< Yohana 8 >
1 Lakini Yesu akaenda katika Mlima wa Mizeituni.
Jesus went to the Mount of Olives.
2 Alfajiri na mapema Yesu akaja tena Hekaluni, watu wote wakakusanyika, akakaa akaanza kuwafundisha.
At dawn, however, he came back to the Temple, where the people came to him in crowds. He had taken his seat and was teaching them,
3 Walimu wa sheria na Mafarisayo wakamleta mwanamke mmoja aliyefumaniwa akizini. Wakamsimamisha katikati ya umati wa watu wote.
when the Scribes and Pharisees had brought a woman who had been caught in the act of adultery. They made her stand in the middle of the court, and said to him.
4 Wakamwambia Yesu, “Mwalimu, huyu mwanamke amekutwa akizini.
"Rabbi, this woman has been found in the very act of adultery.
5 Katika sheria, Mose alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake wa namna hii, mpaka wafe. Sasa wewe wasemaje?”
"Now Moses, in the Law, has commanded us to stone such creatures. But you, what do you say?"
6 Walimuuliza swali hili kama mtego ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Yesu akainama akaanza kuandika ardhini kwa kidole chake.
(This they said to tempt him, so that they could bring a charge against him.)
7 Walipoendelea kumuulizauliza akainuka, akawaambia, “Kama kuna mtu yeyote miongoni mwenu ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe.”
But Jesus stooped down, and began to write on the ground with his finger. When they continued to question him, he raised himself and said to them, "Let the innocent man among you be the first to throw the stone at her."
8 Akainama tena na kuandika ardhini.
Then he stooped down again, and again began to write on the ground.
9 Waliposikia haya, wakaanza kuondoka mmoja mmoja, wakianzia wazee, hadi Yesu akabaki peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake.
When they heard that, they went out one by one, beginning with the eldest. And Jesus was left behind alone - and the woman in the middle of the court.
10 Yesu akainuka na kumwambia, “Wako wapi wale waliokuwa wanakuhukumu kuwa mwenye hatia?”
Then Jesus raised himself up and said to her. "Woman, where are they? Has no man condemn you,"
11 Yule mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akamwambia, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda zako, kuanzia sasa usitende dhambi tena.”]
"No one, Sir," she answered. "Neither do I condemned you," said Jesus. "Go, and never sin again."
12 Kisha Yesu akasema nao tena akawaambia, “Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”
Once more Jesus addressed them. "I am the light of the world," he said; "He who follows me shall not walk in the darkness, but he shall have the Light of life."
13 Mafarisayo wakamwambia, “Ushuhuda wako haukubaliki kwa kuwa unajishuhudia mwenyewe.”
Then said the Pharisees to him. "You are bearing testimony to yourself; your testimony is not true."
14 Yesu akawajibu, “Hata kama najishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli kwa sababu najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
In reply Jesus said to them. "Even if I do bear testimony to concerning myself, my testimony is true, because I know where I have come from and where I am going. But you do not know where I have come from, or where I am going.
15 Ninyi mnahukumu kwa kufuata vipimo vya kibinadamu, mimi simhukumu mtu yeyote.
"For you are judging according to the flesh. I am judging no man.
16 Lakini hata kama nikihukumu, uamuzi wangu ni sahihi kwa sababu sitoi hukumu yangu peke yangu, bali niko pamoja na Baba, aliyenituma.
"Though even if I do judge, my judgment is trustworthy, because I am not alone, but the Father who sent me is with me.
17 Imeandikwa katika Sheria yenu kwamba, ushahidi wa watu wawili ni thabiti.
"And in your Law it is written that the testimony of two men is true.
18 Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma hunishuhudia.”
"I am one who gives testimony concerning myself, and the Father who sent me gives testimony concerning me."
19 Ndipo wakamuuliza, “Huyo Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu, “Ninyi hamnifahamu mimi ni nani, wala hammfahamu Baba yangu. Kama mngenifahamu mimi, mngemfahamu na Baba yangu.”
"Where is your Father?" they asked him. "You have neither known me nor my Father," answered Jesus. "If you had known me, you would have known my father also."
20 Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika chumba cha hazina Hekaluni. Lakini hakuna mtu aliyemkamata kwa kuwa saa yake ilikuwa haijawadia.
He said these words in the Treasury, while he was teaching in the Temple; yet no one arrested him, because his hour was not yet come.
