuwahukumu. Lakini yeye aliyenituma ni wa kweli, nami nanena na ulimwengu niliyoyasikia kutoka kwake.”
I have many things to say about you and to judge, but he who sent me is true, and I tell the world what I have heard from him.”
27 Hawakuelewa kuwa alikuwa akiwaambia juu ya Baba yake wa Mbinguni.
(They did not know that he was speaking to them about the Father.)
28 Kisha Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha kumwinua juu Mwana wa Adamu, ndipo mtakapojua kuwa, ‘Mimi ndiye yule niliyesema na kwamba mimi sitendi jambo lolote peke yangu bali ninasema yale tu ambayo Baba yangu amenifundisha.
So Jesus said to them, “When you lift up the Son of Man, then you will know that I am he and that I do nothing on my own authority, but I speak these things just as my Father taught me.
29 Yeye aliyenituma yu pamoja nami, hajaniacha, kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.’”
He who sent me is with me. The Father has not left me alone, for I always do what pleases him.”
30 Wengi waliomsikia Yesu akisema maneno haya wakamwamini.
As he was saying these things, many believed in him.
31 Kisha Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkidumu katika maneno yangu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli.
Then Jesus said to the Jews who had believed in him, “If you abide in my word, you are truly my disciples.
32 Ndipo mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.”
Then you will know the truth, and the truth will set you free.”
33 Wao wakamjibu, “Sisi tu wazao wa Abrahamu, nasi hatujawa watumwa wa mtu yeyote. Wawezaje kusema kwamba tutawekwa huru?”
They answered him, “We are descendants of Abraham, and we have never been enslaved to anyone. How then can yoʋ say, ‘You will be set free’?”
34 Yesu akajibu, “Amin, amin nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
Jesus answered them, “Truly, truly, I say to you, everyone who commits sin is a slave of sin.
35 Mtumwa hakai nyumbani anakotumika siku zote, lakini mwana hukaa nyumbani daima. (aiōn )
The slave does not abide in the house forever; the son abides forever. (aiōn )
36 Hivyo Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
So if the son sets you free, you will be free indeed.
37 Ninajua ya kuwa ninyi ni wazao wa Abrahamu, lakini mnatafuta wasaa wa kuniua kwa sababu ndani yenu hamna nafasi ya neno langu.
I know that you are Abraham's descendants, but you are seeking to kill me because your hearts have no room for my word.
38 Ninasema yale niliyoyaona mbele za Baba yangu, nanyi inawapa kufanya yale mliyosikia kutoka kwa baba yenu.”
I speak of what I have seen with my Father; so you also are doing what you have seen with your father.”
39 Wakajibu, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, “Kama mngekuwa wazao wa Abrahamu mngefanya mambo yale aliyofanya Abrahamu.
They answered him, “Our father is Abraham.” Jesus said to them, “If you were children of Abraham, you would be doing the works of Abraham.
40 Lakini sasa ninyi mnatafuta kuniua, mtu ambaye nimewaambia kweli ile niliyosikia kutoka kwa Mungu, Abrahamu hakufanya jambo la namna hii.
But now you are seeking to kill me, a man who has spoken to you the truth I heard from God. Abraham did not do such a thing.
41 Ninyi mnafanya mambo afanyayo baba yenu.” Wakamjibu, “Sisi hatukuzaliwa kwa uzinzi. Tunaye Baba mmoja, Mungu pekee.”
You are doing the works of your father.” They said to him, “We were not born of fornication. We have one Father—God.”
42 Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
Jesus said to them, “If God were your Father, you would love me, for I have come here from God. I have not come of my own accord, but he sent me.
43 Kwa nini hamwelewi ninayowaambia? Ni kwa sababu hamwezi kusikia nisemacho.
Why do you not understand what I am saying? It is because you cannot bear to accept my word.
44 Ninyi ni watoto wa baba yenu ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli maana hamna kweli ndani yake. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo.
