< Yohana 7 >

1 Baada ya mambo haya, Yesu alikwenda sehemu mbalimbali za Galilaya. Hakutaka kwenda Uyahudi kwa sababu Wayahudi huko walitaka kumuua.
Después de esto, Jesús andaba en Galilea, porque no quería andar en Judea, pues los judíos lo buscaban para matar[lo].
2 Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
Se acercaba El Tabernáculo, la fiesta de los judíos,
3 Hivyo ndugu zake Yesu wakamwambia, “Ondoka hapa uende Uyahudi ili wanafunzi Wako wapate kuona miujiza unayofanya.
y sus hermanos le dijeron: Sal de aquí y vé a Judea para que también tus discípulos vean las obras que haces.
4 Mtu anayetaka kujulikana hafanyi mambo yake kwa siri. Kama unafanya mambo haya, jionyeshe kwa ulimwengu.”
Porque el que quiere darse a [conocer] no actúa en secreto. Puesto que haces estas cosas, manifiéstate al mundo.
5 Hata ndugu zake mwenyewe hawakumwamini.
Porque ni aun sus hermanos creían en Él.
6 Yesu akawaambia, “Wakati wangu bado haujawadia, lakini wakati wenu upo siku zote.
Jesús les dijo: Mi tiempo aún no llegó, aunque para ustedes cualquier tiempo es oportuno.
7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini unanichukia mimi kwa sababu ninawashuhudia kwamba matendo yao ni maovu.
El mundo no puede aborrecerlos, pero a Mí me aborrece porque Yo testifico que sus obras son malas.
8 Ninyi nendeni kwenye Sikukuu, lakini mimi sitahudhuria Sikukuu hii kwa sababu wakati wangu haujawadia.”
Suban ustedes a la fiesta. Yo no subo a esta fiesta, porque mi tiempo aún no se cumplió.
9 Akiisha kusema hayo, akabaki Galilaya.
Dijo esto y se quedó en Galilea.
10 Lakini ndugu zake walipokwisha kuondoka kwenda kwenye Sikukuu, yeye pia alikwenda lakini kwa siri.
Sin embargo, cuando sus hermanos subieron a la fiesta, Él también subió, pero en secreto.
11 Wayahudi walikuwa wakimtafuta huko kwenye Sikukuu na kuulizana, “Yuko wapi huyu mtu?”
Los judíos lo buscaban en la fiesta y preguntaban: ¿Dónde está Aquél?
12 Kulikuwa na minongʼono iliyoenea kumhusu Yesu katika umati wa watu, wakati wengine wakisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walikuwa wakisema, “La, yeye anawadanganya watu.”
Había mucha murmuración entre la gente con respecto a Él, pues unos decían: Es bueno. Otros decían: No, más bien engaña a la gente.
13 Lakini hakuna mtu yeyote aliyemsema waziwazi kumhusu kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi.
Pero nadie hablaba francamente con respecto a Él por temor a los judíos.
14 Ilipokaribia katikati ya Sikukuu, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
En la mitad de la fiesta, Jesús subió al Templo y enseñaba.
15 Wayahudi wakastaajabia mafundisho yake wakasema, “Mtu huyu amepataje kujua mambo haya bila kufundishwa?”
Los judíos decían con asombro: ¿Éste cómo sabe tanto, si no ha estudiado?
16 Ndipo Yesu akawajibu, “Mafundisho yangu si yangu mwenyewe, bali yanatoka kwake yeye aliyenituma.
Entonces Jesús les respondió: Mi enseñanza no es mía, sino de Quien me envió.
17 Mtu yeyote akipenda kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu au ninasema kwa ajili yangu mwenyewe.
Si alguien quiere hacer la voluntad de Dios sabrá si la enseñanza es de Dios, o si Yo hablo de Mí mismo.
18 Wale wanenao kwa ajili yao wenyewe hufanya hivyo kwa kutaka utukufu wao wenyewe. Lakini yeye atafutaye utukufu wa yule aliyemtuma ni wa kweli, wala hakuna uongo ndani yake.
El que habla de él mismo busca su propia fama. Pero el que busca la gloria del que lo envió es veraz y no hay perversidad en Él.
19 Je, Mose hakuwapa ninyi sheria? Lakini hakuna hata mmoja wenu anayeishika hiyo sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”
¿Moisés no les dio la Ley? Pero ninguno de ustedes la cumple. ¿Por qué quieren matarme?