21 Yesu akawaambia tena, “Ninaenda zangu, nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi ninyi hamwezi kuja.”
Then again he said them. "I am going away, and you will seek me, and you will die in your sins. Where I am going, you cannot come."
22 Ndipo wale Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Je, hii ndiyo sababu amesema, ‘Niendako mimi ninyi hamwezi kuja’?”
Then the Jews said. "He will not kill himself, will he? Is that why he says, ‘Where I am going you cannot come’?"
23 Akawaambia, “Ninyi mmetoka chini, mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
And he said to them. "You are from below. I am from above; you are of this world, I am not of this world.
24 Niliwaambia kuwa mtakufa katika dhambi zenu, kwa maana msipoamini ya kwamba ‘Mimi Ndiye,’ mtakufa katika dhambi zenu.”
"That is why I said that you would die in your sins. For if you do not believe that I am He, you will die in your sins."
25 Wakamuuliza, “Wewe ni nani?” Naye Yesu akawajibu, “Mimi ndiye yule ambaye nimekuwa nikiwaambia tangu mwanzo.
"Who are you?" then they asked him. "What I am telling you from the beginning," Jesus answered.
26 Nina mambo mengi ya kusema juu yenu na mengi ya kuwahukumu. Lakini yeye aliyenituma ni wa kweli, nami nanena na ulimwengu niliyoyasikia kutoka kwake.”
"I have many things to say and to judge concerning you. But he who sent me is true, and I speak to the world only those things which I have heard from him."
27 Hawakuelewa kuwa alikuwa akiwaambia juu ya Baba yake wa Mbinguni.
They did not understand that he meant the Father,
28 Kisha Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha kumwinua juu Mwana wa Adamu, ndipo mtakapojua kuwa, ‘Mimi ndiye yule niliyesema na kwamba mimi sitendi jambo lolote peke yangu bali ninasema yale tu ambayo Baba yangu amenifundisha.
so Jesus added. "When you lifted up the Son of man, then you will know that I am He; and that I do nothing on my own authority, but that I speak just as the Father has taught me,
29 Yeye aliyenituma yu pamoja nami, hajaniacha, kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.’”
"and he who sent me is with me. He has not left me alone, for I do always the things that please him."
30 Wengi waliomsikia Yesu akisema maneno haya wakamwamini.
When he spoke in this way, many of the Jews believed in him.
31 Kisha Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkidumu katika maneno yangu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli.
So Jesus spoke to the Jews that believed him, saying. "If you abide in my teaching, you are my true disciples;
32 Ndipo mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.”
"and you shall know the truth, and the truth will make you free."
33 Wao wakamjibu, “Sisi tu wazao wa Abrahamu, nasi hatujawa watumwa wa mtu yeyote. Wawezaje kusema kwamba tutawekwa huru?”
"We are descendants of Abraham," they replied, "and have never been in slavery to any man. What do you mean by saying, ‘You shall become free’?"
34 Yesu akajibu, “Amin, amin nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
"In solemn truth I tell you," Jesus replied, "every one who commits sin is a slave
35 Mtumwa hakai nyumbani anakotumika siku zote, lakini mwana hukaa nyumbani daima. (aiōn )
"Now the slave does not remain permanently in the household, but the son does remain. (aiōn )
36 Hivyo Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
"So then, if the Son shall set you free, you will be free indeed.
37 Ninajua ya kuwa ninyi ni wazao wa Abrahamu, lakini mnatafuta wasaa wa kuniua kwa sababu ndani yenu hamna nafasi ya neno langu.
"I know you are Abraham’s descendants; but you are seeking to kill me, Because my teaching has no place in you.
38 Ninasema yale niliyoyaona mbele za Baba yangu, nanyi inawapa kufanya yale mliyosikia kutoka kwa baba yenu.”
"I am declaring what I have seen with the Father, and you are acting as you have learned from your father."
39 Wakajibu, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, “Kama mngekuwa wazao wa Abrahamu mngefanya mambo yale aliyofanya Abrahamu.
"Abraham is our father," they answered. "If you are indeed Abraham’s children," said Jesus "do the deeds of Abraham.
40 Lakini sasa ninyi mnatafuta kuniua, mtu ambaye nimewaambia kweli ile niliyosikia kutoka kwa Mungu, Abrahamu hakufanya jambo la namna hii.
"But now you are seeking to kill me - a man who has told you the truth which I heard from God. Abraham did not do that.
41 Ninyi mnafanya mambo afanyayo baba yenu.” Wakamjibu, “Sisi hatukuzaliwa kwa uzinzi. Tunaye Baba mmoja, Mungu pekee.”
"You are doing the deeds of your father." "We were not born of adultery," they said; "we have one Father, God."
