< Yohana 7 >
1 Baada ya mambo haya, Yesu alikwenda sehemu mbalimbali za Galilaya. Hakutaka kwenda Uyahudi kwa sababu Wayahudi huko walitaka kumuua.
Après ces choses, Jésus parcourait la Galilée, car il ne voulait pas demeurer en Judée, parce que les Juifs cherchaient à le faire mourir.
2 Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
Or, la fête des Juifs, appelée des Tabernacles, approchait.
3 Hivyo ndugu zake Yesu wakamwambia, “Ondoka hapa uende Uyahudi ili wanafunzi Wako wapate kuona miujiza unayofanya.
Et ses frères lui dirent: Pars d'ici, et va en Judée, afin que tes disciples voient aussi les ouvres que tu fais.
4 Mtu anayetaka kujulikana hafanyi mambo yake kwa siri. Kama unafanya mambo haya, jionyeshe kwa ulimwengu.”
Car personne ne fait rien en cachette, quand il cherche à être connu. Si tu fais ces choses, montre-toi toi-même au monde.
5 Hata ndugu zake mwenyewe hawakumwamini.
Car ses frères même ne croyaient pas en lui.
6 Yesu akawaambia, “Wakati wangu bado haujawadia, lakini wakati wenu upo siku zote.
Jésus leur dit: Mon temps n'est pas encore venu; mais votre temps est toujours venu.
7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini unanichukia mimi kwa sababu ninawashuhudia kwamba matendo yao ni maovu.
Le monde ne peut vous haïr; mais il me hait, parce que je rends de lui le témoignage que ses ouvres sont mauvaises.
8 Ninyi nendeni kwenye Sikukuu, lakini mimi sitahudhuria Sikukuu hii kwa sababu wakati wangu haujawadia.”
Pour vous, montez à cette fête; pour moi, je n'y monte pas encore, parce que mon temps n'est pas encore venu.
9 Akiisha kusema hayo, akabaki Galilaya.
Et leur ayant dit cela, il demeura en Galilée.
10 Lakini ndugu zake walipokwisha kuondoka kwenda kwenye Sikukuu, yeye pia alikwenda lakini kwa siri.
Mais, lorsque ses frères furent partis, il monta aussi à la fête, non pas publiquement, mais comme en cachette.
11 Wayahudi walikuwa wakimtafuta huko kwenye Sikukuu na kuulizana, “Yuko wapi huyu mtu?”
Les Juifs donc le cherchaient pendant la fête, et disaient: Où est-il?
12 Kulikuwa na minongʼono iliyoenea kumhusu Yesu katika umati wa watu, wakati wengine wakisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walikuwa wakisema, “La, yeye anawadanganya watu.”
Et il y avait une grande rumeur à son sujet parmi le peuple. Les uns disaient: C'est un homme de bien; et les autres disaient: Non, mais il séduit le peuple.
13 Lakini hakuna mtu yeyote aliyemsema waziwazi kumhusu kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi.
Toutefois, personne ne parlait librement de lui, par crainte des Juifs.
14 Ilipokaribia katikati ya Sikukuu, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
Vers le milieu de la fête, Jésus monta au temple, et il enseignait.
15 Wayahudi wakastaajabia mafundisho yake wakasema, “Mtu huyu amepataje kujua mambo haya bila kufundishwa?”
Et les Juifs étaient étonnés, et disaient: Comment cet homme connaît-il les Écritures, ne les ayant point apprises
16 Ndipo Yesu akawajibu, “Mafundisho yangu si yangu mwenyewe, bali yanatoka kwake yeye aliyenituma.
Jésus leur répondit: Ma doctrine n'est pas de moi, mais de celui qui m'a envoyé.
17 Mtu yeyote akipenda kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu au ninasema kwa ajili yangu mwenyewe.
Si quelqu'un veut faire la volonté de Dieu, il connaîtra si ma doctrine est de Dieu, ou si je parle de mon chef.
18 Wale wanenao kwa ajili yao wenyewe hufanya hivyo kwa kutaka utukufu wao wenyewe. Lakini yeye atafutaye utukufu wa yule aliyemtuma ni wa kweli, wala hakuna uongo ndani yake.
Celui qui parle de son chef cherche sa propre gloire; mais celui qui cherche la gloire de celui qui l'a envoyé, est digne de foi, et il n'y a point d'injustice en lui.
19 Je, Mose hakuwapa ninyi sheria? Lakini hakuna hata mmoja wenu anayeishika hiyo sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”
Moïse ne vous a-t-il pas donné la loi? et aucun de vous n'observe la loi. Pourquoi cherchez-vous à me faire mourir?