You belong to your father the devil, and you want to carry out your father's desires. He was a murderer from the beginning and does not stand in the truth, because there is no truth in him. When he speaks lies, he speaks from his own character, because he is a liar and the father of lies.
45 Lakini kwa sababu nimewaambia kweli hamkuniamini!
But because I speak the truth, you do not believe me.
46 Je, kuna yeyote miongoni mwenu awezaye kunithibitisha kuwa mwenye dhambi? Kama nawaambia yaliyo kweli, mbona hamniamini?
Which one of you convicts me of sin? If I am telling the truth, why do you not believe me?
47 Yeye atokaye kwa Mungu husikia kile Mungu asemacho. Sababu ya ninyi kutosikia ni kwa kuwa hamtokani na Mungu.”
Whoever belongs to God hears the words of God. The reason you do not hear them is because you do not belong to God.”
48 Wayahudi wakamjibu Yesu, “Je, hatuko sahihi tunaposema ya kwamba wewe ni Msamaria na ya kwamba una pepo mchafu?”
The Jews answered him, “Do we not rightly say that yoʋ are a Samaritan and have a demon?”
49 Yesu akawajibu, “Mimi sina pepo mchafu, bali ninamheshimu Baba yangu, nanyi mnanidharau.
Jesus answered, “I do not have a demon, but I honor my Father, and you dishonor me.
50 Lakini mimi sitafuti utukufu wangu mwenyewe, bali yuko anayetaka kunitukuza, naye ndiye mwamuzi.
I do not seek my own glory; there is one who seeks it, and he is the judge.
51 Amin, amin nawaambia, mtu yeyote akilitii neno langu hataona mauti milele.” (aiōn )
Truly, truly, I say to you, if anyone keeps my word, he will certainly never see death.” (aiōn )
52 Ndipo Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kwamba una pepo mchafu. Ikiwa Abrahamu alikufa na vivyo hivyo manabii, nawe unasema ‘Mtu akitii neno langu hatakufa milele.’ (aiōn )
The Jews said to him, “Now we know that yoʋ have a demon. Abraham died, and so did the prophets, yet yoʋ say, ‘If anyone keeps my word, he will certainly never taste death.’ (aiōn )
53 Je, wewe ni mkuu kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa na manabii ambao nao pia walikufa? Hivi wewe unajifanya kuwa nani?”
Are yoʋ greater than our father Abraham, who died? The prophets also died. Who do yoʋ make yoʋrself out to be?”
54 Yesu akawajibu, “Kama nikijitukuza utukufu wangu hauna maana. Baba yangu, huyo ambaye ninyi mnadai kuwa ni Mungu wenu, ndiye anitukuzaye mimi.
Jesus answered, “If I glorify myself, my glory is nothing. It is my Father who glorifies me, of whom you say, ‘He is our God.’
55 Ingawa hamkumjua, mimi ninamjua. Kama ningesema simjui, ningekuwa mwongo kama ninyi, lakini mimi ninamjua na ninalitii neno lake.
You do not know him, but I know him. If I were to say that I do not know him, I would be a liar like you. But I do know him, and I keep his word.
56 Baba yenu Abrahamu alishangilia kwamba angaliiona siku yangu, naye akaiona na akafurahi.”
Your father Abraham was glad that he would see my day. He saw it and rejoiced.”
57 Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza hata miaka hamsini, wewe wasema umemwona Abrahamu?”
Then the Jews said to him, “Yoʋ are not yet fifty years old, and yoʋ have seen Abraham?”
58 Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, kabla Abrahamu hajakuwako, ‘Mimi niko.’”
Jesus said to them, “Truly, truly, I say to you, before Abraham was, I am.”
59 Ndipo wakaokota mawe ili kumpiga, lakini Yesu akajificha, naye akatoka Hekaluni.
So they picked up stones to throw at him, but Jesus hid himself and went out from the temple grounds. And passing through the crowd, he walked away.