42 Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
Jesus said to them. "If God were your Father, you would love me, for I proceeded forth and am now come from God. I did not come on my own authority, but God himself sent me.
43 Kwa nini hamwelewi ninayowaambia? Ni kwa sababu hamwezi kusikia nisemacho.
"How is it that you do not understand what I say? It is because you cannot listen to my message.
44 Ninyi ni watoto wa baba yenu ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli maana hamna kweli ndani yake. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo.
"You are of your father, the devil, and you want to do what your father desires. He was a man-slayer from the very beginning; and he has no standing place in the truth, because truth is not in him. Whenever he utters a lie, he speaks from his nature, for he is a liar and the father of lying.
45 Lakini kwa sababu nimewaambia kweli hamkuniamini!
"But as for me, it is because I speak the truth to you that you do not believe me.
46 Je, kuna yeyote miongoni mwenu awezaye kunithibitisha kuwa mwenye dhambi? Kama nawaambia yaliyo kweli, mbona hamniamini?
"Which one of you convicts me of sin? Why then, if I am speaking the truth, do you not believe me?
47 Yeye atokaye kwa Mungu husikia kile Mungu asemacho. Sababu ya ninyi kutosikia ni kwa kuwa hamtokani na Mungu.”
"He who is from God listens to God’s words. For this reason you do not listen, because you are not from God."
48 Wayahudi wakamjibu Yesu, “Je, hatuko sahihi tunaposema ya kwamba wewe ni Msamaria na ya kwamba una pepo mchafu?”
In reply the Jews said to him, "Are we not right in saying that you are a Samaritan, and you also have a demon?"
49 Yesu akawajibu, “Mimi sina pepo mchafu, bali ninamheshimu Baba yangu, nanyi mnanidharau.
"I do not have a demon," said Jesus, "but I am honoring my Father, and you are dishonoring me.
50 Lakini mimi sitafuti utukufu wangu mwenyewe, bali yuko anayetaka kunitukuza, naye ndiye mwamuzi.
"Yet I am not seeking my own honor. There is One who is seeking it, and He is judge.
51 Amin, amin nawaambia, mtu yeyote akilitii neno langu hataona mauti milele.” (aiōn )
"In solemn truth I tell you that if any one obeys my teaching he shall never behold death." (aiōn )
52 Ndipo Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kwamba una pepo mchafu. Ikiwa Abrahamu alikufa na vivyo hivyo manabii, nawe unasema ‘Mtu akitii neno langu hatakufa milele.’ (aiōn )
"Now we know that you have a demon," exclaimed the Jews. Abraham died, and so did the prophets; and yet you say, ‘If any man obeys my teaching he shall never taste death.’ (aiōn )
53 Je, wewe ni mkuu kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa na manabii ambao nao pia walikufa? Hivi wewe unajifanya kuwa nani?”
"You are not greater than our father Abraham, are you? And he died, and the prophets died. Who are you making yourself out to be?"
54 Yesu akawajibu, “Kama nikijitukuza utukufu wangu hauna maana. Baba yangu, huyo ambaye ninyi mnadai kuwa ni Mungu wenu, ndiye anitukuzaye mimi.
"If I glorify myself." said Jesus, "my glory is nothing. It is my Father that glorifies me, and you say, ‘He is our God.’
55 Ingawa hamkumjua, mimi ninamjua. Kama ningesema simjui, ningekuwa mwongo kama ninyi, lakini mimi ninamjua na ninalitii neno lake.
"You are not acquainted with him; I know him. Were I to say, ‘I do not know him,’ I should be like you, a liar. But I do know him, and I obey his teaching.
56 Baba yenu Abrahamu alishangilia kwamba angaliiona siku yangu, naye akaiona na akafurahi.”
"Your father Abraham rejoiced that he should see my day; and he saw it and was glad."
57 Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza hata miaka hamsini, wewe wasema umemwona Abrahamu?”
"You are not yet fifty years old," said the Jews to him, "and you have seen Abraham?"
58 Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, kabla Abrahamu hajakuwako, ‘Mimi niko.’”
"In solemn truth I tell you," answered Jesus, "that before Abraham came into existence, I am."
59 Ndipo wakaokota mawe ili kumpiga, lakini Yesu akajificha, naye akatoka Hekaluni.
Then they picked up stones to throw at him, but Jesus hid himself and went out of the Temple.