20 Ule umati wa watu ukamjibu, “Wewe una pepo mchafu! Ni nani anayetaka kukuua?”
La gente respondió: ¡Tienes demonio! ¿Quién quiere matarte?
21 Yesu akawajibu, “Nimefanya muujiza mmoja na nyote mkastaajabu.
Jesús respondió: Hice una obra, y todos ustedes están asombrados.
22 Lakini kwa kuwa Mose aliwaamuru tohara (ingawa kwa kweli haikutoka kwa Mose bali kwa baba zenu wakuu), mnamtahiri mtoto hata siku ya Sabato.
Moisés les dio la circuncisión, la cual no es de Moisés sino de los antepasados, y en sábado circuncidan al varón.
23 Ikiwa mtoto aweza kutahiriwa siku ya Sabato kusudi sheria ya Mose isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia kwa kumponya mtu mwili wake wote siku ya Sabato?
Si [el] varón es circuncidado en sábado para no quebrantar la Ley de Moisés, ¿se enojan conmigo porque en sábado sané a todo un hombre?
24 Acheni kuhukumu mambo kwa jinsi mnavyoona tu, bali hukumuni kwa haki.”
No juzguen según [la] apariencia, sino juzguen según [la] justicia.
25 Ndipo baadhi ya watu wa Yerusalemu wakawa wanasema, “Tazameni, huyu si yule mtu wanayetaka kumuua?
Entonces algunos de Jerusalén decían: ¿No es Éste a Quien buscan para matarlo?
26 Mbona yuko hapa anazungumza hadharani na wala hawamwambii neno lolote? Je, inawezekana viongozi wanafahamu kuwa huyu ndiye Kristo?
Miren, habla con libertad, y nada le dicen. ¿Tal vez los gobernantes reconocieron que Éste es verdaderamente el Cristo?
27 Tunafahamu huyu mtu anakotoka, lakini Kristo atakapokuja, hakuna yeyote atakayejua atokako.”
Sabemos de dónde es Éste. Pero cuando venga el Cristo nadie sabrá de dónde es.
28 Ndipo Yesu, akaendelea kufundisha Hekaluni, akisema, “Ninyi mnanifahamu na kujua nitokako. Mimi sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, bali yeye aliyenituma ni wa kweli na ninyi hammjui.
Entonces Jesús, al enseñar en el Templo, exclamó: ¡A Mí me conocen y saben de dónde soy! Pero Yo no vine por iniciativa propia, sino me envió el Verdadero, a Quien ustedes no conocen.
29 Mimi namjua kwa kuwa nimetoka kwake, naye ndiye alinituma.”
Yo lo conozco, porque de Él vengo y Él me envió.
30 Ndipo wakatafuta kumkamata, lakini hakuna mtu yeyote aliyethubutu kumshika kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijawadia.
Entonces procuraban arrestarlo, pero nadie puso la mano sobre Él, porque aún no había llegado su hora.
31 Nao watu wengi wakamwamini, wakasema, “Je, Kristo atakapokuja, atafanya miujiza mikuu zaidi kuliko aliyoifanya mtu huyu?”
Pero muchos de la multitud creyeron en Él y decían: Cuando venga el Cristo, ¿hará más señales que las que Éste ha hecho?
32 Mafarisayo wakasikia watu wakinongʼona mambo kama hayo kuhusu Yesu, ndipo wao pamoja na viongozi wa makuhani wakatuma walinzi wa Hekalu waende kumkamata.
Cuando los fariseos y los principales sacerdotes oyeron los comentarios de la gente acerca de [Jesús] enviaron alguaciles para que lo arrestaran.
33 Yesu akasema, “Mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo, kisha nitarudi kwake yeye aliyenituma.
Entonces Jesús [les] dijo: Aún estoy con ustedes poco tiempo, y regresaré al que me envió.
34 Mtanitafuta lakini hamtaniona, nami niliko ninyi hamwezi kuja.”
Ustedes me buscarán y no [me] hallarán, y a donde Yo esté, ustedes no pueden ir.
35 Wayahudi wakaulizana wao kwa wao, “Huyu mtu anataka kwenda wapi ambako hatuwezi kumfuata? Je, anataka kwenda kwa Wayunani ambako baadhi ya watu wetu wametawanyikia, akawafundishe Wayunani?