20 Ule umati wa watu ukamjibu, “Wewe una pepo mchafu! Ni nani anayetaka kukuua?”
Le peuple lui répondit: Tu as un démon; qui est-ce qui cherche à te faire mourir?
21 Yesu akawajibu, “Nimefanya muujiza mmoja na nyote mkastaajabu.
Jésus répondit et leur dit: J'ai fait une ouvre, et vous en êtes tous étonnés.
22 Lakini kwa kuwa Mose aliwaamuru tohara (ingawa kwa kweli haikutoka kwa Mose bali kwa baba zenu wakuu), mnamtahiri mtoto hata siku ya Sabato.
Moïse vous a ordonné la circoncision (non qu'elle vienne de Moïse, mais des pères), et vous circoncisez un homme le jour du sabbat.
23 Ikiwa mtoto aweza kutahiriwa siku ya Sabato kusudi sheria ya Mose isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia kwa kumponya mtu mwili wake wote siku ya Sabato?
Si un homme reçoit la circoncision le jour du sabbat, afin que la loi de Moïse ne soit pas violée, pourquoi vous irritez-vous contre moi, parce que j'ai entièrement guéri un homme le jour du sabbat?
24 Acheni kuhukumu mambo kwa jinsi mnavyoona tu, bali hukumuni kwa haki.”
Ne jugez point selon l'apparence, mais jugez selon la justice.
25 Ndipo baadhi ya watu wa Yerusalemu wakawa wanasema, “Tazameni, huyu si yule mtu wanayetaka kumuua?
Et quelques-uns de ceux de Jérusalem disaient: N'est-ce pas celui qu'on cherche à faire mourir?
26 Mbona yuko hapa anazungumza hadharani na wala hawamwambii neno lolote? Je, inawezekana viongozi wanafahamu kuwa huyu ndiye Kristo?
Et le voilà qui parle librement, et on ne lui dit rien. Les chefs auraient-ils vraiment reconnu qu'il est véritablement le Christ?
27 Tunafahamu huyu mtu anakotoka, lakini Kristo atakapokuja, hakuna yeyote atakayejua atokako.”
Cependant nous savons d'où il est; au lieu que, quand le Christ viendra, personne ne saura d'où il est.
28 Ndipo Yesu, akaendelea kufundisha Hekaluni, akisema, “Ninyi mnanifahamu na kujua nitokako. Mimi sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, bali yeye aliyenituma ni wa kweli na ninyi hammjui.
Et Jésus s'écriait donc dans le temple, enseignant, et disant: Vous me connaissez, et vous savez d'où je suis. Je ne suis pas venu de moi-même, mais celui qui m'a envoyé est véritable, et vous ne le connaissez point.
29 Mimi namjua kwa kuwa nimetoka kwake, naye ndiye alinituma.”
Moi, je le connais; car je viens de sa part, et c'est lui qui m'a envoyé.
30 Ndipo wakatafuta kumkamata, lakini hakuna mtu yeyote aliyethubutu kumshika kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijawadia.
Ils cherchaient donc à se saisir de lui; mais personne ne mit la main sur lui, parce que son heure n'était pas encore venue.
31 Nao watu wengi wakamwamini, wakasema, “Je, Kristo atakapokuja, atafanya miujiza mikuu zaidi kuliko aliyoifanya mtu huyu?”
Cependant, plusieurs du peuple crurent en lui, et disaient: Quand le Christ viendra, fera-t-il plus de miracles que n'en fait celui-ci?
32 Mafarisayo wakasikia watu wakinongʼona mambo kama hayo kuhusu Yesu, ndipo wao pamoja na viongozi wa makuhani wakatuma walinzi wa Hekalu waende kumkamata.
Les pharisiens, ayant appris ce que le peuple disait sourdement de lui, envoyèrent, de concert avec les principaux sacrificateurs, des sergents pour se saisir de lui.
33 Yesu akasema, “Mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo, kisha nitarudi kwake yeye aliyenituma.
C'est pourquoi Jésus leur dit: Je suis encore avec vous pour un peu de temps; et je m'en vais à celui qui m'a envoyé.
34 Mtanitafuta lakini hamtaniona, nami niliko ninyi hamwezi kuja.”
Vous me chercherez, et vous ne me trouverez point, et vous ne pourrez venir où je suis.
35 Wayahudi wakaulizana wao kwa wao, “Huyu mtu anataka kwenda wapi ambako hatuwezi kumfuata? Je, anataka kwenda kwa Wayunani ambako baadhi ya watu wetu wametawanyikia, akawafundishe Wayunani?