Entonces los judíos se dijeron: ¿A dónde se irá Éste, que nosotros no lo hallemos? ¿Se irá a los judíos que están entre los griegos para enseñar a los griegos?
36 Yeye ana maana gani anaposema, ‘Mtanitafuta lakini hamtaniona,’ na, ‘nami niliko ninyi hamwezi kuja’?”
¿Qué quiere decir esta Palabra: Me buscarán y no [me] hallarán, y a donde Yo esté ustedes no pueden ir?
37 Siku ile ya mwisho ya Sikukuu, siku ile kuu, wakati Yesu akiwa amesimama huko, akapaza sauti yake akasema, “Kama mtu yeyote anaona kiu na aje kwangu anywe.
El último día grande de la fiesta Jesús se puso en pie y exclamó: ¡Si alguno tiene sed, venga a Mí y beba!
38 Yeyote aniaminiye mimi, kama Maandiko yasemavyo, vijito vya maji ya uzima vitatiririka ndani mwake.”
De lo más profundo del ser del que cree en Mí, como dice la Escritura, fluirán ríos de agua viva.
39 Yesu aliposema haya alimaanisha Roho Mtakatifu ambaye wote waliomwamini wangempokea, kwani mpaka wakati huo, Roho alikuwa hajatolewa, kwa kuwa Yesu alikuwa bado hajatukuzwa.
Dijo esto con respecto al Espíritu que recibirían los que habían creído en Él, porque aun no se [había concedido] el Espíritu, pues Jesús aún no había sido glorificado.
40 Waliposikia maneno hayo, baadhi ya watu miongoni mwa ule umati wakasema, “Hakika huyu ndiye yule Nabii.”
Cuando oyeron estas Palabras, [algunos] entre la multitud decían: ¡Verdaderamente Éste es el Profeta!
41 Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine wakauliza, “Je, Kristo kwao ni Galilaya?
Otros decían: ¡Éste es el Cristo! Pero otros decían: ¿El Cristo viene de Galilea?
42 Je, Maandiko hayasemi kwamba Kristo atakuja kutoka jamaa ya Daudi na kutoka Bethlehemu, mji alioishi Daudi?”
¿No dice la Escritura que el Cristo viene de la descendencia de David y de Belén, la aldea de David?
43 Kwa hiyo watu wakagawanyika kwa ajili ya Yesu.
Entonces hubo una división entre la gente por causa de Él.
44 Baadhi yao walitaka kumkamata, lakini hakuna aliyethubutu kumgusa.
Algunos querían arrestarlo, pero nadie le puso las manos.
45 Hatimaye wale walinzi wa Hekalu wakarudi kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo waliokuwa wamewatuma ili kumkamata Yesu, wakaulizwa, “Mbona hamkumkamata?”
Así que los alguaciles fueron a los principales sacerdotes y fariseos, y éstos les preguntaron: ¿Por qué no lo trajeron?
46 Wale walinzi wakajibu, “Kamwe hajanena mtu yeyote kama yeye anenavyo.”
Los alguaciles respondieron: ¡Nunca habló así un hombre!
47 Mafarisayo wakajibu, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
Entonces los fariseos les respondieron: ¿Entonces ustedes también fueron engañados?
48 Je, kuna kiongozi yeyote au mmoja wa Mafarisayo ambaye amemwamini?
¿Alguno de los magistrados o de los fariseos creyó en Él?
49 Lakini huu umati wa watu wasiojua Sheria ya Mose, wamelaaniwa.”
Pero esta gente que no conoce la Ley es maldita.
50 Ndipo Nikodemo, yule aliyekuwa amemwendea Yesu siku moja usiku, ambaye alikuwa mmoja wao akauliza,
Nicodemo, quien visitó a Jesús y era uno de ellos, les dijo:
51 “Je, sheria zetu zinaturuhusu kumhukumu mtu kabla ya kumsikiliza na kufahamu alilotenda?”
¿Nuestra Ley juzga al hombre si no lo oye primero y sabe qué hizo?
52 Wakamjibu, “Je, wewe pia unatoka Galilaya? Chunguza nawe utaona kwamba hakuna nabii atokae Galilaya!” [
[Ellos le] respondieron: ¿Tú también eres de Galilea? Investiga y ve que de Galilea no se levanta profeta.
53 Kisha wakaondoka, kila mtu akarudi nyumbani kwake.

< Yohana 7 >