Les Juifs dirent donc entre eux: Où ira-t-il que nous ne le trouverons point? Ira-t-il vers ceux qui sont dispersés parmi les Grecs, et enseignera-t-il les Grecs?
36 Yeye ana maana gani anaposema, ‘Mtanitafuta lakini hamtaniona,’ na, ‘nami niliko ninyi hamwezi kuja’?”
Que signifie ce qu'il a dit: Vous me chercherez, et ne me trouverez point, et vous ne pourrez venir où je suis?
37 Siku ile ya mwisho ya Sikukuu, siku ile kuu, wakati Yesu akiwa amesimama huko, akapaza sauti yake akasema, “Kama mtu yeyote anaona kiu na aje kwangu anywe.
Le dernier et le grand jour de la fête, Jésus se trouvait là, et s'écriait: Si quelqu'un a soif, qu'il vienne à moi, et qu'il boive.
38 Yeyote aniaminiye mimi, kama Maandiko yasemavyo, vijito vya maji ya uzima vitatiririka ndani mwake.”
Celui qui croit en moi, des fleuves d'eau vive couleront de son sein, comme dit l'Écriture.
39 Yesu aliposema haya alimaanisha Roho Mtakatifu ambaye wote waliomwamini wangempokea, kwani mpaka wakati huo, Roho alikuwa hajatolewa, kwa kuwa Yesu alikuwa bado hajatukuzwa.
(Or, il dit cela de l'Esprit que devaient recevoir ceux qui croiraient en lui; car le Saint-Esprit n'avait pas encore été donné, parce que Jésus n'était pas encore glorifié. )
40 Waliposikia maneno hayo, baadhi ya watu miongoni mwa ule umati wakasema, “Hakika huyu ndiye yule Nabii.”
Plusieurs de la foule, ayant entendu ces paroles, disaient: Celui-ci est véritablement le prophète.
41 Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine wakauliza, “Je, Kristo kwao ni Galilaya?
D'autres disaient: C'est le Christ. Et d'autres disaient: Mais le Christ vient-il de Galilée?
42 Je, Maandiko hayasemi kwamba Kristo atakuja kutoka jamaa ya Daudi na kutoka Bethlehemu, mji alioishi Daudi?”
L'Écriture ne dit-elle pas que le Christ sort de la postérité de David, et du bourg de Bethléhem d'où était David
43 Kwa hiyo watu wakagawanyika kwa ajili ya Yesu.
Le peuple était donc partagé à son sujet.
44 Baadhi yao walitaka kumkamata, lakini hakuna aliyethubutu kumgusa.
Et quelques-uns d'entre eux voulaient le saisir; mais personne ne mit la main sur lui.
45 Hatimaye wale walinzi wa Hekalu wakarudi kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo waliokuwa wamewatuma ili kumkamata Yesu, wakaulizwa, “Mbona hamkumkamata?”
Les sergents retournèrent donc vers les principaux sacrificateurs et les pharisiens, qui leur dirent: Pourquoi ne l'avez-vous pas amené?
46 Wale walinzi wakajibu, “Kamwe hajanena mtu yeyote kama yeye anenavyo.”
Les sergents répondirent: Jamais homme n'a parlé comme cet homme!
47 Mafarisayo wakajibu, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
Les pharisiens leur dirent: Avez-vous aussi été séduits?
48 Je, kuna kiongozi yeyote au mmoja wa Mafarisayo ambaye amemwamini?
Y a-t-il quelqu'un des chefs ou des pharisiens qui ait cru en lui?
49 Lakini huu umati wa watu wasiojua Sheria ya Mose, wamelaaniwa.”
Mais cette populace, qui n'entend point la loi, est exécrable.
50 Ndipo Nikodemo, yule aliyekuwa amemwendea Yesu siku moja usiku, ambaye alikuwa mmoja wao akauliza,
Nicodème (celui qui était venu de nuit vers Jésus, et qui était l'un d'entre eux) leur dit:
51 “Je, sheria zetu zinaturuhusu kumhukumu mtu kabla ya kumsikiliza na kufahamu alilotenda?”
Notre loi condamne-t-elle un homme sans l'avoir entendu auparavant, et sans savoir ce qu'il a fait?
52 Wakamjibu, “Je, wewe pia unatoka Galilaya? Chunguza nawe utaona kwamba hakuna nabii atokae Galilaya!” [
Ils lui répondirent: Es-tu aussi Galiléen? Examine, et vois qu'aucun prophète n'est sorti de la Galilée.
53 Kisha wakaondoka, kila mtu akarudi nyumbani kwake.
Et chacun s'en alla dans sa maison.